Ghosryder
JF-Expert Member
- Jul 6, 2014
- 10,308
- 4,294
Ukisikia uonevu wa polisi Tanzania basi hii hapa ni ya mwaka! Chama cha CCM inabidi ijipange kuhususiana na watendakazi wake. Raia hawatawavumilia tena. Kesi za uonevu na unyanyasaji zimezidi! . Kuna mshikaji wangu mmoja anaishi huko majuu marekani. Alikuja likizo kumuona mkewe. Wife akawa anaendesha gari maeneo ya Ubungo, ghafla polisi akawasimamisha na kumuomba leseni. Baada ya huyo mama kumpa leseni, huyo polisi hapo hapo akasimamisha madereva wengine watatu. Ghafla alifika dada mwingine, matokeo yake akamsimamisha, na kuingia kwenye gari lake na kuongozona naye akidai wanakwenda kituoni. Hapa ana leseni ya watu wanne. Hao wengine wote wakaambiwa wamfuate kkwenda Ubungo Bus Terminal Police. Walipofika hapo kituoni, polisi mwenyewe hakawa hayupo kumbe lile gari alilopanda alimalizana na dereva wake njiani. Basi wote waliokuwa wakidai leseni zao wakaondoka.
Baada ya kurudi kesho yake, huyo traffic akawa hayupo tena, jamaa na mkewe wakaondoka. Baada ya wiki tena, huyo mama akarudi mtu mzima akarudi kutafuta leseni yake, bahati nzuri akamkuta yule polisi sasa. Akaambiwa atoe laki tatu ili asamehewe Tsh. 300,000. Mama akashtuka aksema hana hela, basi wakamuomba laki na nusu. Mama akakataa, basi hapo hapo. Wale polisi wakaamua kumbambia kesi ya kutanua na kumuingiza mama wa watu Sero na waalifu wengine vibaka, majambazi nk... (hii ni wiki moja baadae, na mama kaja mwenyewe kutafuta leseni yake). Huyu mama alikuwa na $1,900 taslimu siku hiyo alizoachiwa na mumewe kwa ajili ya shuguli zao a kimaendeleo. Basi wakati wa kuzikabidhi hizo hela, akaomba kumjua jina anayekabidhiwa. Kosa kuuliza, akabambikiziwa kesi nyingine ya kashfa dhidi ya polisi na tayari hapa walishagawana hizo $1,900. Mama wa watu, mtu mzima akakaa sero kwa siku nzima bila kosa akiambiwa kesho anapelekwa mahakamani, mtu aliyeondoka nyumbani kwake kuja kuchukua leseni yake aliompa polisi kwenye routine check ya kwaida, matokeo yake kuswekwa ndani.
Bahati yake ikawa kuomba simu yake kuwataarifu ndugu zake kuhusu mkasa uliomkuta. Baada ya kumpigia mumewe, bahati nzuri mume ana ukaribu na Kamanda Kova. Mume akampigia Kova, naye Kova kampigia mkuu wa trafiki wa mkoa haraka haraka kuzima hii kashfa. Sasa kumbe shemeji yake huyu dada ni mtu mkubwa sana TAKUKURU. Shemeji mtu wa TAKUKURU akaenda moja kwa moja hadi Ubungo Terminal Police Station. Polisi wakawa hawajui nani kaja pale wakaanza kumchimba mkwara, kumbe wanachimbia bosi mkubwa sana wa taukururu. huyu bosi wa TAKUKURU na ile tabia ya kulindana na wakuu wa polisi, naye pia kazima hii skendo kutokana na ombi la mkuu wa trafiki..... Mimi niliposimuliwa nikabaki mdomo wazi. Ikiwa watu wakubwa wanafanyiwa hivi watu wa kawaida je? Mimi na wewe tukikamatwa itakuwaje? kwa maana hawa polisi walipoona mambo yamekuwa magumu, wakaanza kumfukuza huyo mama aondoke hapo kituoni haraka sana.... yaani basi tu. Ila najiuliza maswali machache
-Mtu anakuja kudai haki yake, anakamatwa na kuwekwa sero na wahalifu sugu kama majambazi na wauaji?
-Rushwa inakuwa ya kulazimisha, wakuu wanataarifiwa lakini hawachukui hatua, nchi inaelekea wapi?
-Wakuu wao wanataarifiwa kuhusu uhuni kama huu alafu wanazima skendo, bila ya kuwawajibisha hawa polisi wasio na nidhamu? Kova kaletewa kesi kama hii, Polisi wa Ubungo Terminal kufanya uchafu kama huu, alichukua hatua gani dhidi ya hawa vibaka ndani ya jeshi lake, au kuuzima kwa kumuachia huyo mama ndio mambo kwisha, na hela zake je??
C.C.M inafanya nini dhidi ya hawa watendaji wake, has apolisi wasio na nidhamu? Kamanda Lema kayazungumzia haya majuzi Bungeni lakini tunaona wanamagmba hawasikii. Hatutakubali uonevu kama huu, mrudishieni huyu mama hela zake. $1,900 ni nyingi sana kumnyang'angya mtu
IGP Mwema,
Cmdr. Kova,
Fuatilieni huu mkasa na kuwawajibisha hawa polisi wa Ubungo Terminal kabla haujaingia kwenye media. Hii ni skendo kubwa
Hii ishu mbona ilishaletwa humu jamvini kitaambo, yaani kuirudisha tena ni ajenda ya kutia pilipili kwenye swala la maandamano yenu ili watu wajazwe upepo wachukie polisi sana sio! Bavicha akili zenu sawa na za ng'ombe.