Uongozi Wetu Na Hatima Ya Tanzania - Je, Kutatokea Nini Katika Hatima Yake?!

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Nikiangalia ahadi zilizotolewa na Mh. Rais Kikwete na muda uliopita tangu orodha hizi za mambo yanayowakera Watanzania zitolewe, kinamna fulani naanza kuhisi kuwa, utabiri wa Mwl. Nyerere (RIP) katika kitabu chake unatimia. Walau pole pole katika ahadi zisizo tekelezeka kiuongozi hapa nchini.

-Orodha ya wala rushwa ninayo....
-Orodha ya wauza unga ninayo....
-Orodha ya majambazi ninayo.....
-
-
-

--------------------------------------------------

Kama orodha hapo juu inazidi kurefuka bila kuona jambo kubwa linatendeka katika kutatua kero hizi za Watanzania, naanza kushikwa na wasiwasi mkubwa na kujiuliza, hatima ya Tanzania itakuwaje iwapo maswala kama haya yanayo walenga wananchi moja kwa moja hayatekelezeki? Ni urefu gani 'orodha hii ya orodha' itafikia ndipo tutaona matunda ya mojawapo ya orodha iliyomo? Tukitafakari yaliyotendeka wakati wa Mh. Mwinyi na Mh. Mkapa, hatima ya Tanzania itakuwa ipi iwapo orodha ya viongozi wetu nayo itazidi kurefuka bila kuona Tanzania inabadilika kwa hali ya juu katika nyanja zake mbalimbali?


SteveD.
 
"Magufuli aliwatahadharisha wakurugenzi watakaokaidi agizo hilo na kuendelea kuwabomolea wakazi wa maeneo yasiyopimwa na kueleza kuwa watakaokaidi agizo hilo watajifunza kwa kuwekwa ndani.

Aidha, aliwataka wakurugenzi hao kuacha kumpelekea barua za mapendekezo ya kubadilisha matumizi ya ardhi ya maeneo ya wazi na kudai kwamba watakaofanya hivyo, atazituma barua zao moja kwa moja kwa Rais Jakaya Kikwete na kusisitiza kuwa hatobadilisha hati hizo kama wanavyotaka."


Na hii ajitayarishe kupokea pia ya Wakurugenzi. Hadi 2010 mbona balaa kwa orodha!
 
Nikiangalia ahadi zilizotolewa na Mh. Rais Kikwete na muda uliopita tangu orodha hizi za mambo yanayowakera Watanzania zitolewe, kinamna fulani naanza kuhisi kuwa, utabiri wa Mwl. Nyerere (RIP) katika kitabu chake unatimia. Walau pole pole katika ahadi zisizo tekelezeka kiuongozi hapa nchini.

-Orodha ya wala rushwa ninayo....
-Orodha ya wauza unga ninayo....
-Orodha ya majambazi ninayo.....
-
-
-

--------------------------------------------------

Kama orodha hapo juu inazidi kurefuka bila kuona jambo kubwa linatendeka katika kutatua kero hizi za Watanzania, naanza kushikwa na wasiwasi mkubwa na kujiuliza, hatima ya Tanzania itakuwaje iwapo maswala kama haya yanayo walenga wananchi moja kwa moja hayatekelezeki? Ni urefu gani 'orodha hii ya orodha' itafikia ndipo tutaona matunda ya mojawapo ya orodha iliyomo? Tukitafakari yaliyotendeka wakati wa Mh. Mwinyi na Mh. Mkapa, hatima ya Tanzania itakuwa ipi iwapo orodha ya viongozi wetu nayo itazidi kurefuka bila kuona Tanzania inabadilika kwa hali ya juu katika nyanja zake mbalimbali?


SteveD.

Kati ya falsafa kubwa ya nyerere nitakayokumbuka maisha yangu yote hi ile ya elimu ya watu wazima alipokuwa akinyooshea kidole akisema "Nenda kasome wakati ni huu."


J. K. I. Kwete anatumia opportnunity ya kuwa watanzania wengi hawakuitikia mwito ule wa Nyerere kwa hiyo wengi wao hawaoni pumba na mchele.
 
Kati ya falsafa kubwa ya nyerere nitakayokumbuka maisha yangu yote hi ile ya elimu ya watu wazima alipokuwa akinyooshea kidole akisema "Nenda kasome wakati ni huu."


J. K. I. Kwete anatumia opportnunity ya kuwa watanzania wengi hawakuitikia mwito ule wa Nyerere kwa hiyo wengi wao hawaoni pumba na mchele.

Hivi hatuwezi fanya lolote kwa sasa kuwasaidia waone??
Mie nazidi kuwaalika wana JF na watanzania wenzangu popote mlipo.. hebu tuchangamke tuwaonyeshe wenzetu ambao hawakubahatika kuona, hebu tuwasimulie na ya waingie hasa hukooooo vijijini kwetu, Naamini tukiwa na umoja wa siafu/mchwa ''swarm intelligence'' niki kunukuu mkuu kichuguu?? tutafanikiwa.
 
Back
Top Bottom