Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
Nikiangalia ahadi zilizotolewa na Mh. Rais Kikwete na muda uliopita tangu orodha hizi za mambo yanayowakera Watanzania zitolewe, kinamna fulani naanza kuhisi kuwa, utabiri wa Mwl. Nyerere (RIP) katika kitabu chake unatimia. Walau pole pole katika ahadi zisizo tekelezeka kiuongozi hapa nchini.
-Orodha ya wala rushwa ninayo....
-Orodha ya wauza unga ninayo....
-Orodha ya majambazi ninayo.....
-
-
-
--------------------------------------------------
Kama orodha hapo juu inazidi kurefuka bila kuona jambo kubwa linatendeka katika kutatua kero hizi za Watanzania, naanza kushikwa na wasiwasi mkubwa na kujiuliza, hatima ya Tanzania itakuwaje iwapo maswala kama haya yanayo walenga wananchi moja kwa moja hayatekelezeki? Ni urefu gani 'orodha hii ya orodha' itafikia ndipo tutaona matunda ya mojawapo ya orodha iliyomo? Tukitafakari yaliyotendeka wakati wa Mh. Mwinyi na Mh. Mkapa, hatima ya Tanzania itakuwa ipi iwapo orodha ya viongozi wetu nayo itazidi kurefuka bila kuona Tanzania inabadilika kwa hali ya juu katika nyanja zake mbalimbali?
SteveD.
-Orodha ya wala rushwa ninayo....
-Orodha ya wauza unga ninayo....
-Orodha ya majambazi ninayo.....
-
-
-
--------------------------------------------------
Kama orodha hapo juu inazidi kurefuka bila kuona jambo kubwa linatendeka katika kutatua kero hizi za Watanzania, naanza kushikwa na wasiwasi mkubwa na kujiuliza, hatima ya Tanzania itakuwaje iwapo maswala kama haya yanayo walenga wananchi moja kwa moja hayatekelezeki? Ni urefu gani 'orodha hii ya orodha' itafikia ndipo tutaona matunda ya mojawapo ya orodha iliyomo? Tukitafakari yaliyotendeka wakati wa Mh. Mwinyi na Mh. Mkapa, hatima ya Tanzania itakuwa ipi iwapo orodha ya viongozi wetu nayo itazidi kurefuka bila kuona Tanzania inabadilika kwa hali ya juu katika nyanja zake mbalimbali?
SteveD.