Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Katika hali ya Kushangaza Hospitali inayotajwa kuwa ni ya Wilaya ya Chato ( kwa Magufuli) kuna utata mkubwa kuhusu wahudumu walioko Hospitali hapo kuwapatia huduma wagonjwa. Wagonjwa wengi wanaotoka pale wanajiuliza ni kwa nini ile isiitwe tu lituo cha afya. Waganga na Manesi waliopo hawana kabisa moyo wa kuwahudumia wagonjwa. Wanaolalamika sana ni wale ambao wanaishi na virusi vya Ukimwi pindi wanapolazwa kupata huduma ni kwa tabu kwa sababu wao hawalipi. Watu wanapoteza maisha hivihivi.Wanaopata huduma pale au sie wana Chato tuna tabu, anayetaka kuhakikisha aende kimya kimya aingie wodini aone kinachoendelea na ikiwezekana awahoji walioko wodini ndo mtaamini maneno wanayoyasema. Siku hizi hatuna madaktari kama wa zamani. Siku hizi kuna madaktari - maaskari, wauguzi - mgambo. Yaani hawa watu utu hakuna wao wanataka pesa. Hakuna wanachofanya.
Kuna walioshuhudia wagonjwa wakifa kwa Pneumonia, wanajiuliza hospitali ( ya Wilaya) haina Oxygen Machine? Mwingine anatoka Thietre kafunukiwa nguo zake za nyumbani je hakuna hata Shuka safi la hospitali la kumfunika? Ni nini wanataka hawa wauguzi ili wawatibu Watanzania hawa. Mkuu Magufuli alivyokuwa serious kwenye mambo ya utendaji, lakini kwake huku watu wanastarere wagonjwa wanaangaika kisa huduma ni bure ( kwa wanaoishi na vvu), Swali najiuliza hata wale wanaolipa kwani fedha zinaingia mifukoni mwa wauguzi? Si zinalipiwa dirishani? au baadae wanakutana wanagawana? Kwa ujumla huduma ni mbovu anayetaka kuhakikisha hili aende Chato awaulize wananchi, waliowahi kulazwa pale au waliolazwa sasa watakueleza kilio kilichoko hapo lakini Uongozi kimya.
Wito wangu kwa Viongozi wa juu wa Serikali, kama mwananchi njooni mfanye uchunguzi mjionee, hali si Shwari. Fanyeni ukaguzi wa ghafla mtashangaa!!!! Wauguzi ni wengi lakini kinachofanyika hakionekani. Tatizo la nchi hii tukieleza matatizo ya wananchi utasikia wahusika wanasema leta ushahidi. Ushahidi upi? manataka mareremu aliyepoteza maisha kwa kukosa huduma afufuke atoe ushahidi? Kawaulizeni wananchi ndo mpate ushahidi. Ndo maana Msanii aitwaye ROMA aliimba kuwa wagonjwa wanakufa huku doctor anakunywa Valeur. Jamani viongozi chukueni hatua.
Kuna walioshuhudia wagonjwa wakifa kwa Pneumonia, wanajiuliza hospitali ( ya Wilaya) haina Oxygen Machine? Mwingine anatoka Thietre kafunukiwa nguo zake za nyumbani je hakuna hata Shuka safi la hospitali la kumfunika? Ni nini wanataka hawa wauguzi ili wawatibu Watanzania hawa. Mkuu Magufuli alivyokuwa serious kwenye mambo ya utendaji, lakini kwake huku watu wanastarere wagonjwa wanaangaika kisa huduma ni bure ( kwa wanaoishi na vvu), Swali najiuliza hata wale wanaolipa kwani fedha zinaingia mifukoni mwa wauguzi? Si zinalipiwa dirishani? au baadae wanakutana wanagawana? Kwa ujumla huduma ni mbovu anayetaka kuhakikisha hili aende Chato awaulize wananchi, waliowahi kulazwa pale au waliolazwa sasa watakueleza kilio kilichoko hapo lakini Uongozi kimya.
Wito wangu kwa Viongozi wa juu wa Serikali, kama mwananchi njooni mfanye uchunguzi mjionee, hali si Shwari. Fanyeni ukaguzi wa ghafla mtashangaa!!!! Wauguzi ni wengi lakini kinachofanyika hakionekani. Tatizo la nchi hii tukieleza matatizo ya wananchi utasikia wahusika wanasema leta ushahidi. Ushahidi upi? manataka mareremu aliyepoteza maisha kwa kukosa huduma afufuke atoe ushahidi? Kawaulizeni wananchi ndo mpate ushahidi. Ndo maana Msanii aitwaye ROMA aliimba kuwa wagonjwa wanakufa huku doctor anakunywa Valeur. Jamani viongozi chukueni hatua.