Salaam Alekuim.
Katika siku za karibuni kumekuwa na maneno,malalamiko mengi juu ya uongozi wa Rais Samia Suluhu katika mitandao ya kijamii na mitaani.
Rai yangu kama watanzania ili tusonge mbele pamoja tubadilike na kuacha hizi lawama na malalamiko yasiyo na tija kwa uongozi wa Rais Samia.
Uongozi wa mama Samia unafanya mengi na kwa dhati kurekebisha na kuendeleza nchi kiuchumi,kisiasa na kijamii hivyo sisi kama wadau hatuna budi kuchangia mawazo yetu chanya na kukosoa kwa Nia ya kurekebisha lakini sio hivi inavyofanyika katika siku za karibuni. Kwani kufanya hivyo sio tu ni kukosa heshima kwa uongozi na kukatisha tamaa bali vile vile tunazalisha nyongo mbaya kwa vizazi vijavyo na kuzalisha taifa lilokosa matumaini.
Na katika kujenga tunapokosoa tutoe na mbinu mbadala za kuboresha naamini uongozi kwa hivyo watayachukua na kuyafanyia kazi.
Mwisho tuwe na Imani uongozi wa mama wanafanya kazi nzuri ndio maana yote yalioanzishwa na Marehemu JPM wanayaendeleza.
Tubadilike tuwe na misamamo chanya
Katika siku za karibuni kumekuwa na maneno,malalamiko mengi juu ya uongozi wa Rais Samia Suluhu katika mitandao ya kijamii na mitaani.
Rai yangu kama watanzania ili tusonge mbele pamoja tubadilike na kuacha hizi lawama na malalamiko yasiyo na tija kwa uongozi wa Rais Samia.
Uongozi wa mama Samia unafanya mengi na kwa dhati kurekebisha na kuendeleza nchi kiuchumi,kisiasa na kijamii hivyo sisi kama wadau hatuna budi kuchangia mawazo yetu chanya na kukosoa kwa Nia ya kurekebisha lakini sio hivi inavyofanyika katika siku za karibuni. Kwani kufanya hivyo sio tu ni kukosa heshima kwa uongozi na kukatisha tamaa bali vile vile tunazalisha nyongo mbaya kwa vizazi vijavyo na kuzalisha taifa lilokosa matumaini.
Na katika kujenga tunapokosoa tutoe na mbinu mbadala za kuboresha naamini uongozi kwa hivyo watayachukua na kuyafanyia kazi.
Mwisho tuwe na Imani uongozi wa mama wanafanya kazi nzuri ndio maana yote yalioanzishwa na Marehemu JPM wanayaendeleza.
Tubadilike tuwe na misamamo chanya