Uongozi wa Chuo cha Afya Tanga, fanyeni kazi kwa weledi

Status
Not open for further replies.

The Spirit of Tanzania

JF-Expert Member
Mar 7, 2020
537
928
Nina vijana wangu wamepata nafasi chuo cha afya tanga moja kwa moja kutoka kidato cha nne.

Katika mambo yalilonishangaza ni kama ifuatavyo:

1. Suala la chakula mwanafunzi anatakiwa kujitegemea ila kwenye form ya kujiunga hawajaandika kabisa habari hii.

2. Chuo kutoza fedha ya kujiunga NACTE baada ya kuwa mwanafunzi amefika chuoni hali amechaguliwa moja kwa moja na wizara

3. Baadhi ya walimu hawafundishi kwa kufata vipindi, sasa inafika wakati wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanafundishwa kuanzia asubuhi saa 12 hadi saa 2 usiku, hivi hapa mnaandaa wataalamu wa afya kweli au mnataka kuonekana mmefundisha?

4. Bima ya afya kutotolewa kwa wanafunzi kwa wakati, inafikia muda mwanafunzi anaumwa anatumia gharama zake kujitibu hali amelipia bima ya afya.

5. Form ya kujiunga haiko wazi na ni kama kuna gharama zisizo za lazima, ile form ya kujiunga chuo hiki ni scanned copy, halafu imewekwa kwenye mtandao, mtu wa IT chuo hiki hayuko makini kabisa, pia kuna fedha imeandikwa fedha ya michezo, hivi kweli mnaibia watanzania waziwazi kwa kuita fedha ya michezo? Kama mwanangu hachezi mchezo wowote kutokana na afya yake kwanini nilipie?

TAFADHALI, UONGOZI WA CHUO HIKI ANGALIENI, WAZAZI WENGI TUMEUMIA MWAKA HUU KWA UBOVU WA MUUNDO WENU.
 
Wazee wa Lawama kazini😂

1. Vyuo vya Afya vya serikali vyote, mwanafunzi anajitegemea chakula
2. Vyuo vya Afya vyote vya Umma ambavyo viko chini ya wizara ya Afya, Joining Instructions zinafanana kila kitu
3. BIMA (NHIF) ndo kwanza vyuo vimefunguliwa November ushaanza kulalamika muda huu?
4. Kuhusu masomo... ongea na wanao wasome kweli kweli waache kulialia, Vinginevyo hawatavuka Level 4

NB: Nimetoa maoni yangu kama mwananchi wa kawaida tu anayeishi Tanga na anayejua ubora wa Elimu ya Chuo hicho cha Bombo
 
Uzi mwingine nimetoka kuona hapa jamaa anawalaumu NACTE wanafunzi wamefeli sana mwaka huu!

Hali ya Baba wa Taifa ni Mbaya!
Mkapa 1999
 
Hakuna lawama ya msingi hata moja hapo, ushauri wangu km inawezekana abadilishe kozi mara moja, kwa hoja hizo hapo juu hatoboi
 
Duh pole mkuu ila ndo Ivo kijana wacha akaze vingine msikilize tu mwambie utavifanyia kazi.

Kwanza ajue kabisa hicho ni chuo tena cha afya ko sio lelemama kama kule olevel....
pili sidhani kama wanasoma kuanzia hiyo saa mbili mpaka usiku wanasoma tuuuuuuuuuuuu.....
hapa kuna kauchumvi kidogo..
Issue ya bima ndo Kwanza vyuo vimefunguliwa na vyuo kibao karibu nchi nzima vinaomba hizo bima Kwa ajili ya vijana wao ....ko awe mvumilivu kidogo japo nafikiri kuna utaratibu wa kutibiwa muda huu ukiwa unasubir kuletewa bima zenu aulizie...

kijana akaze awache ujanja ujanja na kulalamika sana ....maana hasomi peke yake hapo wapo na wengine....changamoto zipo taratibu ata adapt...
 
Asante kwa kuchangia,ila umesema uwazavyo,uwe na kijana achaguliwe direct hapo ndio utaweza kuona nina hoja au malalamiko.
Kama chuo kiko makini kwanini hawakusema wazi kuwa chakula ni kujitegemea?,
Kwanini vyuo vingine vimefungua November hiyohiyo ila ukiugua hauambiwi kujitegemea?,na ungejua kuhusu hiki chuo cha tanga wanafunzi wanalipa bima ila kuna wakati wanakaa mwaka mzima bila kupata kadi ya bima.
hapa sijasema lolote kuhusu ubora wa elimu ya hiki chuo,nasema haya uliyoshindwa kuona.
Mkuu hili la vyuo hata wewe mwenyewe ulifaa ulifanyie utafiti kabla hata kijana hajakwenda kuripoti .....
vyuo vingi kama si vyote issue ya chakula ni kujitegemea.....

Issue ya matibabu anasema kwamba inabidi "ajitegemee" ni maneno kaenda mwenyew ofisini ama ya kuambiwa na alowakuta ...

na Hilo la bima ya afya ni amesikia Tu kwamba maneno ya kuambiwa ama ...maana umesema ndo kaenda report... na ukitazama vizur kijana amegusa karibu kila sekta chakula, afya, masomo

usikiattack chuo direct na kuweka negativity nyingi Sana ....
Em jaribu kukaa na kijana umsikilize vizuri ....ujue je anataka kusoma hiko chuo au hiyo kozi ama hataki kuna anachotaka yeye labda umemlazimisha.....
halafu pia jaribu upate mawasiliano direct na wahusika chuo uwaulize mwenyewe ikiwezekana upate ufafanuzi yakinifu directly kutoka Kwa wahusika.
usije kuta umekichukia chuo na uongozi kumbe ni "maneno ya kuambiwa"
 
Pole,vyuo vyote vya serikali chakula ni kujitegemea ingawa awamu hii walipanga kuwe na chakula mchana lakini mambo si shwari hapasomeki.
Bima ya afya inategemea na utoaji wa wanafunzi maana pesa zote za wanafunzi zinakusanywa na kupelekwa ofisi ya bima husika wao ndiyo wanaotengeneza vitambulisho vya bima kwahiyo kama makusanyo hayajatolewa na wanafunzi wote hapo ukiumwa lazima utajitegemea. Kusoma toka asubuhi mpaka jioni usishangae waalimu wanakimbizana na ratiba waliyopewa na wizara wakamilishe ratiba kwa kipindi walichoambiwa. Waambie watoto wakaze msuli tu utaalamu wataupata
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom