Uongozi wa CHADEMA Taifa unaisha muda wake siku ya Ijmaa tarehe 14.09. 2019

Taarifa nilizodokezwa kutoka ndani ya CHADEMA ni kwamba uongozi wa chama hicho Taifa unaisha muda wake siku ya ijmaa tarehe 14.09. 2019 na kama hawajafanya uchaguzi msajili wa vyama siasa Nchini atalazimika kukifuta chama hicho au kukitaka kisitishe shughuli za kisiasa Nchini.

Hata hivyo viongozi wake akiwemo mwenyekiti Freeman Mbowe na Dr Mashinji wapo kimya na hakuna dalili zozote za kuitisha uchaguzi hivi karibuni jambo litakalohalalisha kufutiwa usajili.
My Take: Yale Yale ya kupuuza katiba ya Nchi.
Choma moto ofisi ya msajili. Thubutu!
 
Mbona ninyi mnataka mpoteze watu kisa miaka kumi eti akichaguliwa term ya kwanza kusiwe na wa kumpinga term inayofuata demokrasi ipo?
Yani ulichoandika hapa ukilinganisha na mada ni mbingu na ardhi!
Any way watu kama nyie ndio mataji wa Mbowe kuendelea kuwa Mugabe hapo chadema
 
Naunga mkono hoja! Chadema kama chama kikuu cha upinzani na chama kinachoamini kwenye Demokrasia na Maendeleo, hawana budi kuwa mfano wa kuigwa!

Muda wa Mwenyekiti wa sasa kimsingi ulitakiwa kufikia kikomo mwaka 2014, kwa kuongoza mihula miwili! lakini katika hali ya kushangaza aliongezewa muhula mwingine.

Kwa sasa hakuna namna, unatakiwa ufanyike uchaguzi wa ndani na mwenyekiti wa sasa awaachie vijana wa kumhenyesha Magufuli na pia kwa ajili ya kurudisha mvuto kwa hili kundi la vijana ambalo ni muhimu sana kwenye ujenzi wa chama.

Iwapo mh.Mbowe ataendelea kuwa mwenyekiti, mtawapa ccm kiburi cha kuanzisha mchakato wa Rais wa sasa kutawala maisha! Maana chama kitakosa nguvu ya kukemea hali hiyo kama kilivyoshindwa kwenye hoja ya ufisadi baada tu ya kumpokea mh. Lowassa kuwa mgombea urais mwaka 2015 na wakati hapo awali walimtuhumu kama mmoja wa mafisadi nchini.

Katibu Mkuu amepwaya sana, na ni ukweli uliowazi ameshindwa kuvaa viatu vya Dr. Slaa! Mwenyekiti mpya aje na timu yake. Mbinu za mapambano zinatakiwa zibadilishwe! Mbinu ya kuvaa magwanda kupambana na ufisadi, kwa awamu hii siyo rafiki. Jk alikuwa ni mwanasiasa aliyekomaa kuliko huyu tuliye naye hivyo ni lazima uongozi mpya ubadilishe.

Ujenzi wa Ofisi za makao makuu ya chama na pia ofisi za mikoani na wilayani, ili kupunguza kejeli kutoka kwa wapinzani wenu ccm!

Chama kianzishe vyombo vyake vya habari mfano magazeti na kituo cha luninga ili kutangaza taarifa zenu muhimu maana awamu hii karibia vyombo vyote vya habari vimegeuzwa kuwa mali ya mtu mmoja na chama chake. Ni mwendo wa kusifia tu huku chadema wakionekana kwenye matukio hasi tu kama yale ya kusikilizwa kwa kesi zao za uchochezi, nk.

Ikibidi Mwenyekiti awamu hii atoke ukanda mwingine kabisa ili tu kuwaziba midomo wapinzani wenu wanaomini kwamba, chama kimeshikiliwa na watu wa kaskazini tu! na hivyo ni chama cha kikanda.

Chadema ni chama kikuu chenye ushawishi mwingi kwenye jamii hivyo hakina budi kupambana mwanzo mwisho. Kikifanya utani, kitarudi nyuma kwa hatua nyingi na hivyo kuwakatisha tamaa wapenda mabadiliko. Tafadhali, makamanda msije mkanishambulia kwa matusi, tujenge tu hoja.
Wenyewe wa nakwambia chadema mtu pekee asiye weza kuhongwa na ccm no Mbowe tu,
Kwamba kama ikatokea Mungu akamchukua Mbowe basi chadema kwisha.
 
Taarifa nilizodokezwa kutoka ndani ya CHADEMA ni kwamba uongozi wa chama hicho Taifa unaisha muda wake siku ya ijmaa tarehe 14.09. 2019 na kama hawajafanya uchaguzi msajili wa vyama siasa Nchini atalazimika kukifuta chama hicho au kukitaka kisitishe shughuli za kisiasa Nchini.

Hata hivyo viongozi wake akiwemo mwenyekiti Freeman Mbowe na Dr Mashinji wapo kimya na hakuna dalili zozote za kuitisha uchaguzi hivi karibuni jambo litakalohalalisha kufutiwa usajili.
My Take: Yale Yale ya kupuuza katiba ya Nchi.
Yaani Mbowe ana wanyima usingizi Lumumba na wakuu wake.. Hebu muacheni Mbowe bado sisi hatujui kama muda wake unaisha.
Hivi pilipili mauzo zila zawawashia nini?? Mwambieni jiwe aache kupendelea kanda. Sote ni watanzania
 
Hivi mbowe kuongoza chdma kwann ni pasua kichwa ka ma CCM? Tangu lini adui yako akakuombea mazuri?
Mkuu mimi naona wewe unatuliza maswali yasiyo kuwa na majibu sijui tuna kwama wapi au tulilogwa na nani harafu wazee wa kukejeli huku nao wakibanwa mbavu nao watakuja kusingizia chadema roho mbaya na ubinafsi tu
 
Naunga mkono hoja! Chadema kama chama kikuu cha upinzani na chama kinachoamini kwenye Demokrasia na Maendeleo, hawana budi kuwa mfano wa kuigwa!

Muda wa Mwenyekiti wa sasa kimsingi ulitakiwa kufikia kikomo mwaka 2014, kwa kuongoza mihula miwili! lakini katika hali ya kushangaza aliongezewa muhula mwingine.

Kwa sasa hakuna namna, unatakiwa ufanyike uchaguzi wa ndani na mwenyekiti wa sasa awaachie vijana wa kumhenyesha Magufuli na pia kwa ajili ya kurudisha mvuto kwa hili kundi la vijana ambalo ni muhimu sana kwenye ujenzi wa chama.

Iwapo mh.Mbowe ataendelea kuwa mwenyekiti, mtawapa ccm kiburi cha kuanzisha mchakato wa Rais wa sasa kutawala maisha! Maana chama kitakosa nguvu ya kukemea hali hiyo kama kilivyoshindwa kwenye hoja ya ufisadi baada tu ya kumpokea mh. Lowassa kuwa mgombea urais mwaka 2015 na wakati hapo awali walimtuhumu kama mmoja wa mafisadi nchini.

Katibu Mkuu amepwaya sana, na ni ukweli uliowazi ameshindwa kuvaa viatu vya Dr. Slaa! Mwenyekiti mpya aje na timu yake. Mbinu za mapambano zinatakiwa zibadilishwe! Mbinu ya kuvaa magwanda kupambana na ufisadi, kwa awamu hii siyo rafiki. Jk alikuwa ni mwanasiasa aliyekomaa kuliko huyu tuliye naye hivyo ni lazima uongozi mpya ubadilishe.

Ujenzi wa Ofisi za makao makuu ya chama na pia ofisi za mikoani na wilayani, ili kupunguza kejeli kutoka kwa wapinzani wenu ccm!

Chama kianzishe vyombo vyake vya habari mfano magazeti na kituo cha luninga ili kutangaza taarifa zenu muhimu maana awamu hii karibia vyombo vyote vya habari vimegeuzwa kuwa mali ya mtu mmoja na chama chake. Ni mwendo wa kusifia tu huku chadema wakionekana kwenye matukio hasi tu kama yale ya kusikilizwa kwa kesi zao za uchochezi, nk.

Ikibidi Mwenyekiti awamu hii atoke ukanda mwingine kabisa ili tu kuwaziba midomo wapinzani wenu wanaomini kwamba, chama kimeshikiliwa na watu wa kaskazini tu! na hivyo ni chama cha kikanda.

Chadema ni chama kikuu chenye ushawishi mwingi kwenye jamii hivyo hakina budi kupambana mwanzo mwisho. Kikifanya utani, kitarudi nyuma kwa hatua nyingi na hivyo kuwakatisha tamaa wapenda mabadiliko. Tafadhali, makamanda msije mkanishambulia kwa matusi, tujenge tu hoja.
Wazo zuri sana,Mungu akubariki
 
Taarifa nilizodokezwa kutoka ndani ya CHADEMA ni kwamba uongozi wa chama hicho Taifa unaisha muda wake siku ya ijmaa tarehe 14.09. 2019 na kama hawajafanya uchaguzi msajili wa vyama siasa Nchini atalazimika kukifuta chama hicho au kukitaka kisitishe shughuli za kisiasa Nchini.

Hata hivyo viongozi wake akiwemo mwenyekiti Freeman Mbowe na Dr Mashinji wapo kimya na hakuna dalili zozote za kuitisha uchaguzi hivi karibuni jambo litakalohalalisha kufutiwa usajili.
My Take: Yale Yale ya kupuuza katiba ya Nchi.
ulisoma sheria chuo gani mkuu? chato au
 
Back
Top Bottom