Econometrician
JF-Expert Member
- Oct 25, 2013
- 15,778
- 28,423
Uongozi wa CCM muda bado mnaweza kufanya mabadiliko rudusheni utaratibu wa zamani ili kumpata mbunge bora, ule utaratibu wa mwanzo wa watu kupimwa kwanza na Kamati husika kabla ya kura za maoni ndio unafaa kisha zipatikane 3 bora zikapigiwe kura za maoni na Wajumbe wa Halmashauri ya Jimbo.
Utaratibu wa sasa unaotaka watia nia wote kupigiwa kura mbele ya wajumbe hatuwezi pata kiongozi bora maana huwezi weka watu wote let say 80 kama hao wa Jimbo la kawe katika ukumbi kisha kila mtu apate muda wa kujielezea na upate kilicho bora, ni kitu kisichowezekana.
Kwanza unawachosha wajumbe watia nia wajieleze 1-80 ni wazi wajumbe watakosa concentration, pili kura zinatakiwa zipigwe siku 1 tu huo muda uko wapi?
Duniani kote kunafanyika kwanza screening kupata walio bora kisha ndio wanashindanishwa, mazingira ya watu wengi kujitokeza kuliko ilivyo kadiriwa kunaharibu umaana wa zoezi hili.
Utaratibu wa sasa unaotaka watia nia wote kupigiwa kura mbele ya wajumbe hatuwezi pata kiongozi bora maana huwezi weka watu wote let say 80 kama hao wa Jimbo la kawe katika ukumbi kisha kila mtu apate muda wa kujielezea na upate kilicho bora, ni kitu kisichowezekana.
Kwanza unawachosha wajumbe watia nia wajieleze 1-80 ni wazi wajumbe watakosa concentration, pili kura zinatakiwa zipigwe siku 1 tu huo muda uko wapi?
Duniani kote kunafanyika kwanza screening kupata walio bora kisha ndio wanashindanishwa, mazingira ya watu wengi kujitokeza kuliko ilivyo kadiriwa kunaharibu umaana wa zoezi hili.