Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,791
Kuna kitu kinaitwa mizani, mizani ni kifaa cha kupimia kitu kwa vipimo vya kilo, mizani inazaa neno mizania. Mizani haitakiwi izidi upande wowote wa kile kinachopimwa. Ikizidi upande wowote kuna mmoja atafaidika na mwingine atapunjika, ikiwa kwenye urari sawia kila mtu atafaidika. Haki pia hupimwa kwenye mizania ya haki, ndio maana kwenye mahakama zetu na vyombo vya sheria hutumia picha ya kikaragosi cha mizani.
Simulizi za akina Yohana Mbatizaji na Yohana mtembezi zinatupa elimu ya mizania ya urari wa haki lakini kwa mitazamo yakinifu na tengeufu. Yohana Mbatizaji akijulikana kama mtume pia ni mtu mwenye simulizi nyingi mpaka kubadilika na kuwa nabii na Mbatizaji. Ametengeneza LEGACY mpaka leo hii kama kiwakilishi cha upendo, utu wema, unyofu wa moyo na kama njia ya wokovu kiimani, kwa wale wana imani na waamini. Yohana huyu ni kiwakilishi cha ulimwengu huru wa nuru.
Tuna huyu Yohani mwingine, Yohana mtembezi ama Yohana chapombe. Ni kutokana na mtu huyu mpaka leo tuna kilevi cha bei ghali, kitamu chenye arikohori ya kutosha tu, ametengeneza LEGACY yake pia.
Simulizi zinasema hapo zamani za kale huko Uskotishi kulikuwa na upungufu wa vileo na Yohana akiwa chapombe maarufu aliweza kutembea kwa miguu muda mrefu tu akisakanya kilevi.. Inasemekana (pengine ni utani tu) hakupenda kupanda gari ili aokoe pesa ya ulabu. Yohana huyu alitembea mji hadi mji akisaka kilevi pendwa. Ni kwa umaarufu wake huu kilizaliwa kileo kikali kiitwacho John Walker kikiwa na kikaragosi cha picha kwa muktadha wa jina. Yohana huyu ni kiwakilishi cha ulimwengu wa nira za starehe, vifungo na tamaa za mwili.
Yohana wa kwanza alizunguka miji mingi akihubiri na kubatiza watu, Yohana wa pili alizunguka miji mingi akitafuta ulabu....
Uongozi unaoacha alama. Unaacha alama gani? Zenye madoa meusi ya damu iliyokauka ama alama zenye rangi nzuri za kuvutia? Mizania ya uongozi unaoacha alama tutaupimaje? Utaegemea wapi? Kwenye haki ama kwenye dhuluma?
Ni sawa na kilio cha samaki machozi yameenda na maji, usifananishe na kilio cha mamba. Siku hizi watu wanatambulika kwa vimo vyao si majina wala vyeo vyao. Vimo! Asante Ally Hapi.
Uongozi unaoacha alama.Yohana Mbatizaji na Yohana mtembezi wote waliacha alama. Kuacha alama si tatizo... Je umeacha alama gani? Kukichwa kutambazuka lakini kabla jua halijachomoza kiza huwa totoro.
Simulizi za akina Yohana Mbatizaji na Yohana mtembezi zinatupa elimu ya mizania ya urari wa haki lakini kwa mitazamo yakinifu na tengeufu. Yohana Mbatizaji akijulikana kama mtume pia ni mtu mwenye simulizi nyingi mpaka kubadilika na kuwa nabii na Mbatizaji. Ametengeneza LEGACY mpaka leo hii kama kiwakilishi cha upendo, utu wema, unyofu wa moyo na kama njia ya wokovu kiimani, kwa wale wana imani na waamini. Yohana huyu ni kiwakilishi cha ulimwengu huru wa nuru.
Tuna huyu Yohani mwingine, Yohana mtembezi ama Yohana chapombe. Ni kutokana na mtu huyu mpaka leo tuna kilevi cha bei ghali, kitamu chenye arikohori ya kutosha tu, ametengeneza LEGACY yake pia.
Simulizi zinasema hapo zamani za kale huko Uskotishi kulikuwa na upungufu wa vileo na Yohana akiwa chapombe maarufu aliweza kutembea kwa miguu muda mrefu tu akisakanya kilevi.. Inasemekana (pengine ni utani tu) hakupenda kupanda gari ili aokoe pesa ya ulabu. Yohana huyu alitembea mji hadi mji akisaka kilevi pendwa. Ni kwa umaarufu wake huu kilizaliwa kileo kikali kiitwacho John Walker kikiwa na kikaragosi cha picha kwa muktadha wa jina. Yohana huyu ni kiwakilishi cha ulimwengu wa nira za starehe, vifungo na tamaa za mwili.
Yohana wa kwanza alizunguka miji mingi akihubiri na kubatiza watu, Yohana wa pili alizunguka miji mingi akitafuta ulabu....
Uongozi unaoacha alama. Unaacha alama gani? Zenye madoa meusi ya damu iliyokauka ama alama zenye rangi nzuri za kuvutia? Mizania ya uongozi unaoacha alama tutaupimaje? Utaegemea wapi? Kwenye haki ama kwenye dhuluma?
Ni sawa na kilio cha samaki machozi yameenda na maji, usifananishe na kilio cha mamba. Siku hizi watu wanatambulika kwa vimo vyao si majina wala vyeo vyao. Vimo! Asante Ally Hapi.
Uongozi unaoacha alama.Yohana Mbatizaji na Yohana mtembezi wote waliacha alama. Kuacha alama si tatizo... Je umeacha alama gani? Kukichwa kutambazuka lakini kabla jua halijachomoza kiza huwa totoro.