Uongozi si Kazi Rahisi; Understanding Mr. Mbowes position

Character X

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
331
382
ndugu zangu wana JF,
Habari,

Ninamshukuru Mungu mwingi wa rehema kwa wakati mzuri aliotupatia tena kushirikishana mawazo tofauti ilikutupatia ushiriki na uhai katika kuukabili mustakabali wa taifa letu hili tukufu pamoja na watu wake.

Ndugu zangu, Leo nikohapa kuyaleta mawazo yangu hasa juu ya dhana nzima ya UONGOZI nikiweka msingi juu ya presentation aliyo ifanya Mh. Freeman Mbowe, mwenyekiti wa Chama cha Democrasia na Maendeleo Taifa wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru 9/12/2013 land mark hotel.

Ndugu zangu Mh. Mbowe alieleza kwakirefu sana juu ya historia yake ndani ya chama na mchango wake mkubwa katika nafasi mbali mbali na hatimaye kama mwenyekiti wa kwanza wa Bavicha na mwenyekiti wa chadema taifa baadae.

Mh. Mbowe alieleza pia mchango wake mkubwa sana katika kutafuta viongozi wengine wakuisogeza CHADEMA karibu zaid na hatima yake iliyokusudiwa wakati wa kuundwa kwake.

Mheshimiwa alizungumza juu ya mchango wake wa kiushawishi na kimkakati uliyo fanikisha chadema kupata viongozi Makini wengi wakiwemo the likes of Mh. Lisu, Mh. Lema, Mh. Mdee, Mh. John mnyika na Mh. Zitto Zuberi Kabwe among others.

ndugu zangu, kazi aliyo ifanya Mh. Mbowe ni kubwa na inajidhihirisha kwa takwimu za mabadiliko makubwa in all levels kuanzia idadi ya wa wakilishi bungeni hadi idadi ya wanachama, kuanzia idadi ya mashina ya chama hadi idadi ya rasilimali za chama among many other aspects relevant.

Kwakazi hii nasema Mungu huchagua viongozi sahihi kulingana na hali ya wakati husika.

Kwakipindi hicho chote chamwanzo hadi sasa, chadema ilihitaji uongozi wa mtu makini lakini mgumu, jasiri, asiyeogopa, mkali na mwenye misimamo au kwalugha nyingine waweza kusema "mtu mbabe" ilikukisimamisha imara amidst strong opposition from the rulling CCM.
Kwakipindi hiki chote tulimuhitaji kiongozi wa mithili ya Mr. Mbowe na Mungu alitupatia Mbowe. Sasa hapa si kusema kwamba sasa hatumuhitaji tena No. Ila nataka kuonyesha tu kwamba he came to us at an opportune time.

kazi ya kusimamisha kitu dhaifu ama kitu kichanga kuwa organization kubwa na yente misingi imara na sahihi ni kazi ngumu sana sana sana kuliko wengi tunavyoweza kudhani.

Hii ndio kazi waliyo ifanya viongozi wetu wazee waliotuwekea misingi ya utaifa wetu. Mzee Mwalimu Nyerere, Ndugu Sokoine, Ndugu Sarakikya, Mzee Kawawa na wengine wengi hapa tanzania na akina Mandela na wenzake huko nje africa kwaujumla.

Kazi imefanyika, na kazi imeonekana!
Hongera sana Mr. Chairman.

However changamoto Hasa zimeanza kujitokeza, na hizi ndizo kipimo hasa cha uimara wa taasisi yetu.

Lakini hapa pia bila kusita maamuzi SAHIHI yalifanyika na kwawakati bila kuchelewa.
Hii imeleta kutoeleweka kwa mh. Mbowe kwa watu wengi. Lakini mimi masema,
Good job Mr. Chairman, uongozi ni jukumu gumu sana, uongozi wowote!!.

Siwengi wanaoweza kuelewa hili. They say it takes a leader to understand one!

however katika kumalizia niombe tu sasa kwamba hekima ikuongoze pia.,

Hapa tunahitaji kuvuka si salama tu, ila PAMOJA.

mimi naamini unaumia yanapotokea haya yanayotokea, lakini huenda unadhani hakuna namna inabidi yaende hivyo. Well, binafsi nadhani kwanafasi yako unaweza kuisimamia HAKI. Na kwamba, sio tu haki itendeke katika hili, laki haki IONEKANE ikitendeka katika hili,
Mh. Mwenyekiti bado upo umuhimu wakuhakikisha maamuzi yanafanyika juu ya taarifa zilizothibitishwa pasipo shaka kabisa lakini pia kwanidhamu na heshima ya utu na nafasi ya anaye kabiliwa na shutuma hizi, ikifika wakati sahihi taratibu sahihi zifuatwe kutoa adhabu yenye lengo la kufundisha na si kukomoa.

Katika hili mh. Mwenyekiti unayo nafasi kubwa! Na hapa ndipo uwezo Wako kiuongozi unapo onekana na wengi.,
Nafasi yako inaweza kuwa nafasi pekee ya kimbilio kwa wote wanaohisi ama kutendewa isivyo haki, ama kuadhibiwa kwa haki kabisa ila wakatafuta huruma ilikupunguza adhabu ambayo pengine ni kali sana.,

wewe ndio nafasi hiyo ya hekima na huruma.

Mheshimiwa,
Mungu akutangulie.
 
ndugu zangu wana JF,
Habari,

Ninamshukuru Mungu mwingi wa rehema kwa wakati mzuri aliotupatia tena kushirikishana mawazo tofauti ilikutupatia ushiriki na uhai katika kuukabili mustakabali wa taifa letu hili tukufu pamoja na watu wake.

Ndugu zangu, Leo nikohapa kuyaleta mawazo yangu hasa juu ya dhana nzima ya UONGOZI nikiweka msingi juu ya presentation aliyo ifanya Mh. Freeman Mbowe, mwenyekiti wa Chama cha Democrasia na Maendeleo Taifa wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru 9/12/2013 land mark hotel.

Ndugu zangu Mh. Mbowe alieleza kwakirefu sana juu ya historia yake ndani ya chama na mchango wake mkubwa katika nafasi mbali mbali na hatimaye kama mwenyekiti wa kwanza wa Bavicha na mwenyekiti wa chadema taifa baadae.

Mh. Mbowe alieleza pia mchango wake mkubwa sana katika kutafuta viongozi wengine wakuisogeza CHADEMA karibu zaid na hatima yake iliyokusudiwa wakati wa kuundwa kwake.

Mheshimiwa alizungumza juu ya mchango wake wa kiushawishi na kimkakati uliyo fanikisha chadema kupata viongozi Makini wengi wakiwemo the likes of Mh. Lisu, Mh. Lema, Mh. Mdee, Mh. John mnyika na Mh. Zitto Zuberi Kabwe among others.

ndugu zangu, kazi aliyo ifanya Mh. Mbowe ni kubwa na inajidhihirisha kwa takwimu za mabadiliko makubwa in all levels kuanzia idadi ya wa wakilishi bungeni hadi idadi ya wanachama, kuanzia idadi ya mashina ya chama hadi idadi ya rasilimali za chama among many other aspects relevant.

Kwakazi hii nasema Mungu huchagua viongozi sahihi kulingana na hali ya wakati husika.

Kwakipindi hicho chote chamwanzo hadi sasa, chadema ilihitaji uongozi wa mtu makini lakini mgumu, jasiri, asiyeogopa, mkali na mwenye misimamo au kwalugha nyingine waweza kusema "mtu mbabe" ilikukisimamisha imara amidst strong opposition from the rulling CCM.
Kwakipindi hiki chote tulimuhitaji kiongozi wa mithili ya Mr. Mbowe na Mungu alitupatia Mbowe. Sasa hapa si kusema kwamba sasa hatumuhitaji tena No. Ila nataka kuonyesha tu kwamba he came to us at an opportune time.

kazi ya kusimamisha kitu dhaifu ama kitu kichanga kuwa organization kubwa na yente misingi imara na sahihi ni kazi ngumu sana sana sana kuliko wengi tunavyoweza kudhani.

Hii ndio kazi waliyo ifanya viongozi wetu wazee waliotuwekea misingi ya utaifa wetu. Mzee Mwalimu Nyerere, Ndugu Sokoine, Ndugu Sarakikya, Mzee Kawawa na wengine wengi hapa tanzania na akina Mandela na wenzake huko nje africa kwaujumla.

Kazi imefanyika, na kazi imeonekana!
Hongera sana Mr. Chairman.

However changamoto Hasa zimeanza kujitokeza, na hizi ndizo kipimo hasa cha uimara wa taasisi yetu.

Lakini hapa pia bila kusita maamuzi SAHIHI yalifanyika na kwawakati bila kuchelewa.
Hii imeleta kutoeleweka kwa mh. Mbowe kwa watu wengi. Lakini mimi masema,
Good job Mr. Chairman, uongozi ni jukumu gumu sana, uongozi wowote!!.

Siwengi wanaoweza kuelewa hili. They say it takes a leader to understand one!

however katika kumalizia niombe tu sasa kwamba hekima ikuongoze pia.,

Hapa tunahitaji kuvuka si salama tu, ila PAMOJA.

mimi naamini unaumia yanapotokea haya yanayotokea, lakini huenda unadhani hakuna namna inabidi yaende hivyo. Well, binafsi nadhani kwanafasi yako unaweza kuisimamia HAKI. Na kwamba, sio tu haki itendeke katika hili, laki haki IONEKANE ikitendeka katika hili,
Mh. Mwenyekiti bado upo umuhimu wakuhakikisha maamuzi yanafanyika juu ya taarifa zilizothibitishwa pasipo shaka kabisa lakini pia kwanidhamu na heshima ya utu na nafasi ya anaye kabiliwa na shutuma hizi, ikifika wakati sahihi taratibu sahihi zifuatwe kutoa adhabu yenye lengo la kufundisha na si kukomoa.

Katika hili mh. Mwenyekiti unayo nafasi kubwa! Na hapa ndipo uwezo Wako kiuongozi unapo onekana na wengi.,
Nafasi yako inaweza kuwa nafasi pekee ya kimbilio kwa wote wanaohisi ama kutendewa isivyo haki, ama kuadhibiwa kwa haki kabisa ila wakatafuta huruma ilikupunguza adhabu ambayo pengine ni kali sana.,

wewe ndio nafasi hiyo ya hekima na huruma.

Mheshimiwa,
Mungu akutangulie.
 
Hapa tulipofika Mbowe ni Shujaa na Jemedari.

Wasaliti na Waasi wote wasakwe mpaka mvunguni wafukuzwe kwa Aibu!

nakubaliana na wewe kabisa ndugu, ila ninachotamani kusisitiza ni kutoa nafasi kwa haki kuonekana ikitendeka. Maanake inafika mahali anayehukumiwa mwenyewe anaona hukumu ilikua balanced iliyozingatia haki yote na taratibu sahihi za kiushahidi na kiungwana kabisa,. Nasianaye hukumiwa tu Bali wote wanaotazama washudie kuwa ama kwahakika kilicho fanyika ni haki na tena uungwana mkubwa pasipo shaka.
Hekima ya Mh. Mwenyekiti bado inanafasi yake!
Asante
 
mhhhhhhhh kiongozi anahijika awe na destiny,kwa yeyote yule ambaye atachaguliwa ,itakua ndo chaguo la watu na heaven,atakua na mamlaka ya kukijenga au hata kukiua
 
Ahsante mh.mbowe kwa kazi nzuri na ya ushindi mkubwa.wasio na maono hata ukitumia ndimu hawatakuelewa ..lakini kwa ujumla umegusa idadi kubwa ya watz.
 
haijawahi kutokea mbowe akawa ni kiongozi mwenye hekima zaidi ya ubabe na mipango michafu ya kuwakwaza na kuwazamisha wale wote wanashindwa kukubaliana na mawazo yake.
 
Ahsante mh.mbowe kwa kazi nzuri na ya ushindi mkubwa.wasio na maono hata ukitumia ndimu hawatakuelewa ..lakini kwa ujumla umegusa idadi kubwa ya watz.

mkuu mbowe nadhani atakuwa amekugusa wewe tu siyo kweli kwamba mbowe kafanya yote haya bali yamefanywa na zito tatizo la mbowe yuko to local.
 
mkuu mbowe nadhani atakuwa amekugusa wewe tu siyo kweli kwamba mbowe kafanya yote haya bali yamefanywa na zito tatizo la mbowe yuko to local.

Niliipenda CDM kwa sababu ya kamanda Mbowe na timu yake walivyoonesha ujasiri na umakini mkubwa katika kupambana na uchafu wa maccm.zzk ni moja ya kiongozi ninayemwona kama kili stars!mara homa inapanda mara inashuka!anakatisha tamaa sana huku akijizolea wafuasi wengi kutoka ccm na kuungana nao kuishambulia CDM.Kamanda Mbowe anabaki kuwa shujaa na kamanda asiyetetereka.After all ubabe ni sifa muhimu kwa kiongozi na hasa anapoufanya mahali na wakati muafaka.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
MBOWE NI KAMANDA AMEPAMBANA NAKUKABILIANA NA NA VIGIMGI VINGI HADI KUIFIKISHA CDM HAPA? Wenyeviti wengi wamejisalimisha CCM, Yuko wapi mzee wa kilacha, Yuko wapi Mzee mapesa wamebaki wao ndio CHAMA!

Kuongoza upinzani silelemama watu wanabanwa na kujisalimisha, yuko wapi Lawmwai, Inno kalogenesi, baado naamini Lamwai ni mpinzani lakini mkate kwanza!
 
mhhhhhhhh kiongozi anahijika awe na destiny,kwa yeyote yule ambaye atachaguliwa ,itakua ndo chaguo la watu na heaven,atakua na mamlaka ya kukijenga au hata kukiua

Umesema sahihi ndugu, ila pia
Siviongozi wote wanaochaguliwa na watu huifanya kazi sahihi waliyo chaguliwa kuifanya,. Kama ulivyosema wengine huchaguliwa na watu lakini huishia kukibomoa chochote walichotakiwa kukijenga badala yake,.

Lakini hii wakati mwingi hutegemea zaidi personality ya kiongozi ikilinganishwa na mazingira yaliyopo kwa wakati husika.,

Labda nieleze tena, kwakipindi kile chamwanzo tulimuhitaji mtu wa aina ya mbowe, tulihitaji mtu atakaeongoza nakuambukiza roho ya ujasiri na kutokuogopa ndani ya wanachama na viongozi wengine, CHADEMA ilihitaji mtu wa aina ya mbowe, hilo hatuwezi kulidharau, walakujidai hatulioni,. Lazima tulikubali,

Lakini kwa hatua hii sasa, CHADEMA inahitaji kubadili aina ya siasa zake,. Zisiendelee kuwa zakimapinduzi kama ambavyo zimekua kwamuda wote kufikia sasa nabadala yake tuanze kuunda CHADEMA yenye siasa za hoja! Siasa za misingi (principles)

Hii sasa kwa CHADEMA ni phase mpya! Ni umri mwingine katika maisha ya chama, lazima siasa zetu zibadilike kuendana na hali na umri wa chama.

Ninamaanisha nini hapa ninasema, CHADEMA sasa tunapaswa kujenga systems za ndani mwa chama mithili ya serikali madarakani.

Hatupasiwi kusubiri kuchukua dola ndotuanze fikiria nini kinafanyika wapi.

niwakati wa kutengeneza policies na programs na kuzitekeleza kuleta mabadiliko yanayo onekana kwa maisha ya watu katika maeneo tunayo ya ongoza.,

Niwakati wa kujenga kuaminika na watanzania WOTE bila kujali dini wala kabila zao.

Lazima viongozi sasa tuanze kuakisi mamlaka,focus,direction,vision, and purpose!

Ndio nasema kwasasa Mh. Mbowe Yuko kwenye nafasi inayohitaji hekima zaidi sana wakati huu kuliko wakati mwingine wowote ule kabla ya sasa.

Mwekundu, nashukuru
 
MBOWE NI KAMANDA AMEPAMBANA NAKUKABILIANA NA NA VIGIMGI VINGI HADI KUIFIKISHA CDM HAPA? Wenyeviti wengi wamejisalimisha CCM, Yuko wapi mzee wa kilacha, Yuko wapi Mzee mapesa wamebaki wao ndio CHAMA!

Kuongoza upinzani silelemama watu wanabanwa na kujisalimisha, yuko wapi Lawmwai, Inno kalogenesi, baado naamini Lamwai ni mpinzani lakini mkate kwanza!

oh yes! That's for sure
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom