Uongozi na Posho/Mshahara: Ukweli na Uwazi

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
WanaJF,

Kwa sababu mimi sio Mbunge nitawasilisha kwenu kile ninachopata kama Diwani.

Ili nichangie kwa uhuru na niweze kutoa mawazo yangu bila kung'ata maneno ni vyema nikaweka wazi kile ninachopata kama Diwani.

Hii itasaidia pia kwa WanaJF kujua na kuchambua tuko wapi, tunaenda wapi na tutafika lini.

Mimi kama Diwani nalipwa posho (sio mshahara) kwa mwezi shilingi laki moja na ishirini (Tzs 120,000).

Posho ya Kikao cha Halmashauri ni shilingi elfu hamsini (Tzs 50,000) kwa kikao. Vikao vinatakiwa angalau vinne kwa mwaka.

Posho ya Vikao vya Kamati (Kamati ya Elimu, Afya na Maji) ni shilingi elfu hamsini (Tzs 50,000). Vikao angalau vinne kwa mwaka.

Posho ya vikao vya Kamati ya ALAT Mkoa ni shilingi elfu sitini na tano (Tzs 65,000) kwa kikao.

Hicho ndicho ninachopata kama Diwani.

Nilichoamua kwa roho nyeupe kabisa ni kama ifuatavyo;

1. Posho ya kila mwezi yote igawanywe kwa shule za msingi kuchangia chakula cha mchana cha watoto. Shule ziko 11. Nimemuelekeza Afisa Mtendaji kila mwezi azichukue na kuzigawanya. Nitazisimamia zifike hata kama ni kidogo.

2. Posho za vikao vya Kamati ya Elimu naanda utaratibu zishindaniwe na watapewa wanafunzi watatu wa kiume na watatu wa kike watakao fanya vizuri zaidi kwenye mitihani ya muhula kwa kata.

3. Posho za vikao vya Halmashauri nitatumia kuwanunulia soda na biscuits wajumbe wa Kamati ya Maendeleo ya Kata ambayo Diwani ndie Mwenyekiti wake. Kamati hii haina fungu lolote na ndio chombo ambacho kinaandaa miradi na mipango yote ya maendeleo ya kata.

4. Posho ya ALAT itachangia mafuta yangu ya gari kuzunguka kwenye kata kuangalia shughuli za maendeleo nk.

Changamoto kwa WanaJF, je haya ambayo nimeamua kuyafanya na kuyasimamia yana faida gani kwa jamii? Je ni njia sahihi?

Si madiwani wote wanaweza kupishana na posho zao. Wengi wanazihitaji kujikimu. Wao ndio 'watendaji' wakuu katika kuhamasisha na kusimamia shughuli za maendeleo.

Nielekezeni, nirekebisheni pale ambapo sipo sahihi. Pale ambapo ni pakuboreshwa nisaidiwe. Sioni aibu au fedheha kama kiongozi kuomba msaada na ushauri.

Naamini ni muda wa viongozi kubadilika na kuanza kutenda si kwa maneno bali vitendo. Sote tushiriki kuleta maendeleo yetu hata kwa kushauri na kuelekeza.
 
How did you manage to buy ML and other expensive vehicles, living very high standard of life.
 
BB, its a Brabus, not ML. I worked hard. Since 2004. I had a good mentor and you know him. Being focused and working hard will take any committed individual places higher than the obvious.

And am still paying for the Brabus. I have a last instalment to pay.
 
Kwa upande wangu kama unachokisema ndo unatenda au unapanga kutenda tekeleza kwani ndo njia bora ya kuleta maendeleo kwa jamii kubwa ya watanzania walio masikini. Wasiwasi wangu ni kuwa viongozi wa tanzania wana kauli ndumila kuwili anavyoongea sivyo anavotenda. Ushauri wangu fanya kama unavyofikilia.
 
That's great Albert, hapo umeonyesha moyo wa kutokuwa mbinafsi, wabunge wetu nao wangekuwa na moyo huo sasa hivi tungekuwa mbali sana. I am trying to imagine 90m x 326 = almost good 30b (six mt meru hosipitals)
 
BB, unajiuliza, kipi kianze? Gari la Mbunge au Hosp? Huku kwetu jibu ni, vyote!

Hatuna priority. Tunataka kufanya kila kitu tunaishia kutokufanya kitu. Trying to be masters of all trades....

Naamini unakumbuka hasira za vijana pale uwanjani wakati wa mkutano wa CDM.

Personally I am very worried. Siku ya siku hapata kalika. Mwananchi ambaye hana kodi ya chumba kimoja anaishi mbauda leo anasikia Mbunge anakopeshwa mil 90 unadhani anafikiria nini? Anapanga nini? Kazi tuliyonayo ni kubwa.
 
I'm certain to know wewe ni diwani wa kata gani na iko wapi katika Tanzania hii?
Otherwise its a good move,kama ulivosema sio kila diwani anaweza kufanya hivo maana wengine wana gombea kutibu njaa zao tu so kutoa hata kidogo bado ni moyo wa ajabu sana
 
Mheshimiwa diwani,

Umenena vyema nakutakia utekelezaji uliotukuka,

Pia kwa sababu Ndesamburo alisema atanunua greda kwa manispaa ya moshini vyema basi posho zikawa accumulated for sometime na kuweka mafuta kwenye hilo greda ili atleast ile barabara ya Mabogini to Chekereni ifae kupitika kwa urahisi.

Pili kama kuna uwezekano wa kuangalia migogoro katika kilimo chetu cha mpunga huko nyumbani.Nafikiri kuna matatizo mahali...may be yanaanzia Chawampu.Nasikia matrekta yaliuzwa pale kwa bei za kutupwa.Sasa hakuna uchumi tena mabogini na chekereni watu wamerudi kuwa wachuuzi.Kifo cha mpunga kimefanya uwezo wa watu kununua bidhaa kupungua sana (purchasing power),,wenzetu wa kahe wao ni tofauti....ukienda kahe wanatuzidi sasa wakati wao tulikua tumeshawaacha.


Shule zetu nazo ndo chachemea kabisa.At least motisha hii ya diwani italeta ahueni.Vijana watashindana sasa na tutarudi where we always supposed to be.

Turudishe uchumi wa vijijini kwetu diwani kwani sasa hivi utakutana na watu wanasema wanaenda kwa mganga mabogini.Ni kero! Tukubali mheshimiwa kwamba the time tunapata jibu la uhakika na endelevu kwa kilimo chetu kila mtu atafanya biashara sahihi!

All the best
 
Mkuu thanks na unaonyesha kwamba upo Patriotic keep it up

Tatizo watu hawaingii kwenye siasa kusaidia watu bali wanaingia kutafuta deals za kuweza kujineemesha (yaani kuacha legacy ya kwamba nilifanya hiki na kile haitoshi...) kwahiyo wanabuni mbinu za kuweza kujitajirisha...

All I can say is do all the good things na tumia media kuonyesha mazuri yote unayofanya ili iwe mfano kwa watu wengine na wasiofanya waone aibu. Tengeza Tapes za mambo unayofanya na jinsi unavyofanya.., tuna makala kwenye magazeti tofauti kuonyesha maendeleo na changamoto zinazokupata... hakikisha everyone knows that you are doing good and its possible to be done..

Nadhani muda umefika siasa kuwa ni wito na huduma na sio sehemu ya kuweza kuneemeka...,
 
Mr Diwani,kutokana na kauli na mipangilio yako naomba nisikuite Mheshmiwa kwani hadi hapo umekuwa ni mfano wa kuigwa,kwamba hautaki kukwezwa wakati wanamchi wanateseka. Ulichoplan kwa posho yako kuwasaidia kizazi kijacho ni sawa kabisa na fuatilia jambo hilo lifanyike kama unavyotaka.Tatizo kwa madiwani wengine ni kwamba wao udiwani ndio ajira yao,hawana kipato kingine zaidi kwahiyo wengi wao hawawezi kamwe kufanya kama unavyofanya wewe,Nakujua wewe ni mpiganaji toka kitambo tukiskuli Ilboru.Fikiria hilo jina langu hapo juu uatajua mimi ni nani.Nakutakia mafanikio..Nitakutembelea katani mwako kuongeza motisha zaidi katika juhudi zako.
 
I'm certain to know wewe ni diwani wa kata gani na iko wapi katika Tanzania hii?
Otherwise its a good move,kama ulivosema sio kila diwani anaweza kufanya hivo maana wengine wana gombea kutibu njaa zao tu so kutoa hata kidogo bado ni moyo wa ajabu sana

Kata ya Mabogini, Moshi Vijijini kamanda
 
Mr Diwani,kutokana na kauli na mipangilio yako naomba nisikuite Mheshmiwa kwani hadi hapo umekuwa ni mfano wa kuigwa,kwamba hautaki kukwezwa wakati wanamchi wanateseka. Ulichoplan kwa posho yako kuwasaidia kizazi kijacho ni sawa kabisa na fuatilia jambo hilo lifanyike kama unavyotaka.Tatizo kwa madiwani wengine ni kwamba wao udiwani ndio ajira yao,hawana kipato kingine zaidi kwahiyo wengi wao hawawezi kamwe kufanya kama unavyofanya wewe,Nakujua wewe ni mpiganaji toka kitambo tukiskuli Ilboru.Fikiria hilo jina langu hapo juu uatajua mimi ni nani.Nakutakia mafanikio..Nitakutembelea katani mwako kuongeza motisha zaidi katika juhudi zako.

Kamanda karibu sana kwenye kata. Its true, it will be good to have you around. And we can cry together for has become our lovely Ilboru Special School.
 
Kutuambia vikao viko vinne kwa mwaka nachelea kuliamini hilo labda kwa mwezi. Vile vile hukusema hivyo vikao vinne vinakuwa vya siku ngapi? Sasa wakati wa kampeni mnakamiana hivyo kwa ajili ya Shs 120,000 au kwenda kujipa tenda na kujigawia viwanja?
 
Kutuambia vikao viko vinne kwa mwaka nachelea kuliamini hilo labda kwa mwezi. Vile vile hukusema hivyo vikao vinne vinakuwa vya siku ngapi? Sasa wakati wa kampeni mnakamiana hivyo kwa ajili ya Shs 120,000 au kwenda kujipa tenda na kujigawia viwanja?

Vincent, Sheria Namba 7 ya Mwaka 1982 ndio inaelekeza hivyo kuhusu vikao na ndiyo ratiba niliyonayo. Sina uhakika unaposema 'wakati wa kampeni mnakamiana' unaniongelea mimi binafsi au wengine nisiowajua. Kuhusu tenda na viwanja sio vitu ninavyohitaji.
 
Chelea pia kuamini wabunge wamepokea mil 90 Mr.Vincent,Maana inaonekana kwako kuamini ni mpaka uguse kama Tomaso kwenye biblia.Inaonekana waaazi kabisa ingekuwa ni wewe ungekamiana tuu pale palipo na maslahi yanayokukidhi haja wewe.WanaCDM,misimamo yao sio kama hiyo unayofikiria wewe ya kukamiana palipo na dau kubwa kama CCM!!!Naona kauli yako tuifananishe na yakifisadi kidogo kwani huna uzalendo hata kidogo.Nashukuru Mr.Diwani wa mabogini,Kamanda wa wanyonge nyota yako inang'ara sio mabogini tuu wanaona hata hapa Dafur naiona kwa uwazi kabisa.Nitatia timu na best/Robart kama uwepo wako utakuwa huko Mabogini mwezi wa 3 tarh za mwishoni.Big up Mkuu.
 
safi sana....napenda kujitoa kwako. kina Obama walianza hivi hivi!!
wewe ni diwani wa chama gani?
 
BB, unajiuliza, kipi kianze? Gari la Mbunge au Hosp? Huku kwetu jibu ni, vyote!

Hatuna priority. Tunataka kufanya kila kitu tunaishia kutokufanya kitu. Trying to be masters of all trades....

Naamini unakumbuka hasira za vijana pale uwanjani wakati wa mkutano wa CDM.

Personally I am very worried. Siku ya siku hapata kalika. Mwananchi ambaye hana kodi ya chumba kimoja anaishi mbauda leo anasikia Mbunge anakopeshwa mil 90 unadhani anafikiria nini? Anapanga nini? Kazi tuliyonayo ni kubwa.

Albert, bila kuangalia ni jinsi gani utaweza kuwapatia watu sources of income hayo mengine yote ni temporal solution zinawafaa tu wale ambao wanataka votes na siyo kuleta permanent solution. Vijana wanahasira kwasababu hawana ajira na wana ambition zao katika maisha; kwangu mimi hasira ya vijana ingekuwa opportunity zaidi kuliko kuwa constraint katika maendeleo... Wewe umesoma ni kazi yako kuwa coordinate vijana katika kuwaunganisha ili wakiunganisha nguvu basi shughuli wanayofanya hatimaye iwe na tija.

One principle ni kuhakikisha huanzishi kitu kipya kati ya wanayoyafanya kama kianzio lakini unapunguza uniformity na kutengeneza categories katika production of goods and services. Namaanisha nini kama vijana ni street vendors kwa mfano basi utakuta wote wanauza vitu vinavyo uzika haraka na kwa faida bila kujua hiyo pekee ina ongeza competition na kupunguza rent/benefit; so unafanya livelihood analysis siyo lazima ukaifanya kiuchumi no rapid appraisal ni njia sahihi kwani ni rahisi kueleweka na wengi. Baada ya hapo unaangalia consumer wakubwa ni kinanani na je market yake ina ukubwa gani rough estimate tu then unaangalia ili mtu apate faida ya kueleweka basi effort kiasi gani iwekwe hapo au kwa lugha rahisi vijana wangapi wa concentate kwenye hilo. Hii ni case moja

Tofautisha makundi ya vijana waliopo katika uwezo wao na jaribu kuwaweka kuwa parsued kutokana na interest zao wale wenye ujuzi wawe leaders depending na specialization then uwa diversify kufuatana na speciality zao. Ukifanya hivyo utagundua wakianza production basi labour haitatosha wanaweza kuvuta vijana wa kata za karibu. Kuweka safety nets kwa vijana wa kata yako unatengeneza criteria ya kuwa exclude watokao nje kwa kutoa incentive nyingi kwa vijana wa ndani ya kata zaidi ya wakutoka nje ila pale ambapo unaona wanaweza waka add value unatoa nafasi under certain condition.

Katika production function ya kata kumbuka comparative advantages na kata zingine. Usifanye shughuli ambayo efficiency yake inaweza kuwa kubwa kuliko kata yako maana kutokana na difussion wale wa kata yenye hiyo comperative advantage wanaweza kuwa washindani na kuwa outsmart katika efficiency lakini unaweza ku ignite huku ukiweka strategy ya kuandaa colaboration iwapo watatokea wenye akili kwenye hiyo kata uliyo earmark.

Kwa ufupi unatengeneza governance katika domain ya kata na kuiendesha kama nchi zinavyoendesha uchumi wao so unahakikisha kila unachoweza kukifanya katika kata unakifanya na kutengeneza informal sysytems ambazo ziko legitimized ndani ya kata.

Kila la heri diwani
 
msando heshima kwako mkuu.nimekukubali ila plse ongea na diwani wa kata ya RAU SABASABA tuna tatizo la barabara kutoka majengo mpaka madukani.plse naomba umpe maujanja ili tusipate shidakipindi hichi cha mvua.:msela:
 
Back
Top Bottom