Uongozi Mpya wa CHADEMA kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010

Hapo tu ndipo panapo tuninya raha na kutukosesha imani na vyama vya siasa,sasa democrasia iko wapi,mmmmmmm apo ndipo pabaya
 
Hawa wote ni Wanasiasa kama vile walivyo watu wengine vile hivyo kuna hali ya freaking fulani hivi so CHADEMa kuwa Imara siku zote
....kweli kabisa uyasemayo...na mimi bado sijawahi kuona mwanasiasa anayegombea nafasi ya uongozi eti ili aje awatumikiye wananchi....sijawahi/sintowahi kuona.....
 
Hili Mbona limeshupaliwa saaana? Mbona Kwenye lile CHAMA CHA MAFISADI(CCM) hii ni kawaida tu watu kuambiwa wajitoe? Mnakumbuka Mzee Kifimbo alivyiowatoa nishai Kina John Na Edrward wakati wa mchakato wa Urais wa Awamu Ya Mkapa? Mbona hamjauliza Demokrasia iko wapi? Leo hii tunasikia watu watu wanampigia debe KIKWETE awe mgombea pekee wa Urais but nodody is Shouting! Ama kweli NYANI HAONI KUNDULE
 
Ukila na kipofu uwe makini usimguse mkono!!!

Hata hivyo, kazi kubwa imebaki kukiweka Chama sawa baada ya dogo kubwabwaja hovyo!!! Mungu amsaidie awe na busara ya kuwasiliana na umma!!! Aliaibisha.
 
Mi nafikiri wakati umefika wa kujadili john mnyika kwa upana,in depth,maana inaonekana katika kila tatizo la chadema,john mnyika anatajwa kutumika,na sio kama mtu huru mwenye misimamo yake.

Kwani huyu John Mnyika katika uongozi wa Chadema ni nani mpaka awe anahusika na kila tatizo ndani ya chama hiki makini?
 
Karibu wapika majungu na kumtafuta nyoka miguu .Kumeibuka wageni hapa wan post 3 hadi 20 kazi yao ni majungu nakujifanya wanataka kumsemea sana Zitto.Mara hajatendewa haki wakati Zitto aliamua mwenyewe kwa kuona hali halisi na mapenzi yake kwa Chama chake .Leo mnasema kanyimwa haki .Demokrasia ni pamoja Zitto kuombwa akatoa jina na si lazima abakie ndiyo iwe demokrasia.Kama vile kule CCM mnavyo mtaka kumuondoa Sitta kwa kuwa hawapa nafasi kuwaibia watanzania .

Karibuni JF muendelee katika mada zingine msiishie hapa na majungu yenu .Sasa una akili timamu unauliza kama Zitto ameridhika lazima uje hapa ? Nenda kwenda Chama kamfatute muulize maana una taka kama karidhika ama hapana .
 
kuridhika ama kutoridhika na cheo inategemea sana falsafa yake juu ya maisha ya kisiasa, na uelewa wako juu ya CHADEMA, PIA HUTEGEMEA na matamanio yake kama kijana.
KURIDHIKA AU KUTORIDHIKA KUTATEGEMEA NAMNA GANI WALE ALIODHANI NI MAADUI ZAKE WATASAMEHEANA NAE PALE MAKAO MAKUU,KINONDONI.
NAAMINI ZITO SI MUOGA HIVYO ATAJITOKEZA HADHARANI KUTUELEZA KAMA AMERIDHIKA AMA LAAH.
 
kuridhika ama kutoridhika na cheo inategemea sana falsafa yake juu ya maisha ya kisiasa, na uelewa wako juu ya CHADEMA, PIA HUTEGEMEA na matamanio yake kama kijana.
KURIDHIKA AU KUTORIDHIKA KUTATEGEMEA NAMNA GANI WALE ALIODHANI NI MAADUI ZAKE WATASAMEHEANA NAE PALE MAKAO MAKUU,KINONDONI.
NAAMINI ZITO SI MUOGA HIVYO ATAJITOKEZA HADHARANI KUTUELEZA KAMA AMERIDHIKA AMA LAAH.


Umesema vyema kabisa .
Thanks man .Watu waacha kumchonganisha Zitto he is above mawazo mgando haya .He is never after vyeo as far as I know na hata wazee wale aliwaambia .
 
Kama hajaridhika wewe inakuhusu nini? Siku ukipewa na mkeo huko nyumbani usiridhike utawatangazia familia yako yote, au utakuja kutuambia hapa JF (don't take this literally)? Nina maana kuna mambo ya rohoni kwa mtu, kuna mambo ya ndani ya chama, kuna mambo ya ndani ya familia. Hukumbuki Chidumule alisema "mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe mwenyewe? Jamani, JF is more than "udaku", we better keep that in mind.
UMK
 
Wameshindwa kulipia hata kwenye redio ili mkutano huu uwe live angalau masikioni tu? Wenzao CCM hii namna moja ya kujinadi na kujitangaza.
wajitangaze nini wakati tunawajua.achana na propaganda za CCM
 
Salaam, nilihudhuria mkutano mkuu wa Chadema uliofanyika ukumbi wa Kiramoo ulioko Mbezi Beach Sec School.
Siku ya kwanza ulianza kwa maandamano na kufuatiwa na hotuba ya ufunguzi iliyotolewa na Mwenyekiti Mbowe.

Siku ya pili ulipokea taarifa mbalimbali za chama na kufanya uchaguzi mkuu.
Matokeo ni:-Mwenyekiti ni Freeman Mbowe: kura ndiyo 425 (93%), kura hapana 22 (5%), Zilizoharibika 10.

Makamu mwenyekiti znz: Said Issa Mohamed 243 (53%), Said Mzee Said 212 (46%), Zilizoharibika 4

Makamu mwenyekiti bara: Said Arfi 315 (69%), Shambwee Shitambala 99 (22%), Ben Kapwani 40 (9%), Zilizoharibika 2.

Uchaguzi umekwisha sasa kwa Chadema imebaki kuponya vidonda, kufukia makovu na kujenga chama tayari kwa uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2010.
Wanabodi, nilihudhuria Mkutano huu, Mabalozi wafuatao walikuwepo in person, Tim Clarke, wa EU, Diane Corner wa Ujerumani, Balozi wa Canada, Balozi wa Uholanzi na Balozi wa Sweden!.
Nimeikumbuka hii kufuatia kelele nyingi kwa balozi wa China kushiriki Mkutano wa CCM.
Pascal.
 
Back
Top Bottom