Uongo na Ukweli Kuhusu TANESCO Kuzuiwa Kufanya Maintenance

Yeah na pia hela za gesi wanazokusanya nyingi zinaenda kwa mabeberu ndio maana Magufuli hakuona tija tokana na mkataba mbovu aliopitisha chief jakaya..ila za JNHPP asilimia 80 au zaidi zitakuwa zetu humu endapo mradi ukikamilika. Tukinunua umeme hela zote zinabakia ndani.

Kinachowaboa kina Marope ni kuwa kule JNHPP mkataba haujachezewa ili kuwanufaisha wao ama CCM vigogo. Ndio maana wakageuka anti-magufulification. Hawakumpenda kabisa sababu hakuwapa chance ya kutengeneza michongo ya 10%
Gesi tumepigwa siku nyingi yule muhuni wa chalinze ni mtu wa ovyo kabisa
 
Sasa si umeuliza alifanya nini? Ulitaka nikujibu majibu ya uongo ama! We lini ulisikia umeme unakatika kwa sababu za hovyo kama anazotoa marope katika utawala wa Magufuli?
Huyo unaye mjibu ni zuzu
 
Je,unakubali kuwa JPM katika suala la umeme kutokatika Mara kwa mara alitengenezewa mazingira hayo na JK kupitia Kinyerezi I iliyoanza kuchangia zaidi ya MW 200 kwenye grid ya taifa mwezi oktoba 2015?
Wacha ujinga kukatika kwa umeme lengo lilikuwa tuuziwe umeme na mafisadi ya iptl hivyo mifumo ya serikali iliuliwa ili sekta binafsi za kifisadi ziuze umeme wa bei ya juu kama siyo magufuli leo tungekuwa tunanunua umeme unit 1sh1500 huo ndiyo ukweli
 
Hizo hoja ni mfu if it ain’t broken why you tryna fix it?

Hizi mishe zote ni sababu ya Marope tu kuingizwa katika nafasi ya uwaziri wa nishati inaeleweka kabisa kuwa amewekwa pale si kwamba ni mmbora sana ila yupo kimkakati ili kukamilisha mipango ovu ya watu flani tu ambao atakula nao.

Siku zote mtu akiwa na jambo lake hakosi sababu hata mwanamke akitaka kukuacha lazma akupe mtihani ambao anajua lazma utaushindwa tu ili iwe kama sababu ya kukuacha.

Kusingizia maintanance ni utoto sababu hata kama ni hivyo unaweza fanya maintanance ya mitambo kwa phase bila kuathiri uzalishaji.'Mkuu 'Extrovert'
Mkuu 'Extrovert', huyo 'jamaa' niliyemjibu hapa na kumsifu kiaina anafahamika vizuri sana kwa misimamo yake iliyo wazi humu JF. Huyu naona ndiye 'mouthpiece' ya hili genge ambalo sasa linaiendesha serikali, kwa hiyo anakuja humu na hoja zao, nyingi zikiwa ni za kupotosha.

Sifa nilizommwagia ni juu ya juhudi zake kubwa za kutafuta taarifa ili kuunga mkono hayo wanayotafuta upotoshaji juu yake, na wala siyo kwa usahihi wa taarifa zenyewe anazoziweka hapa.
Hizo hoja ni mfu if it ain’t broken why you tryna fix it?

Hizi mishe zote ni sababu ya Marope tu kuingizwa katika nafasi ya uwaziri wa nishati inaeleweka kabisa kuwa amewekwa pale si kwamba ni mmbora sana ila yupo kimkakati ili kukamilisha mipango ovu ya watu flani tu ambao atakula nao.

Siku zote mtu akiwa na jambo lake hakosi sababu hata mwanamke akitaka kukuacha lazma akupe mtihani ambao anajua lazma utaushindwa tu ili iwe kama sababu ya kukuacha.

Kusingizia maintanance ni utoto sababu hata kama ni hivyo unaweza fanya maintanance ya mitambo kwa phase bila kuathiri uzalishaji.
 
Wao wanapika data na kuja kuzikomalia wakati hali halisi haiakisi hizo data zao uchwara. Toka siku naskia Magufuli amefariki nilijua tu we are Doomed! Hata kifo chake siamini kwamba kilikuwa natural death ila postmortem imepikwa tu na safu ya wapigaji!

Yani nchi hii matatizo mengi yalikuwepo kwa ajili ya manufaa ya kundi la wachache. Watu wanasaini mikataba mibovu kwa siri ili kujiwekea ulinzi wa 10% katika mabilioni yanayonyonywa na mabeberu kila mwaka. Jamaa mmemua ila hamjaua impact yake kwa raia sababu mengi aliofanya yalileta matokeo chanya kwa public welfare.

Kudhihirisha hilo ni kurejea kwa matatizo ambayo yalishaanza kusahaulika it proves that barely JPM alikuwa kidume kweli.
EeeenHeeeee!

Hapana, mkuu 'Extro', usiende huko kwenye kifo cha huyo jamaa. Achana kabisa na huko, maanake pako wazi kabisa. COVID-19 ilifanya kazi yake hapo. Woote waloomzunguka wakapukutika, na yeye wala hakutaka kujikinga, unadhani angepona, tena mtu mwenyewe mwenye 'predisposition condition'? Wewe si uliona Mkapa alivyodondoka? Naye unadhani ni hizo 'conspiracy theories' zinazodhaniwa hapa?

Jamaa angekuwa anadunda tu, anatamba hadi sasa kama angechukua tahadhari tu ya kujikinga. Sijui nchi ingekuwaje hadi sasa? Pamoja na haya mengine tunayomkubali kwayo, lakini binafsi nilikuwa na hofu kubwa sana juu yake kuhusu hatma ya nchi hii. Pengine ingebidi tuwe makondoo sote ili mradi jamaa atimize maono yake, 'whatever' maono aliyokuwa nayo yeye juu ya nchi hii.
Hata hivyo, tungefika huko alikokuwa anapaona yeye tukiwa hoi kabisa!
 
Wacha ujinga kukatika kwa umeme lengo lilikuwa tuuziwe umeme na mafisadi ya iptl hivyo mifumo ya serikali iliuliwa ili sekta binafsi za kifisadi ziuze umeme wa bei ya juu kama siyo magufuli leo tungekuwa tunanunua umeme unit 1sh1500 huo ndiyo ukweli
Thibitisha hapa hilo dai lako vinginevyo wewe ni zezeta.
 
Baada ya maelezo yako marefu, je wanatuhakikishia kuwa kwa vile sasa wanaweza kufanya matengenezo inavyotakiwa Tanzania haitakuwa na tatizo la upungufu wa nishati ya umeme? Je, matengenezo ya muda na kiasi gani yataondoa tatizo la mgao?
Umepatwa na nini mzee wangu?
 
EeeenHeeeee!

Hapana, mkuu 'Extro', usiende huko kwenye kifo cha huyo jamaa. Achana kabisa na huko, maanake pako wazi kabisa. COVID-19 ilifanya kazi yake hapo. Woote waloomzunguka wakapukutika, na yeye wala hakutaka kujikinga, unadhani angepona, tena mtu mwenyewe mwenye 'predisposition condition'? Wewe si uliona Mkapa alivyodondoka? Naye unadhani ni hizo 'conspiracy theories' zinazodhaniwa hapa?

Jamaa angekuwa anadunda tu, anatamba hadi sasa kama angechukua tahadhari tu ya kujikinga. Sijui nchi ingekuwaje hadi sasa? Pamoja na haya mengine tunayomkubali kwayo, lakini binafsi nilikuwa na hofu kubwa sana juu yake kuhusu hatma ya nchi hii. Pengine ingebidi tuwe makondoo sote ili mradi jamaa atimize maono yake, 'whatever' maono aliyokuwa nayo yeye juu ya nchi hii.
Hata hivyo, tungefika huko alikokuwa anapaona yeye tukiwa hoi kabisa!
Nitoshe tu kukuambia wewe ni mpumbavu sio tusi, ebu niambie watanzania wangapi ukiwepo na wewe ambao mpaka muda huu hawajachanja na hawachukui taadhari yotote ya hiyo corona na hatujafa. Je inamaana corona imeisha tanzania baada ya kufa watu muhimu wa magufuli wakina ben mkapa na magufuli mwenyewe na korona nayo ikaisha!? Acha ujinga wewe kwenye vitu muhimu.
 
Nitoshe tu kukuambia wewe ni mpumbavu sio tusi, ebu niambie watanzania wangapi ukiwepo na wewe ambao mpaka muda huu hawajachanja na hawachukui taadhari yotote ya hiyo corona na hatujafa. Je inamaana corona imeisha tanzania baada ya kufa watu muhimu wa magufuli wakina ben mkapa na magufuli mwenyewe na korona nayo ikaisha!? Acha ujinga wewe kwenye vitu muhimu.
Kutokana na swali lako hili inaonyesha wazi wewe ni 'MJINGA', na hilo siyo tusi, ila ni wazi hujui chochote kuhusu haya magonjwa ya milipuko kama COVID-19.
Sitapoteza muda wangu hapa kukuelimisha wewe, kama wakati wote huu tokea corona imeingia hadi sasa, wewe bado hujaambulia chochote kuhusu taarifa zinazosambazwa kila mahala.
Ni watu kama wewe mliomdanganya akapime mapapai, mbuzi, oil, n.k.; kana kwamba hata hakuwahi kuingia darasani na kujifunza sayansi yoyote! Sijui hiyo Ph.D. ya kemia aliipatia wapi!
Kwa vyovyote na iwavyo, tambua kwamba kuondoka kwake kuliepusha taifa hili kupata madhara makubwa zaidi ya yanayoweza kutokea leo au kesho. That was good riddance! Umeelewa?
 
Kutokana na swali lako hili inaonyesha wazi wewe ni 'MJINGA', na hilo siyo tusi, ila ni wazi hujui chochote kuhusu haya magonjwa ya milipuko kama COVID-19.
Sitapoteza muda wangu hapa kukuelimisha wewe, kama wakati wote huu tokea corona imeingia hadi sasa, wewe bado hujaambulia chochote kuhusu taarifa zinazosambazwa kila mahala.
Ni watu kama wewe mliomdanganya akapime mapapai, mbuzi, oil, n.k.; kana kwamba hata hakuwahi kuingia darasani na kujifunza sayansi yoyote! Sijui hiyo Ph.D. ya kemia aliipatia wapi!
Kwa vyovyote na iwavyo, tambua kwamba kuondoka kwake kuliepusha taifa hili kupata madhara makubwa zaidi ya yanayoweza kutokea leo au kesho. That was good riddance! Umeelewa?
Wewe ni mpumbavu na mshamba ,nyie ndo wale mkiona mtoto mdogo anaongea kiingereza mnasema ni msomi

taifa lenye watu zaidi ya 60m mmeletewa chanjo hazifiki 2m nawasiwasi ata zile 1m za mwanzo hazikuisha,kama corona yako ingekuwa na impact ungeona mtaani mwenye
,wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani bro, unajifanya mjuaji mbele giza.na utaalamu wako wa kujivika wa magonjwa ya mlipuko mmeshindwa kuitetea chanjo yenu kwa wananchi ndo maana tunawachora na kusema nyie ni braliomashenzy bure kabisa
 
Kama ambavyo wadau mbalimbali wamekuwa wakisema mara kadhaa, Mkakati wa Taifa kuhusu uzalishaji wa umeme ulikuwa:-

View attachment 2015968
Yaani, malengo hadi kufikia June 2020, tulitakiwa tuwe tumezalisha 4,915 MW. Hiyo ni Performance Audit Report iliyotolewa na CAG March 2019.

Hata hivyo, ripoti ya wizara inasema hadi kufikia mwishoni mwa 2019, tulikuwa tunazalisha ONLY 1,565.72 MW... ni takribani 33% TU ya malengo!

View attachment 2015977

Na hapa ieleweke kwamba, total INSTALLED CAPACITY sio JUMLA ya umeme tunaozalisha bali mitambo yetu YOTE, katika hali ya kawaida basi inaweza kuzalisha HADI 1,602 MW of power.

Ni rahisi kidogo kwa upande wa umeme wa gesi kufanya total capacity kuwiana na total power generated kwa sababu, kwa gesi, all is needed is to pump enough gas provided factors zingine zipo constant! Kwa umeme wa maji, inaweza isiwe rahisi sana kwa sababu some factors are uncontrollable.

Kutofikiwa huko kwa malengo kulitokana na kuhamishia nguvu ZOTE kwenye Bwawa la Nyerere, na hata zile Kinyerezi III na Kinyerezi IV, zikatekelezwa!!!

Of course, labda waliamini kwamba 1,602.32 zingetosha kutufikisha hadi kuanza kutumia Bwawa la Nyerere!! Sasa sijui walizingatia kila siku kuna wateja wapya wa umeme, na kwamba kuna kuharibika kwa mitambo... only God knows!!!

Tuje kwenye Ubungo II ambayo tunaambiwa ni mbovu, huku wengine wakihoji ikiwa ubovu umeanza baada ya JPM kufariki!!! Au ni janja janja tu ya kutaka kuhujumu Mradi wa Bwawa la Nyerere!!!

Je, maintance ilikuwa inafanyika?! Jibu lipo kwenye ripoti kwamba:-
View attachment 2015999
Utaona hapo, Mashine #1 na #2 zilipitisha zaidi ya saa 10,000 tangu siku zilipotakiwa kufanyiwa maintanance!! Yaani Machine #1 iliendelea kuburuzwa kwa mwaka 1 na miezi tangu ilipotakiwa kufanyiwa ukarabati, huku Mashine #2 ikiburuzwa kwa zaidi ya miezi 18 bila kufanyiwa maintanance tangi siku ilipotakiwa kufanyika!!

Je, ikiwa hiyo ni ripoti iliyoandikwa kutoka kwenye takwimu za 2018, je maintance ilifanyika? Na kama ilifanyika, ilifanyika lini?

TANESCO wenyewe, hawa hapa chini:-
View attachment 2016022

Kumbe, hata baada ya miaka 3 baadae, bado Ubungo II ilikuwa haisomeki!!!

Sasa ikiwa tatizo lililopo miaka na miaka, ni mjinga tu ndie anaweza kuamini kwamba hivi sasa Ubungo II ipo operational, lakini sie wapiga deal za kuuza majenereta tunafahamu mambo bado si shwari!!!

Ina maana shida ni kukosekana kwa vifaa peke yake ndo maana haya mambo ya maintanance yanachelewa namna hii?!

Again, CAG's Performance Audit Report iliyotolewa March 2019 inasema:-

Kumbe, jamaa ilikuwa wakitaka kufanya maintanance, wanapigwa STOP, na matoke yake mitambo ikawa inaburuzwa tu hivyo hivyo!!!

View attachment 2016037

Wadau walipozungumzia hilo suala, wakaitwa majina yote ya ovyo ili mradi tu....!!

Ndipo tunarudi pale pale, mbona hilo tatizo la upungufu wa umeme halikuwepo wakati wa JPM!!!

Swali ambalo nimekuwa nikiwauliza wanaotoa hiyo hoja ni kwamba nyie wenzetu mlikuwa mnaishi Tanzania ipi ambayo haikuwa na matatizo ya umeme!!

Anyway, inawezekana wenzetu ni watoto wa kishua mnaoishi kwenye viunga vya Ikulu... lakini sie tulio huku Ushenzini, hususani kwenye miji na vitongoji vikongwe vyenye uchakavu wa miundombinu, kwetu tatizo liliendelea kuwepo muda wote!!

But on top of that, ripoti hapo inaonesha, TANESCO walikuwa wanapigwa STOP kufanya maintenance pale Ubungo II kwa sababu hatukuwa na hifadhi ya kutosha ya umeme kwenye Grid ya Taifa.

Hofu ikawa kwamba, kutokana na kutokuwa na hifadhi ya kutosha, kama mitambo ingezimwa kwa ajili ya maintenance, basi huenda tungelazimika kuingia kwenye mgao!!

Sasa kama tulikuwa tunaogopa kuzima Ubungo II ambayo umeme unaotoka pale is ONLY 105MW, nini kinaweza kutokea kukiwa na upungufu wa maji ambapo, total power generated from hydro, ni 574MW?!

View attachment 2016047

Kama unakataa nchi haipo kwenye ukame, basi tatizo hili la sasa ni la kutegenezwa na mafisadi na wapinzani wa Bwawa la Nyerere, huku sie vibaraka wao tukikesha kuwapanga watu!

Akili za kuambiwa, changanya na zako!

Lakini itoshe tu kusema kwamba, ushabikiwa kijinga unaliangamiza taifa!!!
Ngoja matengezo yaishe na ITPL inaze kazi kusudi tupate umeme tena. Katika maisha yangu ya utumiaji wa Umeme ni kipindi chia Magufuli tu mabapo sikusumbuliwa na ukatikaji wa Umeme. Maintance kwenye power generation haihitaji uzime mitambo yote ya umeme nchi iwe giza. Hapo mimi ninaona ni misheni ya kutengeza tatizo lisilokuwapo kusudi lihalalishe upigaji tu. Yaani kwamba siku Kalemani alipofukuzwa tu, ndipo mitambo iliyokuwa haipati service nayo ikashindwa kabisa kufanya kazi nchi ikaingia gizani. JF inatunza records sana, tutazirudia records hizi siku zijazo.
 
Ngoja matengezo yaishe na ITPL inaze kazi kusudi tupate umeme tena.
Katika mipango ya TANESCO ya kukabiliana na hali hii kwa sasa, SIJAONA POPOTE ikitajwa IPTL ingawaje nafahamu watu aina yenu mngependa kuona IPTL ikiwashwa ili mpate cha kuongea!!
Katika maisha yangu ya utumiaji wa Umeme ni kipindi chia Magufuli tu mabapo sikusumbuliwa na ukatikaji wa Umeme.
Nimeshasema hapa mara kadhaa, kwanza sio kweli kwamba hapakuwa na matatizo ya umeme na nimeshaweka ushahidi kibao wa watu waliokuwa wanalalamika kuhusu umeme!!
'
Kama wewe haukuwa na matatizo ya umeme, haimaanishi kote kulikuwa vizuri!! Na kama hakukuwa na matatizo, I bet kama ni Dar es salaam basi itakuwa unaishi vile vitongoji vipya kama vile Mbezi Beach, Mbweni, Bunju, Goba, and the like!!

Amini usiamini, usishangae ukasikia Toangoma hakuna matatizo ya umeme lakini Kinondoni yapo, WHY? Kwa sababu Toangoma ni kitongoji kipya, na kwahiyo hata miundombinu yao ya umeme ni mipya!!

Sasa kama unaishi eneo ambalo sio among old residential areas, na kuna umeme wa kutosha, tatizo la umeme kwenu linaweza kuwa rare!

Sasa huo umeme wa kutosha ambao JPM unamfanya aonekane ndio ametatua tatizo, huo umeme ameukuta kwa sababu, almost 350MW ni mradi wa JK ulioanza kutumika October 2015, kwahiyo impact yake imeonekana wakati wa JPM, huku more than 100MW zikiwa zlizoingizwa kweney grid ya taifa back in 2013!!

Kwahiyo JPM ana-enjoy matunda ya waliomtangulia, matunda ambayo waanzilishi hawakuyatumi!
Maintance kwenye power generation haihitaji uzime mitambo yote ya umeme nchi iwe giza. Hapo mimi ninaona ni misheni ya kutengeza tatizo lisilokuwapo kusudi lihalalishe upigaji tu. Yaani kwamba siku Kalemani alipofukuzwa tu, ndipo mitambo iliyokuwa haipati service nayo ikashindwa kabisa kufanya kazi nchi ikaingia gizani. JF inatunza records sana, tutazirudia records hizi siku zijazo.
Nani amekuambia inazimwa mitambo yote?!

Tatizo mmezidisha mahaba, matokeo yake hata nyie wenye uwezo wa kufanya kautafiti kidogo mnashindwa kufanya utafiti kufahamu ikiwa wakati wa Kalemani pale Ubungo hali ilikuwaje?! The problem, hata mtu akiwawekea ushahidi, mahaba yanawafanya MUUKTAKATE ushahidi ili muendelee kujiaminisha kila kitu kilikuwa njema!!

Do your own research kwa kutafuta SPECIAL PERFORMANCE REPORT 2019 ambayo ilichunguza utendaji wa TANESCO kisha rudi tena hapa utueleze kama hayo matatizo yameanza baada tu ya Kalemani kuondoka!!
 
Kwa mfano, Machine #1, Hours Required For Maintenance is 30,000 Hours, and Actual Machine Running Hours is 40,356.

Maana yake ni kwamba, kitalaamu hiyo mashine ilitakiwa kufanya kazi kwa saa 30,000 na zikishagonga saa 30,000 hapo inatakiwa kufanyiwa maintanence.

Lakini wakati ilitakiwa kufanya kazi kwa saa 30,000 kisha kufanyiwa maintanence, hadi ripoti inatolewa mashine hiyo ilikuwa imefanya kazi kwa Saa 40,356.

Sasa, 40,356 - 30,000 = 10, 356. Yaani mashine iliendelea kuburuzwa hivyo hivyo kwa saa zingine 10,356 huku ikiwa bado haijafanyiwa maintenance. Ni kama umeambiwa ukimbie 30,000KM kisha upumzike na kupata chakula, lakini baada ya kumaliza zile 30,000KM unalazimishwa ukimbie 10,356KM nyingine, na hivyo kuwa umekimbia 40,356KM bila kupata chakula ulichoahidiwa!!
Kwahiyo kukatika kwa umeme issue ni machine au ni kupungua kwa maji? Mbona mnatuchanganya? Mi naona huu ni ule wizi wa makaratasi, data nyingii ambazo zinatengenezwa na binadamu ili kuhalalisha jambo fulani. Katika taarifa ya CAG je alitahadharisha kwamba maintanance isipofanyika kuna shida ya umeme itatokea? maana hata magari yetu kuna kipindi tunazidisha kilometres bila kufanya service na yanaendelea kutembea bila shida yoyote.

Jambo lingine ni kwamba CAG siyo mungu wala malaika na taarifa yake siyo msahafu kwamba ina ukweli 100%. Kama aliweza kusema kituo cha mabasi cha mbezi hakina tija na kitasababisha foleni na mpaka leo hatujaona hiyo foleni, tunawezaje kumuamini kwenye masuala mengine?

Shida ya taarifa za CAG huwa haziwi challenged na mamlaka nyingine yoyote ile, akishatoa taarifa yake basi inabebwa kama ilivyo mpaka Bunge lije liifanyie kazi. Mi nadhani ingekua vizuri ukatuwekea taarifa ya Bunge baada ya kuwaita TANESCO kutoa ufafanuzi wa hizo hoja za CAG kuhusu kutofanya maintanance ya mitambo yao ili tubalance story .
 
Katika mipango ya TANESCO ya kukabiliana na hali hii kwa sasa, SIJAONA POPOTE ikitajwa IPTL ingawaje nafahamu watu aina yenu mngependa kuona IPTL ikiwashwa ili mpate cha kuongea!!

Nimeshasema hapa mara kadhaa, kwanza sio kweli kwamba hapakuwa na matatizo ya umeme na nimeshaweka ushahidi kibao wa watu waliokuwa wanalalamika kuhusu umeme!!
'
Kama wewe haukuwa na matatizo ya umeme, haimaanishi kote kulikuwa vizuri!! Na kama hakukuwa na matatizo, I bet kama ni Dar es salaam basi itakuwa unaishi vile vitongoji vipya kama vile Mbezi Beach, Mbweni, Bunju, Goba, and the like!!

Amini usiamini, usishangae ukasikia Toangoma hakuna matatizo ya umeme lakini Kinondoni yapo, WHY? Kwa sababu Toangoma ni kitongoji kipya, na kwahiyo hata miundombinu yao ya umeme ni mipya!!

Sasa kama unaishi eneo ambalo sio among old residential areas, na kuna umeme wa kutosha, tatizo la umeme kwenu linaweza kuwa rare!

Sasa huo umeme wa kutosha ambao JPM unamfanya aonekane ndio ametatua tatizo, huo umeme ameukuta kwa sababu, almost 350MW ni mradi wa JK ulioanza kutumika October 2015, kwahiyo impact yake imeonekana wakati wa JPM, huku more than 100MW zikiwa zlizoingizwa kweney grid ya taifa back in 2013!!

Kwahiyo JPM ana-enjoy matunda ya waliomtangulia, matunda ambayo waanzilishi hawakuyatumi!

Nani amekuambia inazimwa mitambo yote?!

Tatizo mmezidisha mahaba, matokeo yake hata nyie wenye uwezo wa kufanya kautafiti kidogo mnashindwa kufanya utafiti kufahamu ikiwa wakati wa Kalemani pale Ubungo hali ilikuwaje?! The problem, hata mtu akiwawekea ushahidi, mahaba yanawafanya MUUKTAKATE ushahidi ili muendelee kujiaminisha kila kitu kilikuwa njema!!

Do your own research kwa kutafuta SPECIAL PERFORMANCE REPORT 2019 ambayo ilichunguza utendaji wa TANESCO kisha rudi tena hapa utueleze kama hayo matatizo yameanza baada tu ya Kalemani kuondoka!!

Kama matatizo yalikuwapo kwa nini watu walalamike sana leo? Siyo hapa JF tu, wewe pita mitaani ndiko utakapopata feedback halisi. Kujaribu kuhalalisha makosa ni kosa zaidi kuliko kutenda makosa yenyewe. Kati ya makosa yaliyofanywa na unaowatetea ni kule kufanya makosa yao so abrupt kiasi kuwa demarcation line ya effects inakuwa so obvious. Ni mara tu baada ya uongozi wote wa Wizara ya Nishani na Tanesco kuondolewa ndipo blackout ikaanza mara moja- ndani ya wiki mbili au tatu tu.

Hiyo ya ITPL imekuwa latently covered na na hayo madai ya kuwa "kuwa na vyanzo vingi" wakati sis tunataka kuwa na vyanzo robust, siyo uwingi wa vyanzo unao-matter.
 
Wewe ni mpumbavu na mshamba ,nyie ndo wale mkiona mtoto mdogo anaongea kiingereza mnasema ni msomi

taifa lenye watu zaidi ya 60m mmeletewa chanjo hazifiki 2m nawasiwasi ata zile 1m za mwanzo hazikuisha,kama corona yako ingekuwa na impact ungeona mtaani mwenye
,wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani bro, unajifanya mjuaji mbele giza.na utaalamu wako wa kujivika wa magonjwa ya mlipuko mmeshindwa kuitetea chanjo yenu kwa wananchi ndo maana tunawachora na kusema nyie ni braliomashenzy bure kabisa
Ni wazi , kutokana na kiwango chako, siwezi kuwa na msaada wowote kwako.
Endelea na ujinga wako hivyo hivyo!
 
Karibu kwenye mjadala...

Hata hivyo, mjadala huu utakuwa na tija ukiweka kwanza data zako ambazo ni za ukweli kwa sababu haina maana kukujibu kwa kutumia data za uongo!
Bwawa la Mtera maji yametoka lini mto Chato?
Nasikia na mto Ruvu umejaa kwa hisani ya Makunduchi
 
Matatizo yenu huwa hamsomi vingenevyo usingeandika kitu ambacho sijakisema!!!

Nilichosema ni kwamba, kabla ya ujenzi wa Bomba la Mtwara kulikuwa na upungufu mkubwa wa umeme! Baada ya kujenga bomba, Serikali ya JK ikapanga kujenga Vituo 4 vya kuzalisha umeme... Kinyerezi I, II, III, na IV ili kuongeza uzalishaji wa umeme!

JK akafanikiwa kujenga Kinyerezi I, lakini kwavile muda wake ulikuwa umeisha, Kinyerezi II iliishia tu kwenye hatua za awali ikiwa ni pamoja na kusaini mkataba!!

Magufuli alipoingia, alitakiwa kujenga Kinyerezi II, III, na IV lakini kinyume chake, akajenga tu Kinyerezi II ambayo mchakato ulishaanza, na ile III na IV akapiga chini akaanzisha Bwawa la Nyerere!!

Sasa kwavile Bwawa la Nyerere linahitaji investment kubwa na time, matokeo yake hadi amekutwa na umauti, mradi ulikuwa hujakamilika!

Matokeo yake, hadi kesho umeme unaotegemewa kwa kiasi kikubwa ni ule ule ambao aliukuta huku wa gesi ukiwa 57% na wa maji 36% na kiasi kilichobaki ni vyanzo vingine!

Hivi kiangazi na ukame ni kitu kile kile?! Au unataka kubisha kwamba hakuna ukame?!

Man, kama si JK kujenga Bomba la Gesi kutoka Mtwara hali ingekuwa MBAYA! Watu mnampa credit JPM kwa sababu ule mradi ulifanyika mwishoni kabisa mwa utawala wa JK, kwahiyo manufaa yake yameanza kuonekana wakati wa JPM, na ndo maana mnadhani JPM ndie alitatua tatizo la umeme!!

Kinyerezi I kwa mfano, tumeanza kutumia umeme wake October 25, 2015!! Na Kinyerezi I na II, zimeingiza zaidi ya 400 MW kwenye grid ya taifa, let alone Ubungo II ambayo installed capacity ni zaidi ya 100 MW!!

Hivi ulishawahi kujiuliza ukitoa hizo 500MW, huyo JPM angekuta hali gani?!

Na kwanini wakati wa huo upungufu hakuonekana nishasema hapa mara nyingi! Kwanza, SIO KWELI kwamba eti hapakuwa na upungufu!! Lakini hayo tuyaache! Ripoti ya CAG imesema wazi kwamba:-
View attachment 2017728

Hayo sio maneno yangu bali ni maneno ya CAG! Na wala sio Ripoti ya wakati wa JK au Samia bali ni wakati wa JPM mwenyewe! CAG hapo anasema hapo TANESCO walikuwa wanakataliwa kuzima mitambo na kufanya ukarabati kwa sababu hifadhi ya umeme ilikuwa ndogo to the point, kama mitambo ingezimwa, ingesababisha mgao!!

Kwahiyo ili serikali ijioneshe hakuna tatizo la umeme, ikawa inalazimisha hizo mashine ziburuzwe hivyo hivyo kwa hofu wakizima, mahali kama Dar penye watu wenye kelele nyingi, ingeingia kwenye mgao! Kwahiyo ikawa "bora punda afe, lakini mzigo ufike"!

Sasa lau kama Kinyerezi III na IV zingejengwa, hiyo hofu isingekuwepo!!

Now tell me: Katika hali ya kawaida tu, hakuna ukame wala nini, bado TANESCO walikuwa wanapigwa STOP kuzima mashine kwa sababu umeme ulikuwa hautoshi... what about chanzo kimoja kinapoathirika?

Hebu nijibu yafuatayo:-
1. Hivi kiangazi na ukame ni kitu kile kile?
2. Unabisha kwamba kina cha maji kwenye mito yetu kimepunguwa?

Look at you... "namba mnazotoa"

Hizo namba ni za kwangu mimi hadi useme "...namba mnazotoa"?

Let me guess... you're the victim of political lies kwa sababu, inaonesha unaamini zaidi kauli zinazoongelewa na wanasiasa na watu wao kuliko ripoti za kitalaamu!!

Hapo kuna takwimu kutoka National Audit Office na zingine kutoka Wizara ya Nishati; na zote hizo ni za wakati wa JPM!! Sasa zangu kivipi?

Na hilo la wapigaji... hivi nchi hii ni lini palikosekana kuwa na wapigaji?

Au nawe ni wale wanaoamini JPM alidhibiti ufisadi?! Hivi ufisadi wakati wa JK watu tulikuwa tunaufahamu vipi kama sio kupitia bungeni na kwenye vyombo vya habari?!

Hiyo awamu ya JPM mnayotaka kutuaminisha hapakuwa na ufisadi, hilo bunge lilikuwa na uwezo wa kujadili hayo mambo?
Huyo JPM wako na kikwete wako ni wanachama wa chama gani na walihudumia nchi gani?
Mmekalia siasa za watu huku watanzania wanateseka na mnaposhindwa tatua changamoto mnazozisababisha mnatafuta marehemu wa kuwasingizia, muone aibu basi.
Tunataka huduma za jamii, Bei za bidhaa zishuke pia.
Hizi porojo zenu hatuhitaji sie Watanzania mnatuchoshaaaa
 
Tanesco kama mko hapa....
Fanyeni mrudishe umeme hapa MBAGALA KIPATI,mbele ya kituo cha sabasaba na karibu na St Antony....mmekata umeme toka saa 9 alfajiri....na haujarudi mpaKa sasa.

Kama kuna hitilafu umeme umeshindwa rudi mtujuze.
 
78 Reactions
Reply
Back
Top Bottom