Uonezi katika udahili 2017, Maombi chuoni na kila chuo unalipa

Mkuu umeona mwenyewe jinsi watu hawa wanavyochangia bila hata kujua mantiki ya hoja ni nini? Mantiki ni kuwa utaratibu huo ni mzuri wa kuomba vyuo unavyoona vitakufaa kwa sababu mbalimbali ikiwemo aina ya kozi utakayo na jiografia ya mahali penyewe. Shida iko kwenye ongezeko la gharama. Wakati wa TCU tuliona wazazi wengi wa kipato cha chini hiyo fee ya 50 thou ikiwahenyesha na sasa wataingia mifukoni zaidi jee wataweza?
Tatizo la wenye fikra potofu kila aandikaye jambo huwa wanadhani anaandika kwa kujipigania yeye mwenyewe. No, sie wengine tumeshawasomesha watoto wetu na wategemezi wengi tuu lakini tunaishi kwenye jamii ambayo tunaijua iko katika dhiki kiasi gani na jaribio lolote la kuwaongezea magumu tutalisemea kwa sauti. Gharama zimeongezeka.
Kinachoshangaza ni kuwa kesho na kesho kutwa mzee wa maamuzi ya kukurukakara akijua kuwa vyuo vinafanya hivyo na kibao kinamgeukia anaweza kusimama jukwaani akasema hakuna sabau ya kuweka fee hiyo kubwa iwe 5000 kwani wanaomba online, kisha hawa wapambe upepo watageuka na kupongeza pia wakati wanakataa sasa hivi kwa vile wanajiangalia wao na sii wengine

Unajua maana ya apllication fee? kuna application fee na kuna admission fee unajua zitofautisha?

FYI application fee lazima ilipwe wakati wa maombi sababu iyo pesa ndo italipa wanaokagua hizo application zako kununulia chai na lunch na stationeries. sasa usipolipa hawa watu watalipwa na nini?

Na hii system ilikuepo kabla ya TCU kuna vyuo vilikua vinachaji 30000 na vingine 50000 na watu waliapply sasa sasa hivi mnalalamika nini wakati nyie ndo mliosema TCU inawapangia vya kusoma?

Application fee inachajiwa vyuo vyote duniani na nyingine unakuta ni gharama kuzidi hata vya hapa Tanzania.

Tusiwe twalalamika bila sababu unafanya research kwanza
 
Confidence ni muhimu Kama anaona hawezi pata UDSM aache aombe pengine sio lazima UDSM

else wakapige magoti Ikulu au MOE wabembeleze kwamba they were wrong na waombe msamaha. si walisema hawataki kupangiwa haya wajichagulie wenyewe.

By the way watu wanalalamika lakini hawajui application fee huwa zina kazi gani.

Kuwalipa wanaopitia applications posho... na kuwasaidia breakfast lunch etc kulipa umeme wa feni, taa na ac zitakazotumika kwenye room wanazofanyia mchujo, stationeries, wanaojaza majina ya successifully candidates kwenye system kuwaprintia ma admission letters etc. ndo maana kila chuo kina application fees
NIKUJIBU KWA KIFUPI TU. UONGOZI hasa wa nchi NI PAMOJA NA HEKIMA
 
Wabongo hatujielewi tunataka nini

Makandila
Issue siyo watu kutokujielewa? kuna watoto wa maskini hata hiyo sihirini ni issue kupiata, Suala la kutokupangiwa chuo sawa issue ni ada ya kuomba kujiunga na chuo, haya mambo yanawaumiza sana watz na yapo sehemu nyingi hata shule binafsi unakuta mtu shule inauweza wa kuchukuwa wanafunzi 100, lakini anachapisha form 1,000.

Fikiria ni kwa namna gani unaweza kujihakikishia kujiunga na chuo? wengine wanasema confidence unakuwa na confidence gani hapo, wewe unajua alama ulizo nazo hujui alama za mwenzio. Hivo lazima tu atalazimika kuomba chuo zaidi ya kimoja. na wabongo tulivo hapa tutarudi kwenye kujuana, kama huna mtu anayekujua lazima utachukuliwa baada ya chuo kushindwa kupata namba ya wanachuo wanahohitajika.

Utajikuta mtu ana point za kutosha kabisa anaachwa na yule wa chini yake anachukuliwa kwa sababu tu ya vimemo. Binafsi naungana na mleta mada hapa kutakuwa na shida zaidi ya TCU.
 
Kama gharama ni kubwa sana,acha ku-apply.

Kwani lazima watu wote msome elimu ya chuo kikuu,mambo mangapi umeachana nayo kutokana na ughali wake?

Go for ignorance, it's free.
 
Issue siyo watu kutokujielewa? kuna watoto wa maskini hata hiyo sihirini ni issue kupiata, Suala la kutokupangiwa chuo sawa issue ni ada ya kuomba kujiunga na chuo, haya mambo yanawaumiza sana watz na yapo sehemu nyingi hata shule binafsi unakuta mtu shule inauweza wa kuchukuwa wanafunzi 100, lakini anachapisha form 1,000.

Fikiria ni kwa namna gani unaweza kujihakikishia kujiunga na chuo? wengine wanasema confidence unakuwa na confidence gani hapo, wewe unajua alama ulizo nazo hujui alama za mwenzio. Hivo lazima tu atalazimika kuomba chuo zaidi ya kimoja. na wabongo tulivo hapa tutarudi kwenye kujuana, kama huna mtu anayekujua lazima utachukuliwa baada ya chuo kushindwa kupata namba ya wanachuo wanahohitajika.

Utajikuta mtu ana point za kutosha kabisa anaachwa na yule wa chini yake anachukuliwa kwa sababu tu ya vimemo. Binafsi naungana na mleta mada hapa kutakuwa na shida zaidi ya TCU.
ila wafahamu hii system ilikuepo kabla ya TCU?
 
Tatizo ni kulalamika kwa watanzania badala ya kuonesha njia mbadala.
Zamani, ulikuwa unaomba vyuo tofauti tofauti na unalipia application fee, watu wakasema tuwe na CAS ndipo TCU ikaanzishwa.

Hata miaka 10 haijaiisha, ninyi ao hao , mkaanza oooh oooh, TCU mara sijui hawako makini , mkatoa tuhuma bila kuonesha njia ya kusahihisha makosa au udhaifu wa TCU.

Wengine, wakamwambia hadi rais, aiondoe TCU.

Basi, rais , ameona isiwe nongwa, tatizo ni CAS ya TCU mkajibu ndiyooooooo, basi, akauliza mnataka iweje, mkajibu wenyewe, tuombe vyuoni wenyewe direct.

Tena, hata mwaka haujaiisha tangia mjirohojeshe hivyo, mmeishaanza oooh, gharama, oooh usafiri, oooh, kama kozi inahitaji watu 100 , tukaomba 300, inakuwaje!?

Ndiyo mkome. Tena, naomba vyuo viwakomeshe kabisa kwenye cut off points na idadi ya wanafunzi kwa kila faculty/ program ndiyo mkome kulialia bila sababu.
Hasira za nn,Nenda taratibu tu utaeleweka,ya nn kuongelea puani?
Hata km watu walilalamikia mfumo wa TCU,serikali nayo ilibidi iangalie changamoto zake na namna ya kutatua kabla ya kuurejesha mfumo huu haswa Gharama,sio wote waliofaulu wana pesa,na ili kuweka uhakika lazima uombe chuo zaid ya kimoja,ndio maana hata mfumo wa zaman mtu alichagua vyuo vitano.
Kama ni wa PCB huwez omba Muhimbil tu,lazma uombe na Vyuo vingine ili huku ikigoma sabb ya ushindan unaweza pata sehem nyingine.
Hili suala la gharama lingepunguzwa ili kumuwezesha hata yule Maskini kumudu kudahiliwa vyuo mbali mbali.

Philips X2560
 
Kama unajiamini jaza chuo kimoja usave pesa au acha kusoma ukiona pesa huwezi. Kama umeona hela ya application ni kubwa ungeweza kulipia ada ambayo TCU watakulazimisha kusoma chuo chenye gharama kubwa
 
hii system ilikuagapo miaka hiyo.

Ikaja TCU mkalalamikaaa weee kwamba mnapangiwa na Serikali vyuo vya kusoma na mkataka TCU isiwepo ili kila mtu achague anachotaka kusoma.

Kaja Rais anayewapenda ambaye anataka msipangiwe vyuo vya kusoma kawarudishia system mnayotaka ya kuapply moja kwa moja chuoni. Mnalalamika tena MNATAKA NINI JAMANI?

Sio lazima uapply vyuo vitatu kama uko confident chagua chuo kimoja unachokipenda
Shida niliyoona ni TCU kupangia watu kozi ambazo hawapendi?

Magufuli aliwaambia waache kuwapangia vyuo vya kusoma ingawa shida si vyuo bali nini hasa mwanafunzi anataka kusoma.... chuo chochote kinafaa ilimradi kiwe kinatambulika kisheria.

Watu wengi walipangiwa kozi wasizotaka hivyo kuzua malalamiko kuhusu mfumo wa TCU .

Mlioingia vyuoni 2010 mtakumbuka kuwa kila mtu alitakiwa ajaze kozi 12 katika vyuo vitano .. ukiangalia uhalisia hapo ni mtu kuwa na malengo na kupenda kozi 2 au 3... TCU walichokifanya ni kuwapangia watu wengi kozi ambazo hawakuzipenda kutokana na kozi nyingi kuombwa ukilinganisha na idadi ya vyuo walivyoomba.

Mfumo wa tcu ungekuwa imara ikiwa tu mwanafunzi angeomba kozi chache kwenda vyuo vingi.

Mfano: mwanafunzi kamaliza PCB aombe kozi tatu kwenye vyuo vingi like 12 hivi.

Akiomba kozi chache kama Medicine, Pharmacy Na laboratory science kwenda vyuo vingi (12) chance ya kupata chuo na kozi anayoipenda ni kubwa mno. Kama first choice ni medicine second ni phamarcy uwezekano wa kupata utakuw mkubwa kwa kuwa ame-apply vyuo vingi ingawa vigezo vya ufaulu vitazingatiwa.
Kama ingefanyika hivi kusingekuwa na malalamiko lukuki kwa kuwa wanafunzi wangepelekwa Kozi za ndoto zao.

Uhalisia uliokuwepo TCU.
Mwanafunzi huyo juu kwenye mfano amechagua kozi 12 katika vyuo vitano tofauti tofauti huku passion yake ni hizo kozi 3 tu... kwa kuwa alilazimika kujaza kozi nyingi unakuta kapelekwa Agricultural general ambayo ilikuwa ya 11 kwenye list ya kozi alizo zijaza... hakuipenda lakini alihakikisha kuwa nafasi zote zinazotakiwa zijazwe amejaza.

Mtu huyo lazima alalamike na aone TCU haofai ... imeacha machaguo yake bora ya mwazo na kumtupia kozi asiyoipenda au hana future nayo.

Conclusion yangu: mfumo wa TCU ulikuwa mzuri ikiwa tu mwanafunzi angejaza Kozi chache kwenda vyuo vingi..

Shida si kuchaguliwa vyuo as long as kama nilikuwa na dream ya kuwa Daktari na nimeweza kusomea hiyo fani iwe nimesomea muhimbili, saint John au Hata kama mzumbe wanatoa udaktari ningefurahi kusoma hapo.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo mkome kurohoja bila facts!! Wenyewe , mlikuwa kila siku kwenye majukwaa na mitandao ya kijamii mkiomba TCU iondolewe ama msifanye udahili kupitia CAS ya TCU hayo hamkuyawaza!!?

Sikia, hata ulaya, USA, Asia unalipia application fees kulingana na vyuo unavyohitaji na kila chuo unalipia. Na hakuna huo ujinga wa eti ulipie baada ya kuchaguliwa, unalipa unasubiria kama hujakidhi vigezo application fee yako ndiyo kwa heri hiyo.

Rais, Dr Magufuli, nampongeza sana , maana aliwasikiliza ninyi wenyewe na kuwapa mnachokitaka. Basi bila hiyana, akainua kalamu akaandika na akatamka basi mmekipata mlichokitafuta na ndivyo mlivyotaka.
Shida si kuchagua vyuo tunavyotaka shida ni kuchagua kozi tunayotaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ka watz sio wafikiriaji kwa yanayokuja mbele hiki kitendo cha kufuta TCU mi na kuweka kutma maombi ktk chuo husika mi nishajuaga kwamba hapa watu wtz watapigwa hela tena nying hii na kwel hiyo inaonekana..aya bhn maisha ya sasa ni yakinyonyaji tu..
 
Tatizo ni kulalamika kwa watanzania badala ya kuonesha njia mbadala.
Zamani, ulikuwa unaomba vyuo tofauti tofauti na unalipia application fee, watu wakasema tuwe na CAS ndipo TCU ikaanzishwa.

Hata miaka 10 haijaiisha, ninyi ao hao , mkaanza oooh oooh, TCU mara sijui hawako makini , mkatoa tuhuma bila kuonesha njia ya kusahihisha makosa au udhaifu wa TCU.

Wengine, wakamwambia hadi rais, aiondoe TCU.

Basi, rais , ameona isiwe nongwa, tatizo ni CAS ya TCU mkajibu ndiyooooooo, basi, akauliza mnataka iweje, mkajibu wenyewe, tuombe vyuoni wenyewe direct.

Tena, hata mwaka haujaiisha tangia mjirohojeshe hivyo, mmeishaanza oooh, gharama, oooh usafiri, oooh, kama kozi inahitaji watu 100 , tukaomba 300, inakuwaje!?

Ndiyo mkome. Tena, naomba vyuo viwakomeshe kabisa kwenye cut off points na idadi ya wanafunzi kwa kila faculty/ program ndiyo mkome kulialia bila sababu.

Umeandika vizuri sana.Nazidi kupata picha ni jinsi gani sisi waafrika hatuendelei.Kuanzia mwananchi wa chini mpaka kiongozi.Wote hatujielewi.Na hapo ndipo utaelewa zaidi ya aina ya shida zetu na maendeleo yetu kwanini tupo hivyo.Nazidi kuamini zaidi mbali zaidi,kuwa mwafrika atabaki kuwa mwafrika.Kuna siku mkuu ataambiwa mabomu hayajalipuka siku nyingi na ataamrisha yalipuliwe kisa tu baadhi ya watu wasiojielewa wametaka.

Kama ndivyo ilivyo kuwa sasa kwa CAS basi tutegemee mambo mengi sana katika hizi nchi zisizo na muelekeo wa dira maalumu.Sipingani na wewe,nimekuelewa sana.Ila ukikaa ukaona tulichokitaka utajua ziadi na zaidi.Na ndivyo wanavyofanya vyuo kwa sasa na kama unavyosema.
 
Mliwaponda sana TCU.

Sasa hivi ndio mtaona umuhimu wao.

Bora wangetatua changamoto chache zilizokuwepo ila sio hiki walichokifanya.

 
Umeandika vizuri sana.Nazidi kupata picha ni jinsi gani sisi waafrika hatuendelei.Kuanzia mwananchi wa chini mpaka kiongozi.Wote hatujielewi.Na hapo ndipo utaelewa zaidi ya aina ya shida zetu na maendeleo yetu kwanini tupo hivyo.Nazidi kuamini zaidi mbali zaidi,kuwa mwafrika atabaki kuwa mwafrika.Kuna siku mkuu ataambiwa mabomu hayajalipuka siku nyingi na ataamrisha yalipuliwe kisa tu baadhi ya watu wasiojielewa wametaka.

Kama ndivyo ilivyo kuwa sasa kwa CAS basi tutegemee mambo mengi sana katika hizi nchi zisizo na muelekeo wa dira maalumu.Sipingani na wewe,nimekuelewa sana.Ila ukikaa ukaona tulichokitaka utajua ziadi na zaidi.Na ndivyo wanavyofanya vyuo kwa sasa na kama unavyosema.


Ndiyo maana, huwa napenda kuandika kuwa inahitaji hekima na elimu kuhusu mambo mengi sana.
Hii itasaidia ili kabla hatujaomba au hatujapinga jambo, tuhakikishe kuwa tunaelewa faida na hasara na kupima pande zote mbili.

Sasa tena naona wananza kuhamisha magoli kwa kusema kuwa hawakukataa TCU kudahili wanafunzi, bali walihitaji TCU isiwapangie kozi tofauti na walizoomba.

Hii nalo, ukiliangalia vizuri pana kozi daima wanadahili wanafunzi wachache kwa sababu ya aina ya kozi na ufundishwaji wake.

Hapo napo, watakuja na ngojela mpya kuwa walikuwa na point nzuri ila hawakudahili. Bila wao kuangalia kuwa kozi hiyo inadahili wanafunzi kiasi kwa kila intake moja.

Any way, afrika na Tanzania watu wengi ni vilalamishi na kuwafurahisha ni kazi ngumu sana.
 
Yaan kuomba tu chuo unalipishwa? Kwanini wasilipe admission fee baada ya kuchaguliwa chuo husika?

sent from Sanduku la Posta using JamiiForums mobile app
 
Yaan kuomba tu chuo unalipishwa? Kwanini wasilipe admission fee baada ya kuchaguliwa chuo husika?

sent from Sanduku la Posta using JamiiForums mobile app


Kulipia application fee ni kawaida sana kwa vyuo almost vyote duniani.

TCU ilikuwa inwasaidia , watanzania kwa kujifanya much know na kuchanua midomo wakaikataa TCU.
Sasa ngoja, watatuliwe wallet zao na vyuo na bado wasipate nafasi maana kozi zina cut off points pamoja na idadi y kudahili kwa intake moja kila mwaka.

Wataikumbuka , TCU kama vile baadhi wanamkumbuka JK.
 
Kujadiliana na MTU ambaye hajitambui ni shida. Sikia kijana, serikali haifanyi kazi zake kwa kukomoa RAIA wake kwa vile eti waliwahi kulalamika. Jee walio lalamika ni wote?mbona Leo kuna wanaolalamika Jpm ni dikteta na hajajiuzulu na kusema kuna watu wanalalamika?
Ni wajibu wa serikali kutafuta unafuu kwa watu wake.
Mfumo huu mpya ni mzuri, lakini kuna haja gani kuweka gharama kubwa kwa maombi ambayo hayana uhakika wa kupata?
Tuwazungumzie wale wazazi wanao ishi chini ya dola moja kwa siku sio sie ambao tuna akiba kwenye mabenki hata hatujui ni ngapi. Huo ndii uzalendo


Kwahiyo mkuu unapendekeza iwe pesa ngapi kuapply chuo 10000???
Au bure ?
 
Watanzania tunapenda sana kulalamika. Huo mfumo tuliutumia sisi miaka yetu, serikali ikabadili mfumo na watu wakalalamika, leo wameleta kile mlichotaka bado mnalalamika.
 
Back
Top Bottom