Uonezi katika udahili 2017, Maombi chuoni na kila chuo unalipa

Ndugu yangu kabla ya kujibu tafadhali jaribu kutafakari angalau kidogo,mnaweza wengi mkawa na sifa stahiki na kuchagua course na chuo kimoja kuzidi uwezo wa chuo husika, na hiyo inatokea hivyo basi, kuwa salama inakubidi huombe zaidi ya chuo kimoja, na kinyume cha hapo pia kuna vyuo vinakosa waomba wa kutosha.
NB : Na kwa faida yako na wanajamii wengine TCU bado ipo na inaendelea na shughuli zake za udahili kwa staili tofauti, baada ya waombaji kujaza maombi yao na kuchaguliwa katika vyuo husika, majina ya waliochaguliwa yatawafikia TCU kwa ya kuhakiki kabla ya vyuo husika kuruhusiwa kutangaza wanamaombi waliochaguliwa.
Source : Tafadhali google Admission Procidure for 2017 / 2018 Admission Cycle.
Hivi nani amekuambia TCU inafutwa au haitaki? Umeelezwa kuwa mfumo mpya unawajibisha, kama ilivyokuwa zamani, mdahiliwa kufikiri kimkakati kabla ya kuamua university ipi aombe kudahiliwa kwa kozi anayoitaka kusoma. universitie zinatakazokosa kupta wanafunzi wa kudahili kuna maanisha jambo moja kubwa; kwamba mbele ya wadahiliwa, universities hizo zinaonekana kutokuwa na hadhi (not competitive) ya kuendesha mafunzo ngazi ya chuo kikuu. Sasa hli si suala la wanafunzi bali wamiliki wa vyuo hivyo. Wewe ni msemaji wao?
 
Serikali imegundua namna ya kuongeza mapato, badala ya kutumia 50,000 kutuma maombi katika vyuo vyote nchini sasa kila chuo ni 50,000 ukituma mamombi vyuo vitano zinakutoka 250,000! Familia ngapi zenye uwezo kama huu nchini!?

Hakika Watanzania sasa tunasomeshwa namba na nashangaa wale wanaounga mkono kila kinachofanywa na serikali. Kufikia mwaka jana ili vijana wetu wasome vyuo vikuu maombi yalikuwa yanafanywa sehemu moja tuu nayo ni TCU na mzazi ilikuwa unalipa shs 50,000/ pekee ukisubiri nafasi ya kusoma kijana atapangiwa wapi.

Sasa hivi serikali inayojinasibu kujali raia wake imesema kila mtu ata apply chuo atakacho mwenyewe, sio jambo baya lakini sasa wamelifikiria hili jambo la kulipa wakati wa maombi wakati mtu hana hakika ya kupata nafasi katika chuo anachoomba?

Maana ili kujipa nafasi ya kuweza kupata chuo mwanafunzi atawajibika kuomba vyuo vingi kadiri awezavyo na hapo hapo lazima alipe application fee kila chuo kwani hana hakika kipi atapata.

Kwa hili wazazi tulikuwa tunalipa 50000/ sasa tunaweza kujikuta tunalipa hata milioni, jee huku ndio kumjali mwanachi? Kwa nini malipo yasifanywe kama admission fee kwa wale watakao chaguliwa tuu?

Haya mambo ya kutekeleza mawazo ya mtu mmoja anayokurupuka nayo na kuzoza majukwaani yanatuletea shida kubwa sana na kufanya maisha ya Watanzania kuwa ya misukosuko.
 
Serikali ipange ada elekezi la sio ivyo masikini wengi wanaumia
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Target kile unachoona unafit wewe kusoma, huo utaratibu ulikuwepo enzi zetu.
 
Serikali imegundua namna ya kuongeza mapato, badala ya kutumia 50,000 kutuma maombi katika vyuo vyote nchini sasa kila chuo ni 50,000 ukituma mamombi vyuo vitano zinakutoka 250,000! Familia ngapi zenye uwezo kama huu nchini!?
Mkuu umeona mwenyewe jinsi watu hawa wanavyochangia bila hata kujua mantiki ya hoja ni nini? Mantiki ni kuwa utaratibu huo ni mzuri wa kuomba vyuo unavyoona vitakufaa kwa sababu mbalimbali ikiwemo aina ya kozi utakayo na jiografia ya mahali penyewe. Shida iko kwenye ongezeko la gharama. Wakati wa TCU tuliona wazazi wengi wa kipato cha chini hiyo fee ya 50 thou ikiwahenyesha na sasa wataingia mifukoni zaidi jee wataweza?
Tatizo la wenye fikra potofu kila aandikaye jambo huwa wanadhani anaandika kwa kujipigania yeye mwenyewe. No, sie wengine tumeshawasomesha watoto wetu na wategemezi wengi tuu lakini tunaishi kwenye jamii ambayo tunaijua iko katika dhiki kiasi gani na jaribio lolote la kuwaongezea magumu tutalisemea kwa sauti. Gharama zimeongezeka.
Kinachoshangaza ni kuwa kesho na kesho kutwa mzee wa maamuzi ya kukurukakara akijua kuwa vyuo vinafanya hivyo na kibao kinamgeukia anaweza kusimama jukwaani akasema hakuna sabau ya kuweka fee hiyo kubwa iwe 5000 kwani wanaomba online, kisha hawa wapambe upepo watageuka na kupongeza pia wakati wanakataa sasa hivi kwa vile wanajiangalia wao na sii wengine
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tanzania watu wengi sana ni vilalamishi sana, mliikataa TCU sasa udahili wa moja kwa moja vyuoni nao mnaanza kuleta nongwa!?

Ngoja muisome namba ndiyo mtakoma.
Kweli mzee,wao ndo walikua wa kwanza kuilalamikia TCU,mara ooh inapiga dili na vyuo binafsi,mara watoto wetu wanapelekwa vyuo ambavyo hawajaviomba,sasa watulie dawa iwaingie na wachague vyuo wanavyovitaka bila kupitia TCU.
 
Naunga mkono hoja Mkuu. Wangeweza kabisa kushusha gharama za kuapply kila chuo ili maximum ibaki hiyo hiyo 50,000. Kwa mfano wangeweza kusema iwe 5,000 kwa kila chuo kama ulivyosema hii ingewasaidia sana wale wenye familia za vipato vya chini. Tatizo kubwa la nchi yetu Mkuu sasa hivi ni UZWAZWA ULIOKITHIRI na watu kuandika kwa kujifanya wanajua kila kitu au kwa kuangalia hali zao tu bila ya kujali hali za Watanzania chungu nzima ambao hali zao kiuchumi ni za chini mno.

Mkuu umeona mwenyewe jinsi watu hawa wanavyochangia bila hata kujua mantiki ya hoja ni nini? Mantiki ni kuwa utaratibu huo ni mzuri wa kuomba vyuo unavyoona vitakufaa kwa sababu mbalimbali ikiwemo aina ya kozi utakayo na jiografia ya mahali penyewe. Shida iko kwenye ongezeko la gharama. Wakati wa TCU tuliona wazazi wengi wa kipato cha chini hiyo fee ya 50 thou ikiwahenyesha na sasa wataingia mifukoni zaidi jee wataweza?
Tatizo la wenye fikra potofu kila aandikaye jambo huwa wanadhani anaandika kwa kujipigania yeye mwenyewe. No, sie wengine tumeshawasomesha watoto wetu na wategemezi wengi tuu lakini tunaishi kwenye jamii ambayo tunaijua iko katika dhiki kiasi gani na jaribio lolote la kuwaongezea magumu tutalisemea kwa sauti. Gharama zimeongezeka.
Kinachoshangaza ni kuwa kesho na kesho kutwa mzee wa maamuzi ya kukurukakara akijua kuwa vyuo vinafanya hivyo na kibao kinamgeukia anaweza kusimama jukwaani akasema hakuna sabau ya kuweka fee hiyo kubwa iwe 5000 kwani wanaomba online, kisha hawa wapambe upepo watageuka na kupongeza pia wakati wanakataa sasa hivi kwa vile wanajiangalia wao na sii wengine
 
Nadhani hii ni changamoto kwa mama ndalichako, application ziwe bure ila admision ndio ulipie
 
Kama huko nyuma alisoma bure kwakuwa mtoto wa fukara sasa atatoa wapi hiyo elfu hamsini?
 
Sio lazima uapply vyuo vitatu kama uko confident chagua chuo kimoja unachokipenda
Wanafuzi karibu 80% wanapenda kusoma University of Dar es salaam. Je wote hao wakiomba chuo kimoja ambapo uwezo wa chuo ni 50% tu. Hii 30% kwa ushauri wako watakosa nafasi mpaka mwakani waombe tena kwingine au palepale mana walifuata ushauri wako wa kuomba chuo kimoja tu na SIFA WANAZO. Sijui unaona tatizo hapo.
 
Watanzania mnashangaza!
Mlikashfu sana utendaji wa TCU mkaona hakuna la maana wanalolifanya.
mara ooh wanatupangia vyuo tusivyotaka
Sasa mmepewa uhuru nendeni mkaapply wenyewe mnalialia tena
Mnataka nini??
Kuapply iwe bure? au uchague chuo kimoja hata mkiwa milioni3 mpelekwe tu na chuo hakina uwezo wa kuwabeba wote???
 
Kweli mzee,wao ndo walikua wa kwanza kuilalamikia TCU,mara ooh inapiga dili na vyuo binafsi,mara watoto wetu wanapelekwa vyuo ambavyo hawajaviomba,sasa watulie dawa iwaingie na wachague vyuo wanavyovitaka bila kupitia TCU.

Ndiyo, mkuu.

Ngoja wapasuliwe bila dawa za ganzi wala vipimo. Ndiyo wakome.
 
Wanafuzi karibu 80% wanapenda kusoma University of Dar es salaam. Je wote hao wakiomba chuo kimoja ambapo uwezo wa chuo ni 50% tu. Hii 30% kwa ushauri wako watakosa nafasi mpaka mwakani waombe tena kwingine au palepale mana walifuata ushauri wako wa kuomba chuo kimoja tu na SIFA WANAZO. Sijui unaona tatizo hapo.
Confidence ni muhimu Kama anaona hawezi pata UDSM aache aombe pengine sio lazima UDSM

else wakapige magoti Ikulu au MOE wabembeleze kwamba they were wrong na waombe msamaha. si walisema hawataki kupangiwa haya wajichagulie wenyewe.

By the way watu wanalalamika lakini hawajui application fee huwa zina kazi gani.

Kuwalipa wanaopitia applications posho... na kuwasaidia breakfast lunch etc kulipa umeme wa feni, taa na ac zitakazotumika kwenye room wanazofanyia mchujo, stationeries, wanaojaza majina ya successifully candidates kwenye system kuwaprintia ma admission letters etc. ndo maana kila chuo kina application fees
 
Umelalamika tu, lete ushauri wako, Maoni yako, mpango Kazi.

Vinginevyo ni uwendawazimu tu


Sent using Jamii Forums mobile app

Mimi nadhani mwendawazimu ni wewe, ikiwa umeshindwa kupata hoja katika taarifa hiska, siyo kila kitu ucomment Ch****p mnakera katika mambo ya msingi lazima mlete bangi. Yeye ameongea kile kinachoonekana na kiko wazi. Mtu anapoomba chuo hana uhakika wa kupata nafasi kwa sababu hajui ni wangapi wataomba na wakiwa na sifa zipi, hivo lazima aombe chuo zaidi ya kimoja ili angalau awe na uhakika wa kupata chuo kimojawapo. Lakini wewe unakurupuka tu, She****n Period
 
Watanzania mnashangaza!
Mlikashfu sana utendaji wa TCU mkaona hakuna la maana wanalolifanya.
mara ooh wanatupangia vyuo tusivyotaka
Sasa mmepewa uhuru nendeni mkaapply wenyewe mnalialia tena
Mnataka nini??
Kuapply iwe bure? au uchague chuo kimoja hata mkiwa milioni3 mpelekwe tu na chuo hakina uwezo wa kuwabeba wote???

ndio najaribu kuwambia kama wanaona haiwafai sahivi waende wanatambaa kwa magoti mnaka MOE wakiomba System ya TCU irudishwe
 
Back
Top Bottom