Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Sisi wakazi wa sirari na wilaya ya tarime kwa ujumla tumepatwa na tatizo la bomoa bomoa na zoezi hili limeanza 2march mwaka huu baada ya tangazo la kupewa siku saba tuwe tumebomoa makazi yetu pasipo fidia yoyote,naamini mnajua ugumu wa maisha uliyo kwa sasa .Hawa wakubwa wanatumia umasikini wetu na uelewa mdogo tulionao kutunyanyasa kwa kutumia mabafu kuvunja nyumba zetu na kutufanya tuwe wakimbizi ndani ya nchi yetu,kibaya zaidi wanaziacha nyumba za viongozi wetu kama madiwani na baadhi ya maafisa .Ombi letu ni kuwaomba ndugu zetu wenye uelewa wa haya mambo mtusaidie na kikubwa zaidi tutafurahi ujumbe wetu huu ukiwafikia wakubwa hata kwa njia ya blog zetu na kokote pale mnapokutana nao ili wajue kwamba ,vijana wao wanaosimamia zoezi hili hawatutendei haki na kama kuna fedha ziliwahi kutolea na serikali kufidia hasara hizi kwa raia basi hawa watu waoa watakuwa wamekula na kinachofanyika sasa ni kutimiza wajibu wao kwa kunyanyasa rai.Tunaomba msaada wenu kutuwekea file tuliloambatanisha kwenye hii thread muisambaze ili wakizipitia walione na raia wote wapenda haki wajue kuwa kuna ndugu zao wanateseka huku vijijini.kama mtaguswa mnaweza kutufikishia ujumbe wetu kwa wahusika pia. Samahani tumewatumia nyie kama kaka zetu na kwa kuwa tunatambua msaada wenu katika kutetea hazi zetu,tuliowanyonge.Aksanteni
attachment
View attachment 24321
attachment
View attachment 24321