Uoga, kukosa ujasiri na uthubutu kwetu ni matokeo ya malezi mabovu ya kizamani

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,581
46,178
Watanzania wengi ni watu waoga wasioweza kuhoji au kufuatilia kupata haki zao kwa mambo mengi ya msingi yanayogusa maisha yao mpaka mwisho.Kuna baadhi ya watu ni vigumu hata kumhoji au kujadiliana na daktari anayemtibu afya yake kwa kuamini daktari anajua kila kitu na sio vyema kupendekeza jambo lingine kwake!

Kwa upande mwingine raifa letu linaweza kuwa ni mojawapo ya mataifa yanayoongoza kwa kuwa na mashujaa wengi walio nyuma ya Keyboard.

Sehemu kubwa ya hali hii ni utamaduni wetu wa muda mrefu ambao

Moja, Umewaaminisha watoto na vijana kwamba watu wazima hawakosei na mara zote watu wazima ni watu wenye busara sana.

Mbili, Umehusudu viboko katika malezi; Malezi ya kuchapa watoto kuanzia nyumbani mpaka shuleni. Kuchapwa kwetu kumejenga halia mbaya sana ya kutojiamini na hofu katika maeneo mengi ambayo tulipaswa na tunakuwa na haki ya kuhoji na kujadiliana katika hali ya kawaida tu na wenye mamlaka.

Tusipochukua hatua mahususi kuondokana na huu utamaduni tutaendelea kuwa taifa la wanyonge kwa muda mrefu sana.
 
Ukisema mawazo yako : Huyu dogo anajifanya mjuaji sana.

Ukikaa kimya: Huyu dogo muuza chai tu hana analojua.

_ Ukifuata matakwa ya walimwengu lazima uwe muoga, walimwengu hawaeleweki sababu wenyewe hawaelewi wanataka nini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiulizwa swali ukanyamaza: Yaani nakuuliza unaninyamazia?

Ukiulizwa swali ukajibu: Unanijibu!??
 
Watanzania wengi ni watu waoga wasioweza kuhoji au kufuatilia kupata haki zao kwa mambo mengi ya msingi yanayogusa maisha yao mpaka mwisho.Kuna baadhi ya watu ni vigumu hata kumhoji au kujadiliana na daktari anayemtibu afya yake kwa kuamini daktari anajua kila kitu na sio vyema kupendekeza jambo lingine kwake!

Kwa upande mwingine raifa letu linaweza kuwa ni mojawapo ya mataifa yanayoongoza kwa kuwa na mashujaa wengi walio nyuma ya Keyboard.

Sehemu kubwa ya hali hii ni utamaduni wetu wa muda mrefu ambao

Moja, Umewaaminisha watoto na vijana kwamba watu wazima hawakosei na mara zote watu wazima ni watu wenye busara sana.

Mbili, Umehusudu viboko katika malezi; Malezi ya kuchapa watoto kuanzia nyumbani mpaka shuleni. Kuchapwa kwetu kumejenga halia mbaya sana ya kutojiamini na hofu katika maeneo mengi ambayo tulipaswa na tunakuwa na haki ya kuhoji na kujadiliana katika hali ya kawaida tu na wenye mamlaka.

Tusipochukua hatua mahususi kuondokana na huu utamaduni tutaendelea kuwa taifa la wanyonge kwa muda mrefu sana.
Ukweli ni kwamba.

Mtoto anapokuwa na ujasiri wa kuongea na kujenga hoja mbele ya wazazi wake basi hawezi kushindwa kuyafanya hayo mbele ya wasiokuwa wazazi wake.

Mtoto akiweza kukutukana mzazi basi jua anaweza na kuwatukana wengine pia.

Wazazi wajitahidi kuhakikisha watoto wao wanaweza kufanya mbele yao kile ambacho wangependa watoto hao wafanye mbele ya watu wengine wasiokuwa wazazi.
 
Back
Top Bottom