Unyonyaji - That forgotten term...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Kama kuna neno ambalo leo tunaliogopa kuligusa ni neno "unyonyaji". Kimsingi neno hili lilitokana na dhana ya jinsi kupe anavyoishi kwa kunyonya "host" wake kama ng'ombe, mbwa n.k Kwa maneno mengine mnyonyaji ni mtu ambaye anatumia kila mbinu kujitajirisha kwa kutumia "migongo" ya wengine.

Mwanzoni mwa jamhuri yetu wanyonyaji tuliwaimba na kuweka misemo kama "usiwe mnyonyaji kama kupe" tukiwahimiza watu wafanya kazi au wale kutokana na jasho lao. Tukasema kuwa watu pekee ambao wanastahili kuishi kwa jasho la watu wengine ni watoto, wagonjwa, na wazee ambao wameshachumia juani. Tukawakatalia watu wengine wote ambao wanataka kuishi "kwa njia za mkato".

Hata hivyo baada ya mabadiliko ya kiuchumi yaliyotokea tabaka la wanyonyaji limeanza kujitokeza kwa kiasi kikubwa ambapo kuna watu ambao pasipo kufanya kazi (biashara au kuchakarika kihalali) wanatumia nafasi zao na vyeo vyao kutengeneza fedha ya haraka haraka.

Ni hapo ndipo tumeanza kuona kundi la watu tuwaitao "mafisadi". Wakati neno fisadi linatumika kuelezea kila aina ya uovu katika utumishi wa umma (rushwa, wizi, ubadhirifu, matumizi mabaya ya cheo, ofisi au jina n.k) neno "mnyonyaji" lilikuwa linatumika kuelezea mtu ambaye kimsingi anavuna asichopanda na anameza asichotafuna.

Mnyonyaji ni mtu ambaye hana wasiwasi wa maisha yake kwa sababu ametegesha mirija yake kwenye mabenki, ofisi, n.k ambapo hata akiwa katika ziara ya Rais au akikaa kwenye kiti chake cha ngozi nyeusi mirija hiyo inaendelea kufyonza kama ina kichaa. Mnyonyaji haitaji kufanya kazi yoyote isipokuwa kuweka mrija huo mdomoni na kama mtu anayefyonza ulanzi au mzee aliyekalia kibuyu cha chimpumu au yule anayepulizia mbege basi anajinoma taratibu huku mashavu yake yakitanuka kama chura apigaye mluzi!

Tunachoona sasa hivi ni kuwa wanyonyaji ambao tuliwakatia mirija mwaka 1967 ili angalau na wengine tuweze kunenepa ndio wamerudi kwa ari na nguvu mpya na sasa hivi wananyonya huku wameinua miguu juu kwani wanajua hawanyonyi peke yao. Wakati umefika wa kuchora katuni ya "wanyonyaji mambo leo" ambao wamemzunguka Mtanzania na mirija yao mdomo wakimfyonza kama vile mbu anavyonya damu kama anatumia drill ya kufyonza mafuta!

Wanyonyaji hawa weusi, leo wanasimama wakijua kuwa wanalindwa na hakuna mwenye ujasiri wa kuifyeka mirija yao na kuwakatisha uhondo wao huo. Cha kuudhi ni kuwa sisi Watanzania ndio tumekaa pembeni na kupiga kelele lakini ni kelele za kushangaa siyo kukasirika na kutaka kuikata mirija hiyo. Ndio maana hadi leo hii tunaendelea kuwalipa dowans, Mkapa ameendelea kushika mrija wa Kiwira, na wengine wameshikilia mirija yao huku baadhi yao wakishikilia mirija kwenye kila kidole huku wakicheka cheka na kucheua mafuta yanukayo!

Kinachoendelea si ubepari jinsi unavyoeleweka Magharibi ambapo unajitahidi kuonesha angalau huruma kwa wanyonywaji; wa kwetu ni unyonyaji unaojifanya ni ubepari! Ni nani atakayethubutu kukata mirija hii na kuwakatisha wanyonyaji hawa uhondo wao! Ni nani ambaye yeye mwenyewe si mnyonyaji atakayeona uchungu wa kile kinachoendelea?

Je, mfanyabiashara na mwekezaji anaweza kufanya biashara yake vizuri na akapata faida bila kuwa mnyonyaji wa kutupwa. Je tunaweza kuwaacha watunyonye ilimradi wanatulisha na tunanenepa kidogo kuliko wakitunyonya tukiwa kimbaumbau!? Tufanye nini ili tuwanyang'anye mirija hiyo au tufanye nini ili tuweke machujio kwenye mirija hiyo ili wanapofyonza basi wasivyonze vyote!?

Au tukubali tu kuwa wanyonyaji wana haki ya kutunyonya kwa sababu tumeweka wenyewe migongo yetu wazi ili watunyonye huku tumeipakaa mafuta ili kuitamanisha? Je tuwaache watunyonye kwa sababu wanaweza na jaribio lolote la kutishia kukata mirija hiyo litakutana na upinzani kuwa tunataka kurudia "utaifishaji" na tunataka kutishia wawekezaji?
 
nafikiri watz kunyonywa kuna karaha fulani wanakaona mana hata kama kupiga kelele huwa zina sahaulishwa kwa kitu kidogo sana sasa hapo ndio ndio kupe anapo papenda. ila nafikiri maumivu yamesha anza ingia sasa sijui ni its too late kwamba damu imekwisha!!!!!
 
Yawezekana tumepigwa ganzi... unajua mbu akitaka kukunyonya anaweka tu enzyme fulani hivi na kukupiga ganzi kwanza basi anauteremsha mrija wake kama drill mashine halafu anafyonza weeeee.. pale anapochomoa ndio wewe unasikia maumivu... sasa hivi nadhani tumepigwa ganzi; ndio maana hatujakasirika..!
 
Wazungu walitunyonya...wenzetu na wenyewe wanatunyonya....now conclude yourself...
 
Hii mirija mipya ni tofauti na ile ya kizamani.
Hii ina vipump vidogo ambavyo yule anayenyonya haitaji hata kutumia mashavu yake...unawasha switch tu na kutulia pembeni.
 
Hii mirija mipya ni tofauti na ile ya kizamani.
Hii ina vipump vidogo ambavyo yule anayenyonya haitaji hata kutumia mashavu yake...unawasha switch tu na kutulia pembeni.

Insurgent ulipotelea wapi mkuu!! karibu na tena..
 
Kuna ushahidi mkubwa kuwa mwanadamu na pilika pilika zake zote kuwa, kamwe hataweza kuikana asili yake ya UTU na akabaki salama.

Kipindi chote wanyama wamebaki kuwa wanyama, mimemea imebaki kuwa mimiea na madinini yamebaki kuwa madini. Katika hivi hakuna kilichojaribu kukana na kusaliti asili yake.

Ni mwanadamu pekee yake aliyejaribu kuukana UTU wake ambayo ndio asili yake kuu na kutaka kujivika tabaka la viumbe wengine. Kamwe hili halitafanikiwa.

Mwanadamu hana uchaguzi, LAZIMA ADHIBITISHE UTU WAKE kila sekunde ya maisha yake....vinginevyo UTU aliozaliwa nao uta mtoka na kuwa kwenye ngazi ya viumbe wengine..kama mnyama na kadhalika, na hapo ndipo chimbuko la kila tatizo linapijitokeza.

Tatizo la mwandamu kuukana UTU iliyoasiliyake....hatakwepa majanga yote makuu ndani ya jamii. Mwandamu hatambui kuwa vita hiyo hataiweza.... Itamzalia magonjwa, ujinga na maradhi...nk

Unjoyaji sio utu. .. unjonyaji ni njia ya kuukwepa UTU.

Ujambazi wa kutumia kalamu na akili..(UFISADI)..sio utu! ni escape chanel away from UTU!!

Unapokuwa kiongozi na ukawaongoza watu kukiuka asili yao...Hutabaki salama hata chembe, bila kujali chama au wadhifa wako.

Kuna ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa Mwanadamu anazaliwa mtu ..lakini wengi hufa ...sio watu….wengi wanakufa wanyama. ..hii inapingana kabisa ..na dhana ya Evolution..kuwa wanyama hugeuka watu. Ukweli ni kuwa siku hizi watu hugeuka wanyama. Ndio hao wanyonjaji na mafisadi. Nafikiri uongozi wa juu wa Tanzania kwa sasa unaongoza. Ni nani asimameme abishe??? Tumuone!! Tumchambue ..Ajitokeze tunamakribisha!!

Niseme kuwa hawa wapinga UTU ...bila kujali staili wanayokuja nayo... wajue kuwa hawatabaki salama. waje na kuugana na wapina UTU wa kimataifa kumuumiza mtanzania, waje na viporojo vyovyote…wajue kuwa hawatabaki salama. nafikiri wananielewa.

Kama ni mfanya biashara ..unaweza kufanya biashara yako..kama kini cha kueleleza Utu wako..na pia unaweza kufanya hivyo ..kuukana utu wako na kuumiza wa watu wengine....hiyo haikubaliki. Hiyo ni kupina asili yako na hilo ni kosa la jinai. Nafikiri hata kwa MUNGU!

Jambo la kufanaya! Kuwatokomeza wapinga UTU na wageuka wanyama kupitia bishara, uogozi nk. Nasemea hawa wa nyumbani Tanzania!

Jibu liko kwenye UTU wetu!

Ni utu uliotakata na kuumua kuwa SASA NI WAKATI wa KUUTUMIA NA KULETA MAPINDUZI YA KIUTU NA KIBINADAMU!

Ni wananchi kusema sasa basi.

Nguvu ya UTU inaweza hata kuzima bomu la nuk"

Watu ni utu, hayo ni maneno ya wakubwa waliotutangulia.

Watanzania wengi bado ni watu..wenye utu!

Ni umoja wa nguvu ya watu itakayo wapindua na kuwaangamiza wapinga utu walioshamiri kama wadudu kwenye mwili wa mzoga uliokufa….Nguvu hii ya UTU wa mtanzania bado ni imejisheni kwnye jamii yetu ya wantanzania inabidi kuwa ACTIVETED TU!

Nguvu ya watu na utu wao watakapoamua hata kufanya mapinduzi ya aina yeyote, jibu ni kuwa ushindi upo! Wachilia mabali hata huo utaifishaji peke yake..chochote kikubwa chaweza kufanyika...na ninavyojua mimi na kutokana na ishara za nyakati siku sio nyingi hili halitaepukika. Mafisadi .. Ujembe ndio huo!!

Siiogelei haya kwa dhana ya kisiasa!

La hasha!

Umakini wa ufuatiliaji unaashiria kuwa kuna kiwango mwanadamu hawezi kupitiliza kwa kufanya mzaha wa kujigeuza Mnyama na kuukana utu wake! Kikomo hakipo mbali. Hasa kwa nyie viongozi wa Tanzania ambao mnajua kuwa shina la taifa hili ni UTU uliotukuka

Viongozi wote wa kitanzania walio na akili njema. Wajue asili ya utanzania. wajue kuwa asili ya utanzania ni UTU.

Wajue kuwa alama ya utu kwa taifa la Tanzania ni alama ya mwenge wa uhuru. alama ambayo imepekuliwa kisanyansi na kukutwa kuwa inasimamia UTU!

Ni alama iliyoko kila kona ya nchi… Mafisadi mlikuwa wapi na hamkuona hili!!??

Iko kila kwenye kofia ya askari wa jeshi la Tanzania.

Iko kwenye nembo ya serekali.

Iko kila kwenye kila kumbukumbu ya Taifa hili.

Mafisadi watambue kuwa vijana wa leo wataiulizia ...hii inamaana gani? wata tafiti na watagundua. Mafisadi watajaribu kubadili kila kitu...na kuficha nyaraka nk.lakini sio alama hii Ya UTU wa Mtanzania. Itabidi wajieleze kwa nini iko kwenye nebo ya serekali pale ikulu!! Au mnataka kuibadisha? It’s too late!

Kilio cha UTU sasa ni kikubwa kuliko wakati wote.

Ishara zinaashiria anguko kubwa la wapinga UTU!!

Narudia...!

Mafisadi , wanyoyaji kwa jina lolote mjue fika kamwe hamtaweza kuupindua Utaifa,,utanzania na UTU uliopiganiwa kwa maumivu makuu na wazee waliotangulia. Mjue kuwa bora mjitokeze hadharani na kuinua mikono JUU kabla ya hicho ninachokijua hakijawapata..sio kutisha..!!!

Kamwe hamtaweza kuligeuza Tanzania kuwa Taifa la kinyama.

Kuweza kufanya hivyo..futeni historia ya Mwenge wa uhuru kupandishwa kilimanjaro na mtiririko wake wote wa matukio!!

Ni malizie!!

Watanzania wengi mlio na UTU!! Huundio wakati wa kusonga mbele..ushahidi wa ushindi ni huu!!

Fisadi..monyajanji ..nk..Ni wapumbavu tu..kwanza hawa kujiumba watu..kwa hiyo hawawezi KUUKANA UTU KWA UFISADI NA UCHAFU WANAOFANYIA TAIFA HILI TAKATIFU!!!

Yabidi kujiunga BILA woga wowote na kufanya kinachotakiwa kufanyika!!

Cha kufanya????

Wote mnakijua !!

DO THE IMPOSIBLE!!! DO WHAT MUST BE DONE!!!
 
UNYONYAJI: Ni kitendo kiendekezwacho na watu ambao kwa hulka zao si wasafi, nikiwa na maana si waaminifu, wavivu wa kufanya kazi na kufikiri.

Mnyonyaji anapopata mwanya wa kuwa karibu au kuaminiwa kuwa karibu na mali basi mnyonyaji anafuja kama hana akili mzuri.

Mfano mmoja tu natoa hapa: BM na DY wamejichukulia mgodi wa Kiwira, huu ni unyonyaji rasmi
 
Nafikiri kuna neno linalomisi hapa- "Vibaraka"- Haya makampuni ya madini, mabenki ya nje, makampuni ya nishati yanayoinyonya TANESCO, nk. hao ndio wanyonyaji. Hawa kina Mkapa, Yona, Chenge, Lowasa nk. ni vibaraka wao. Wanasaidia kuishikilia na kuiweka mirija ya wanyonyaji vizuri. Tunapopiga kelele ya kuwataka wanyonyaji watoke, vibaraka wao wanatudhibiti kwa niaba yao. Bado hata hivyo kuna wanyonyaji wachache weusi kama akina Nimrod Mkono, Karamagi na Rostam
 
tufanye nini ili tuwanyang'anye mirija hiyo? Ni vipi wanaweza kukatiwa mirija hiyo ili na wao tuanze kuwaambia..

mafisadi walia
Mafisadi walia
Mafisadi walia kukatiwa mirija..

walipotangaziwa
Walipotangaziwa
Walipotangaziwa.... ????
 
Yawezekana tumepigwa ganzi... unajua mbu akitaka kukunyonya anaweka tu enzyme fulani hivi na kukupiga ganzi kwanza basi anauteremsha mrija wake kama drill mashine halafu anafyonza weeeee.. pale anapochomoa ndio wewe unasikia maumivu... sasa hivi nadhani tumepigwa ganzi; ndio maana hatujakasirika..!

Mzee sasa hivi naona wameongeza mirija ndo maana watu wanaisi maisha magumu sana wakati wao wanasema walichuku vijisenti kidogo. Sasa tunaanza kuisi maumivu kiasi kuwa tutaamka kwenye usingizi.
 
Yawezekana tumepigwa ganzi... unajua mbu akitaka kukunyonya anaweka tu enzyme fulani hivi na kukupiga ganzi kwanza basi anauteremsha mrija wake kama drill mashine halafu anafyonza weeeee.. pale anapochomoa ndio wewe unasikia maumivu... sasa hivi nadhani tumepigwa ganzi; ndio maana hatujakasirika..!

It is important to note that one cannot fight on an empty stomach;or in other words a starving man is not much of a fighter,even when it comes to his survival.And again remember the easyest way to cope with hunger is to go to sleep (not to be mistaken with "kupigkwa ganzi".Eventually never to wakeup again.I hope and pray we can turn around and fight before we get to that stage.
In zenj during Karume Snr days ,school children were taught to sing wakati wa mchakamchaka, "Bepari CHINJA, Mnyoyaji CHINJA" Had it been put into practice what would life be like today in Bongo,I wonder.
 
Azimio Karibu tena ndugu.

Mchungaji, Nashukuru nipo! Ni shughuli za hapa na pale! Ila kichwa kinaniuma... Huu ushindi kweli uko karibu? Hawa mafisadi!!! Bado sipati jibu la moja kwa moja..ila kukaa kimya ni vibaya zaidi. kila siku anaibuka mpya na kituko kipya... kama sio "vijisenti" ni "ajali ya kisiasa.." kama sio hivyo ni "Nimeonewa".... If we had a strong charactered President....!! Pale Butiama..Angelitangaza!!? Na angeacha mzaha. Nafikiri jibu ni kwa wananchi kusema basi!! Na hilo halipo mbali!!! Kuwakataa!!!
 
Hivi hawa mafisadi wetu wanataka tuamini kwamba mtu akishakuwa na madaraka serikalini basi anakuwa mtakatifu na tuhuma zozote dhidi yake ni uzushi na wivu. Wengine hudiriki hata kusema Mungu ndio anajua!!!!!!!!

Watanzania lazima tuelewe kwamba tumejitengenezea kazimbabwe ketu kwa maana kwamba kuin'goa sisiemu hata kwa uchaguzi ni ngumu mno!!!!!!!
 
Back
Top Bottom