Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,831
Walimu hawana utu wala huruma, sasa wameamua liwalo na liwe. Piga, uwa, garagaza.
Hawajali tena namna ya upigaji, mtoto wa kike apigwe mkononi, wa kiume matakoni. Walimu wanapiga ngumi wanafunzi utadhani wako kwenye tamasha la Karate.
Wanawazaba watoto vibao vya uso, ukatili mbalimbali wanaufanyia.
Sasa tunasikia habari za ulawiti, walimu wakiwafanyia watoto wa kiume, huku wale wa kike wakimiminiwa mimbegu iletayo mimba.
Hii kada ni kada adhimu kwa future ya taifa letu na vizazi vijavyo. Iheshimiwe na watu wote, walimu ndio wanatakìwa wawe wa kwanza kuiheshimu.
Na pia wakumbuke kwamba hata Yesu, alikuwa ni nabii. Hivyo elimu ndiye mkombozi pekee wa fikra za taifa letu na kizazi kijacho
DOKEZO - Kagera: Mwanafunzi wa Form 2 abakwa na mwalimu aliyekuwa anamfundisha tuition
Jamii Forums pazeni sauti kuna mtoto wa kidato cha pili amebakwa na Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera wakati akifundishwa tution. Mtoto ni Mwanafunzi wa kidato cha pili Shule ya Sekondari Kagondo. Kwa sasa mtuhumiwa yuko nje kwa dhamana anatamba. Atuhumiwa aliyefanya kitendo hicho anafahamika...
www.jamiiforums.com