Unyama huu ulaaniwe kwa nguvu zote!

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Mjamzito ajifungulia ofisi ya Kata

2007-12-13 10:57:04
Na Anceth Nyahore, PST Shinyanga


Mjamzito aliyekuwa amewekwa chini ya ulinzi katika ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Ilola, Wilaya ya Shinyanga kwa kutolipa mchango wa sekondari ya kata, amelazimika kujifungulia ndani ya ofisi hiyo.

Mjamzito huyo, Bi. Pili Kaya, mkazi wa kijiji cha Kasingili, wilayani humo, alikutwa na kadhia hiyo wakati akishikiliwa katika ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Ilola, Bi. Noela Magesa kwa kushindwa kulipa mchango wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Ilola.

Baada ya kukamatwa, alifikishwa katika ofisi ya Mtendaji wa Kata ambako aliwekwa chini ya ulinzi.

Hata hivyo, akiwa chini ya ulinzi katika ofisi hiyo, Bi. Pili aliwaeleza viongozi wa Kata kuwa, anajisikia vibaya kutokana na hali yake ya ujauzito na kuomba aruhusiwe ili aende hospitali, lakini `walimtolea nje`.

Kufuatia hali hiyo, ndipo mwanamke huyo alipojikuta akijifungua katika ofisi hiyo tena mbele ya wanaume waliokuwepo.

Inasemekana kuwa, Bi. Pili alipatiwa huduma ya kwanza na baadaye kupelekwa hospitalini kwa huduma zaidi.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Kanali Edmund Mjengwa, alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Kanali Mjengwa alisema ofisi yake hivi sasa kwa kushirikiana na ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, inafanya uchunguzi wa tukio hilo na kwamba taarifa zaidi zitatolewa baadaye.

SOURCE: Nipashe
 
Habari hizi za unyanyaji tulianza kuzisikia kutoka wilaya ya Muleba, tukaja wilaya ya Songea na sasa ni Shinyanga. Habari ya Shinyanga imeweka rekodi na kuonyesha wazi kwamba hii michango si bure lazima kuna shinikizo kutoka juu. Nadhani ni wakati muafaka serikali ya JK ikae chini na kutafakari hali halisi. Bunge la June, EL alitamba sana Bungeni kwamba serikali ya JK imepania kuboresha elimu, as if huo uboreshaji wanaufanya wao, na kumbe ni kwa kuwakamua walalahoi mpaka tone la mwisho la damu kwa kile kinachoitwa michango.

Kweli kabisa mjamzito wa kijijini, hujui hata kama ana hiyo hela, huduma za afya ni mbaya kuliko na inawezekana akiba aliyo nayo ni ya kwenda kuwahonga manesi au kununulia gloves na vifaa vya kujifungulia ili aweze kuhudumiwa na manesi. Leo hii analazimishwa kutoa mchango kwa nguvu zote bila kujali hali yake. Hivi kweli tutafika? JK bado ana safari ndefu na huo umaarufu wake lazima utashuka tu, labda akane kwamba hakuwatuma hao wakuu wa wilaya kukusanya michango, na kama hakuwatuma yeye ni nani kawatuma watumie mabavu na kudhalilisha watu? Kuzalia kwenye ofisi ya mtendaji wa kata ni kumdhalilisha huyo mama na ni aibu kubwa sana!
 
Vitendo vya ukatili vinavyofanywa na viongozi wa vijiji au kata ni msalaba wao na havina baraka kutoka serikalini.tabia hii ni hulka ya mtu wwala hitokani na shinikizo lolote.Hakuna binadamu mwenye akili zake timamu anaweza kufanya kama alivyofanya jamaa huyu wa Shinyanga.Si ustaarabu hata kidogo kuwarushia madongo viongozi wa kitaifa kwa vitendo vya kibinafsi vinavyofanywa na watu wengine.
 
WanaJF, Hili jambo si la kwanza na ifike muda tulijadili kwa mapana yake ipatikane solution. Mimi mwenyewe kwa macho yangu nimeshuhudia ujinga huu huu dodoma, tena kijiji cha chamwino iliko ikulu. Nilikuwa katika shughuli za utafiti na ikawa imetokea tunafanya group discussion hapo ofisi ya mtendaji, palikuwepo na mama mjamzito tena ni kabinti tu inaonekana kaliolewa na umri mdogo, sasa kumbe hawajalipa huo mchango wa secondary, mumewe akatoroka ili asikamatwe ndo wakamshika bibie na kumlaza kwenye chumba cha ofisi, can you imagine mmbu zote zilizomshambulia usiku kucha, eti kisa hajalipa elfu tano. I was so angry na ikabidi niwaambie wale viongozi kuwa that is purely nonsense na nikamlipia huyo mam,a akatoka mida ya saa nane. hii ndo tanzania, yani inatia uchungu we acha tu.
 
Vitendo vya ukatili vinavyofanywa na viongozi wa vijiji au kata ni msalaba wao na havina baraka kutoka serikalini.tabia hii ni hulka ya mtu wwala hitokani na shinikizo lolote.Hakuna binadamu mwenye akili zake timamu anaweza kufanya kama alivyofanya jamaa huyu wa Shinyanga.Si ustaarabu hata kidogo kuwarushia madongo viongozi wa kitaifa kwa vitendo vya kibinafsi vinavyofanywa na watu wengine.

Kauli yako ingekuwa na ukweli ndani yake iwapo tungeona hao viongozi wakuu wakiwawajibisha hao viongozi wa chini ili kuthibitisha kuwa hawakuwatuma.
 
Vitendo vya ukatili vinavyofanywa na viongozi wa vijiji au kata ni msalaba wao na havina baraka kutoka serikalini.tabia hii ni hulka ya mtu wwala hitokani na shinikizo lolote.Hakuna binadamu mwenye akili zake timamu anaweza kufanya kama alivyofanya jamaa huyu wa Shinyanga.Si ustaarabu hata kidogo kuwarushia madongo viongozi wa kitaifa kwa vitendo vya kibinafsi vinavyofanywa na watu wengine.

Hivi unaelewa maana ya kuwa kiongozi?

Kiongozi unapaswa uwajibike kwa yale yote yanaoyo tendeka chini yako ndani ya himaya yako!!!

Ndo maana tuna lalama kwamba ni unafiki mkubwa kusema JK ni safi ila mawaziri wake ndo wabaya..

Ndo maana hata wewe baba mwenye nyumba, unawajibika juu ya wana familia wako.. katika jamii!!

Ni jambo lisilo ingia akilini kwamba hawa viongozi wa vijiji na mgambo tunao sikia wakinyanyasa wananchi kwa ajili ya michango hii kwamba wana jiamria tu??, hata hivo wameweka wazi kwamba wameagizwa toka juu!

Na kama uongozi wa juu hauja waagiza mbona hatusikii/kuona ukiingilia unyanyasaji huu??

Huku ni kutumia dhamana zao vibaya, hatujawapa madaraka ili watunyanyase nayo.., wanapaswa kufikiria zaidi na kuishia kujitetea/kutetewa bila msingi wowote kwamba wao hawauhusiki ni watendaji wa chini! Ama basi wakiri wazi kwamba wameshindwa kuongoza na kuachia uongozi mara moja!
 
I am seeing a break down in supervision system. These watendaji are very powerful in the villages. These people are left to interpret the law as they see it fit.
The CD should have been the first person off the block to condemn this act and also give them guidance on how they should be conducting their work.
 
Mambo ya jinsi hii yako mengi sana huko vijijini, ni bahati tu kwamba hili limeripotiwa. Tena hali huwa ni mbaya sana wakati wa ziara ya viongozi na hususan Waziri Mkuu, maana watendaji hutumia nguvu za ziada kuwakamua wanakijiji ili watimize lengo na kuandaa taarifa nzuri itakayomvutia Kiongozi. Siku moja nimeshuhudia mama mmoja kwenye TV akisema "yaani ni afadhali hawa viongozi wasiwe wanakuja huku, maana ukisikia tu kuna ziara ya kiongozi fulani ujue hapo ni mtafutano"
Hakuna tofauti na wakati ule wa kodi ya kichwa. Anyway, nasubiri kusikia mtu kawajibika/shwa
 
Nadhani ningekuwa bongo ningeorganise

maanadamano watu waaandamane uchi kulaani kitendo hicho ikiwa ni pamoja na kushinikiza Diwani, mkurugenzi, mwenyekiti wa halmashauri na DC wote wajiuzulu maana hata enzi za ukoloni haya hayakuwa yana fanyika
 
...I was so angry na ikabidi niwaambie wale viongozi kuwa that is purely nonsense na " nikamlipia huyo mama" akatoka mida ya saa nane. hii ndo tanzania, yani inatia uchungu we acha tu.

Ahsante Judy kwa ujasiri wako. Ulifanya kitendo kizuri sana, hususan ulipokemea na pia kumlipia ili binti wa watu aende kwake, na huwezi kujua labda isingekuwa wewe naye angeishia kujifungulia kwenye ofisi hiyo.

Kitu kingine ni kuwa huyo kanali na wenzake wanatakiwa wawajibike au wawajibishwe, kama hawatawajibika wenyewe, huu ndiyo ujinga ambao baada ya miaka 46 mtu unabaki kujiuliza, je kuna faida kweli ya uhuru ambao tunaambiwa tunao?
 
Nataka kuwashukuru waandishi wa habari kwa kuripoti uozo huu katika jamii yetu. Nashawishika kuamini kwamba hii ni concerted effort ya kuripoti habari hizi, maana kama hakuna a deliberate effort ku focus kwenye hizi habari za unyanyasaji unaokimbilia style ya Gestapo, na kama hizi habari ni random reporting, basi tatizo ni kubwa sana na hizi cases tunazosikia ni chache tu zianzopata bahati kuwa na ukaribu kwa waandishi.

Ni muda kwa viongozi wa kitaifa kutoa tamko litakaloainisha unyanyasaji huu kama jambo la aibu na lisilovumilika katika jamii yetu.

Wako wapi wapinzani sauti ya mnyonge? This is not even a violation of civil rights, this seems to stem from a systematic violation of Tanzanians human rights.Kwanza hamuwapi huduma za jamii, on top of that mnawalipisha mikodi na michango lukuki.

Halafu wananchi kama kule Songea wakiwapiga mgambo utawalaumu kweli?
 
Kauli yako ingekuwa na ukweli ndani yake iwapo tungeona hao viongozi wakuu wakiwawajibisha hao viongozi wa chini ili kuthibitisha kuwa hawakuwatuma.
hata kama umetumwa na rais ,kama una chembe ya ubinadamu ndani ya damu yako huwezi kufanya kitendo cha ukatili kama hiki.hivi wewe leo aje kiongozi akutume ufanye ukatili huu ,je utafanya kwa sababu alokwambia ni kiongozi?
 
Mjamzito ajifungulia ofisi ya Kata

2007-12-13 10:57:04
Na Anceth Nyahore, PST Shinyanga


Mjamzito aliyekuwa amewekwa chini ya ulinzi katika ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Ilola, Wilaya ya Shinyanga kwa kutolipa mchango wa sekondari ya kata, amelazimika kujifungulia ndani ya ofisi hiyo.

Mjamzito huyo, Bi. Pili Kaya, mkazi wa kijiji cha Kasingili, wilayani humo, alikutwa na kadhia hiyo wakati akishikiliwa katika ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Ilola, Bi. Noela Magesa kwa kushindwa kulipa mchango wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Ilola.

Baada ya kukamatwa, alifikishwa katika ofisi ya Mtendaji wa Kata ambako aliwekwa chini ya ulinzi.

Hata hivyo, akiwa chini ya ulinzi katika ofisi hiyo, Bi. Pili aliwaeleza viongozi wa Kata kuwa, anajisikia vibaya kutokana na hali yake ya ujauzito na kuomba aruhusiwe ili aende hospitali, lakini `walimtolea nje`.

Kufuatia hali hiyo, ndipo mwanamke huyo alipojikuta akijifungua katika ofisi hiyo tena mbele ya wanaume waliokuwepo.

Inasemekana kuwa, Bi. Pili alipatiwa huduma ya kwanza na baadaye kupelekwa hospitalini kwa huduma zaidi.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Kanali Edmund Mjengwa, alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Kanali Mjengwa alisema ofisi yake hivi sasa kwa kushirikiana na ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, inafanya uchunguzi wa tukio hilo na kwamba taarifa zaidi zitatolewa baadaye.

SOURCE: Nipashe

inaskitisha sana ,lakini iko siku!!!
 
Ajeruhiwa kwa kutochangia ujenzi wa shule




na Joas Kaijage, Bukoba



USHAHIDI dhidi ya matumizi ya nguvu za ziada katika ukusanyaji wa michango iliyoelezwa ya hiari kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa vya shule za sekondari, umeanza kuonekana.
Katika moja ya matukio yanayodhihirisha ushahidi huo, mkazi wa Kijiji cha Bihanga mkoani Kagera, amelazwa hospitali baada ya kuumizwa vibaya kwa kupigwa wakati wa zoezi la kukusanya michango ya wananchi ya ujenzi wa shule za sekondari za kata wilayani Muleba.

Joel Kanuma (27) alilazwa katika Kituo cha Afya cha Kaigara wilayani Muleba Desemba 7 mwaka huu kutokana na kupigwa na viongozi wa Kata ya Burungura, wakiwamo askari wa mgambo na ofisa mtendaji wa kijiji.

Mkazi huyo alikamatwa na viongozi hao Desemba 4 mwaka huu akiwa nyumbani kwake, kabla ya kufikishwa kwenye ofisi za Kata ya Burungura ambako alipigwa hadi kuzimia, kutokana na kushindwa kulipa mchango wa sh 10,000 aliokuwa anadaiwa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambaye alifika hospitalini hapo kumtembelea juzi, Kanuma alisema baada ya viongozi hao kumpiga hadi kupoteza fahamu, walimtelekeza jirani na ofisi hiyo hadi siku iliyofuata alipochukuliwa na ndugu zake na kurudishwa nyumbani.

Akizungumza kwa maumivu, Kanuma alisema kuwa alikuwa peke yake wakati viongozi hao wanafika nyumbani kwake kumkamata kwa kushindwa kuchangia ujenzi wa sekondari na hivyo jamaa zake hawakutambua mara moja aliokelekea.

Kulingana na maelezo yake, Kanuma alibebwa na jamaa zake hadi nyumbani kwake asubuhi iliyofuata na kuamua kutibiwa kwa miti shamba, si kwa sababu ya kutokuwa na fedha ya kulipia matibabu bali pia kutokana na kuogopa kuripoti polisi ili kupatiwa fomu maalumu ya matibabu kwa hofu ya kukutana na viongozi wanaosimamia msako wa michango.

Hata hivyo, baada ya afya yake kuendelea kuwa mbaya, jamaa zake waliamua kumpeleka polisi ambapo alipatiwa fomu ya matibabu iliyosainiwa na WP 3470 Koplo Tabu, na kumwezesha kulazwa katika Kituo cha Afya cha Kaigara.

Akisimulia kipigo alichokipata, alisema kuwa mmoja wa viongozi hao (jina tunalihuifadhi) alikuwa akimpiga kwa kipande cha chuma cha mwavuli, wakati askari wa mgambo walikuwa wakitumia vitu mbalimbali ikiwamo kumpiga mateke.

Mganga Mfawidhi wa kituo hicho cha afya, Leontine Rwamulaza, alisema kuwa mgonjwa huyo aliumizwa sehemu mbalimbali za mwili, lakini alikiri kuwa kutokana na kutokuwepo kwa X-ray haikuwa rahisi kuelezea kiwango cha madhara aliyoyapata ndani ya kifua.

Kuna taarifa kuwa jamaa za mgonjwa walikuwa wameomba kupewa rufaa hadi Hospitali Teule ya Wilaya ya Rubya, lakini hawakuwa na fedha za kulipia usafiri wa gari la kumsafirisha hapi hospitalini hapo ambapo angepata huduma ya X-ray.

Muuguzi mmoja wa wodi alikolazwa mgonjwa huyo, alisema kuwa kutokana na gharama kubwa za uendeshaji, gari pekee la wagonjwa walilonalo hutolewa pale tu ambapo madaktari wameridhika kuwa mgonjwa husika ana hali mbaya na si kwa maombi ya wagonjwa.

Kwa mujibu wa Daktari Rwamulaza, alipofikishwa hospitalini hapo, Kanuma alipatiwa drip za glukosi kumwongezea nguvu, vidonge vya antibaotiksi na vile vya kupunguza maumivu na kwamba sasa hali yake ilikuwa na nafuu.

Hata hivyo, hadi jana hakuna kiongozi yeyote wa serikali aliyekuwa amefika hospitalini hapo wala kutoa msaada wa aina yoyote.

Madai ya kupigwa kwa Kanuma hadi kulazwa hospitalini yamekuja siku chache baada ya Mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi, kumlalamikia mkuu huyo wa wilaya, mwenyekiti wa halmashauri hiyo na mkurugenzi mtendaji kwa kusimamia vitendo vya kunyanyaswa kwa wananchi wakati wa kukusanya michango ya ujenzi wa sekondari.

SOURCE:Tanzania Daima
 
Kwa taarifa nilizonazo kuna circular iliyotolewa kutoka TAMISEMI kwenda mikoani, kwamba watendaji watumie 'any means necessary' kukusanya michango hiyo, ikiwamo kuwa-detain watu! Kama isingekuwa kweli basi hata Katibu Mkuu wa TAMISEMI angetoa tamko!

Kwa habari zaidi bofya hapa> http://mtanzaniahalisi.wordpress.com

Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom