Kiganyi
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 1,242
- 765
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa (kulia), akizungumza baada ya kufungua moja ya matawi mjini Newala ikiwa ni sehemu ya ziara ya viongozi wa chama hicho. Katikati ni Mwenyekiti, Freeman Mbowe akiwa amembeba mtoto Muaza Mohamed na kushoto ni Makamu Mwenyekiti, Zanzibar, Ali Issa Mohamed.
Akina mama wa kijiji cha Mbuyuni, katika jimbo la Lulindi mkoani Mtwara, wakiimba nyimbo za kumpongeza Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, mara baada ya mkutano wake wa hadhara katika kijiji hicho
Akina mama wa kijiji cha Mbuyuni katika jimbo la Lulindi mkoani Mtwara, wakiitikia kibwagizo cha Peoples Power kinachotumiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wakati wa mkutano wa Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), akihutubia mkutano wa hadhara wa chama hicho wa kampeni ya Vua Gamba Vaa Gwanda, uliofanyika mjini Tandahima mkoani Mtwara.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni ya Vua Gamba Vaa Gwanda, uliofanyika huko Chiungutwa, Lulindi mkoani Mtwara.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akipandisha bendera ya chama hicho, wakati alipofungua Tawi jipya katika Mtaa wa Mkombozi mjini Newala juzi. Kulia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa na kushoto ni Makamu Mwenyekiti, Zanzibar, Ali Issa Mohamed.
Kama imekuuma sana na Magamba yako 'GO & EAT A COKE'