Ununuzi wa pikipiki mpya waingia doa

stweka

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
422
144
Habari za wikiendi bana ndugu,hali ya uchumi kwa wakulima wa ufuta imekuwa ngumu mno mwaka huu,ufuta umepatikana lakini bei ni ya chini sana,kwa kawaida zao hili huuzwa kati ya sh 2000-2500,lakini mwaka huu hali ni ngumu sana kwa huku kusini maana huuzwa kwa sh 1500-1600,na kwa kawaida wakulima huuza zao hili na hukimbilia kununua sanlg na ndani ya kijiji ilikuwa huwezi kukosa pikipiki mpya angalau 3.

Kwa bahati mbaya mwaka huu nimetembelea kata ya chikonji iliyopo Lindi mafundi pikipiki wanalalama kukosa kazi maana kipindi hiki cha msimu hakuna watu wanaoleta kazi mpya, ni mimi mkulima wa ufuta toka kusini.
 
Habari za wikiendi bana ndugu,hali ya uchumi kwa wakulima wa ufuta imekuwa ngumu mno mwaka huu,ufuta umepatikana lakini bei ni ya chini sana,kwa kawaida zao hili huuzwa kati ya sh 2000-2500,lakini mwaka huu hali ni ngumu sana kwa huku kusini maana huuzwa kwa sh 1500-1600,na kwa kawaida wakulima huuza zao hili na hukimbilia kununua sanlg na ndani ya kijiji ilikuwa huwezi kukosa pikipiki mpya angalau 3,kwa bahati mbaya mwaka huu nimetembelea kata ya chikonji iliyopo Lindi mafundi pikipiki wanalalama kukosa kazi maana kipindi hiki cha msimu hakuna watu wanaoleta kazi mpya, ni mimi mkulima wa ufuta toka kusini.
Hapo lindi mjini mlimchagua mbunge wa ccm wacha muisome namba
 
Lindi mumeikumbatia sana serikali pendwa ya chama cha mapinduzi, jaribu kupeleka malalamiko yako kwa mwenyekiti wa ccm mkoa.
 
Unadhani ccm na mbunge wao ndo wenye dhamana ya kununua huo ufuta? unadhan bei ya ufuta hupangwa na mbunge au?
Anaweza kulisemea hilo akiwa bungeni na wizara husika ikalifanyia kazi.
Sasa mbunge bubu anajali tumbo lake unategemea wanakijiji watafaidi kile walichopanda?
 
Watu wengine akili zenu zipo kwenye ma....lio, sasa mbunge ndio kashusha bei au mbunge ndio kalima ufuta mwingi?
Acha upunguani wewe, mbunge anaweza kulisemea hili bungeni na kushirikiana na wananchi waliompeleka pale.
Tatizo mnajali vitambi vyenu.
 
Watu wengine akili zenu zipo kwenye ma....lio, sasa mbunge ndio kashusha bei au mbunge ndio kalima ufuta mwingi?
Wabunge wenu wameenda bungeni kusifia madera na khanga,badala ya kuongelea mambo ya msingi kama suala la bei ya ufuta au mbaazi,unategemea nini?
 
Kwa mazao kama korosho, kahawa,karafu na ufuta bei yake hutegemea soko la dunia Na sio ccm na mbunge wao wa lindi
Karaga bhao wenzenu wa kahawa wanajipigia noti kwa kwenda mbele kwa kuwa wabunge wa sehemu hizo ni wale wanaojali maslahi ya wananchi na taifa,mbeya,kilimanjaro, bukoba
 
Unadhani ccm na mbunge wao ndo wenye dhamana ya kununua huo ufuta? unadhan bei ya ufuta hupangwa na mbunge au?
Yaani mwakilishi wa wananchi unaenda bungeni kuomba eti tanzania ifungue kiwanda cha madera kisa wanawake wa tanzania ni wanene?
 
Back
Top Bottom