Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Ripoti ya mwaka ya CAG kuhusu ukaguzi wa Mashirika ya Umma kwa mwaka wa fedha 2014/2015 iliyotolewa tarehe 28 Machi, 2016 inaonyesha kwamba; kulikuwa na matatizo makubwa ya uendeshaji wa Shirika la Ndege Tanzania ambayo yalipeleka Shirika hilo kupata hasara kubwa hadi kufikia shilika hilo kuelekea kufa kama sio kufikisika na kisha kufa.
CAG aliainisha maeneo yaliyokuwa na matatizo katika Shirika hilo na kutoa mapendekezo ili kunusuru Shirika la Ndege lakini mapendekezo hayo hayakufanyiwa kazi na badala yake Serikali imewekeza mabilioni ya fedha za walipa kodi katika Shirika ambalo linajiendesha kwa hasara.
Licha ya ripoti ya CAG kuonyesha kwamba ATCL haina Mfumo thabiti na endelevu wa Usimamizi wa vihatarishi vya kibiashara, haina mkakati mahususi wa kufufua shirika, haina vyeti vya usafiri wa kimataifa wa anga; inafanya ukodishaji wa ndege usiokuwa na faida, na kwamba hali yake ya kifedha imeporomoka karibu na kufilisika; bado Serikali ilitumia fedha za walipa kodi na kununua Ndege kwa fedha taslimu (shilingi trilioni 1) kinyume na sheria ya manunuzi inayoelekeza kulipa kwa awamu (installment).
Wakati Serikali inawekeza mabilioni hayo ya fedha za walipa kodi kwenye Shirika la ATCL; taarifa ya mwaka ya shughuli za kamati ya kudumu ya Bunge ya UWEKEZAJI na mitaji ya UMMA (PIC) kwa kipindi cha Januari,2017 hadi Januari 2018; ilikuwa ikieleza kwamba matumizi ya Shirika la ndege la ( ATCL ) yamekuwa yakiongezeka kwa kiasi kikubwa hivyo kulifanya Shirika kujiendesha kwa hasara.
Katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo, kuanzia mwaka wa fedha 2014/15 hadi 2016/17 matumizi yaliongezeka kwa kiwango cha juu ikilinganishwa na mapato yaliyokusanywa nakupelekea shirika kupata hasara kwa miaka yote mitatu kama ifuatavyo;
Mwaka 2014/15 shilingi 94,355,952,000/=
Mwaka 2015/16 shilingi 109,271,250,000/=
na mwaka 2016/17 shilingi 113,770,184,000/=
Jumla KUU ni shilingi 317,329,042,000/=!
Hasara ya shilingi bilioni 317.329 ya fedha za walipa kodi ni kubwa na haikupaswa kufumbiwa macho hata kidogo na Bunge ukizingatia tahadhari iliyokuwa imetolewa na CAG na pia Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC).
Ilitegemewa kwamba Bunge lingepitisha azimio kukazia mapendekezo ya CAG na Kamati ya PIC ili kulinusuru shirika la ndege ambalo kimsingi ni sawa na kwamba lilikuwa limekufa.
Bunge halikufanya hivyo; na pale ambapo Serikali ilikiuka Sheria ya manunuzi (Procurement Act) kwa kununua ndege kwa fedha taslimu kabla ya kutekeleza mapendekezo ya CAG na Kamati ya PIC, Bunge pia lilikaa kimya.
Licha ya CAG kuendelea kuonyesha katika ripoti zake za miaka iliyofuata kuwa shirika linajiendesha kwa hasara; bado Serikali iliweka pamba masikioni na kuendelea kutoa mabilioni ya fedha kununua ndege na Bunge pia liliendelea kukaa kimya. Kutokana na hali hiyo, sina hakika kama kuna mchambuzi au mtafiti atakayetafsiri mwenendo huo kama ni ufanisi wa Bunge letu. Nadhani kinyume chake ni sahihi.
Huu ni Uchambuzi wa kawaida tu wa ripoti ya CAG, ambao unaonyesha matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi wa nchi hii, na ni lazima ifike hatua wananchi wachukue hatua za kuiwajibisha serikali ya CCM na Rais wake!
Julius Mwita
jullygabri2020@gmail.com
CAG aliainisha maeneo yaliyokuwa na matatizo katika Shirika hilo na kutoa mapendekezo ili kunusuru Shirika la Ndege lakini mapendekezo hayo hayakufanyiwa kazi na badala yake Serikali imewekeza mabilioni ya fedha za walipa kodi katika Shirika ambalo linajiendesha kwa hasara.
Licha ya ripoti ya CAG kuonyesha kwamba ATCL haina Mfumo thabiti na endelevu wa Usimamizi wa vihatarishi vya kibiashara, haina mkakati mahususi wa kufufua shirika, haina vyeti vya usafiri wa kimataifa wa anga; inafanya ukodishaji wa ndege usiokuwa na faida, na kwamba hali yake ya kifedha imeporomoka karibu na kufilisika; bado Serikali ilitumia fedha za walipa kodi na kununua Ndege kwa fedha taslimu (shilingi trilioni 1) kinyume na sheria ya manunuzi inayoelekeza kulipa kwa awamu (installment).
Wakati Serikali inawekeza mabilioni hayo ya fedha za walipa kodi kwenye Shirika la ATCL; taarifa ya mwaka ya shughuli za kamati ya kudumu ya Bunge ya UWEKEZAJI na mitaji ya UMMA (PIC) kwa kipindi cha Januari,2017 hadi Januari 2018; ilikuwa ikieleza kwamba matumizi ya Shirika la ndege la ( ATCL ) yamekuwa yakiongezeka kwa kiasi kikubwa hivyo kulifanya Shirika kujiendesha kwa hasara.
Katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo, kuanzia mwaka wa fedha 2014/15 hadi 2016/17 matumizi yaliongezeka kwa kiwango cha juu ikilinganishwa na mapato yaliyokusanywa nakupelekea shirika kupata hasara kwa miaka yote mitatu kama ifuatavyo;
Mwaka 2014/15 shilingi 94,355,952,000/=
Mwaka 2015/16 shilingi 109,271,250,000/=
na mwaka 2016/17 shilingi 113,770,184,000/=
Jumla KUU ni shilingi 317,329,042,000/=!
Hasara ya shilingi bilioni 317.329 ya fedha za walipa kodi ni kubwa na haikupaswa kufumbiwa macho hata kidogo na Bunge ukizingatia tahadhari iliyokuwa imetolewa na CAG na pia Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC).
Ilitegemewa kwamba Bunge lingepitisha azimio kukazia mapendekezo ya CAG na Kamati ya PIC ili kulinusuru shirika la ndege ambalo kimsingi ni sawa na kwamba lilikuwa limekufa.
Bunge halikufanya hivyo; na pale ambapo Serikali ilikiuka Sheria ya manunuzi (Procurement Act) kwa kununua ndege kwa fedha taslimu kabla ya kutekeleza mapendekezo ya CAG na Kamati ya PIC, Bunge pia lilikaa kimya.
Licha ya CAG kuendelea kuonyesha katika ripoti zake za miaka iliyofuata kuwa shirika linajiendesha kwa hasara; bado Serikali iliweka pamba masikioni na kuendelea kutoa mabilioni ya fedha kununua ndege na Bunge pia liliendelea kukaa kimya. Kutokana na hali hiyo, sina hakika kama kuna mchambuzi au mtafiti atakayetafsiri mwenendo huo kama ni ufanisi wa Bunge letu. Nadhani kinyume chake ni sahihi.
Huu ni Uchambuzi wa kawaida tu wa ripoti ya CAG, ambao unaonyesha matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi wa nchi hii, na ni lazima ifike hatua wananchi wachukue hatua za kuiwajibisha serikali ya CCM na Rais wake!
Julius Mwita
jullygabri2020@gmail.com