Unigeria na Ukenya wasambaa kila kona Tanzania

Kidzogolae

Senior Member
Apr 20, 2008
133
2
Wengi tunaelewa kuwa, baadhi, nasema baadhi ya wandugu zetu wa Nigeria, kipindi cha nyuma wamekuwa wakisifika sana kwa ulaghai, hasa wa kuwaibia hela watu mbumbumbu au wasio na elimu ya kutosha. wamejaa humu kwenye net. wengi hapa bongo wameliwa hela zao, baada ya kudanganywa kuwa wameshinda loto, na wengine kuambia wamepata scholarship hivyo watume hela na vitu vingi. Inavyoonekana, hivi vitu huwa vinafanywa na watu walioenda shule, kwasababu wanao uwezo mkubwa sana wa kumshawishi mtu hadi aingie laini. Zamani walikuwa wanigeria, lakini kwa muda karibia miaka mitano sana, Wakenya wametawala kwa wizi wa aina hiyo hapa East Africa....., naomba mnielewe, mimi sina chuki binafsi na wakenya, ila naongea kitu cha kweli.

Wametokea mara nyingi sana kuwadanganya watz, na wamewala hela nyingi sana. siku hizi, wanawadanganyishia watu kuwa wameshinda shindano la bahati nasibu, either ya voda com, tigo, au celtel n.k. mimi vilevile nimepata msg mara nyingi sana za aina hii. Mara nyingi watu wa vodacome, celtel au hao wengine, wamekuwa wakiwaelimisha watz kuwa, ukiona mtu anasema umeshinda na anakupa private number, sio customer service number, ujue ni mwizi. watu hawa wamekuwa wakiwaambia wananchi kuwa wameshina pesa nyingi, na ili kuzipata, inabidi wa confirm kama ni wao(wananchi)kwa kuwatumia either dola kumi za vocha n.k, na watu wengi sana wameliwa.

Leo hii, wamemwandikia msg msichana wangu wa kazi, wanasema ameshinda million kumi, na kwa maelezo zaidi, apige number 0754 625389. msichana wangu alikuja akirukaruka, akisema ameamka tajiri....hahaha, nilichukia baada ya kushtukia, nikaamua kumpigia huyo jamaa ile number, akapokea....NILISIKIA JAMAA AKIONGEA KISWAHILI CHA KIKENYA KABISA JAMANI. kama hamniamini, jaribuni kumpigia jaa hiyo simu hapo juu, ndo tapeli mwenyewe....anaongea kiswahili cha kikenya. alipoona anaongea na sauti nzito ya mtu mwelewa na anaeonekana kama ni msomi wa nguvu(yaani mimi), akakata simu haraka, nilipiga hadi nikashindwa walau nimtukane, akazima kabisa ile simu.

hawa watu tutawakamataje? naombeni msaada. na wako hapahapa tz. hawa ndo watu wanaosema wanataka kujiunga na sisi ati. watu wengi nimesikia wameliwa vocha zao kwa namna hii. hebu mpigieni simu muone...ninyi wenyewe mtaona jamaa anaongea kikenya kabisa.
 
Ingekuwa vizuri kwenye issues kama hizi za kitapeli, makampuni ya simu yatangaze hadharani mara inapobainika kwamba mmoja wa wateja wao anafanya utapeli kupitia namba aliyopewa, kwamba namba fulani iliyotolewa kwa fulani bin fulani ni namba ambayo inatumiwa kwa utapeli. Si ajabu hata jina aliloandikisha huko ni la uwongo.
 
Ata nami ilinitokea nikawaambia Vodacom wakanambia kuwa ni watu ambao wako kule boarder ie labda wakenya wanafanya huo utumbo!
 
Simu kadi zinauzwa kama karanga,utawakamata vipi? cha msingi tupashane habari kuwa kuna wevi kwa njia ya simu.Pili kampuni za simu zikijulishwa juu ya namba ya tapeli zichukue hatua za haraka kuzifunga hizo namba.
 
Kuna umuhimu sasa wa kuanza ku-control mauzo ya sim cards; they have contributed significantly kuongeza uhalifu na kuondoa amani majumbani. Tukifanya usajili makini kwa waombaji na kuchukua copy za vitambulisho tunaweza kupunguza shida nyingi
 
Ingekuwa vizuri kwenye issues kama hizi za kitapeli, makampuni ya simu yatangaze hadharani mara inapobainika kwamba mmoja wa wateja wao anafanya utapeli kupitia namba aliyopewa, kwamba namba fulani iliyotolewa kwa fulani bin fulani ni namba ambayo inatumiwa kwa utapeli. Si ajabu hata jina aliloandikisha huko ni la uwongo.
Mkubwa Bongo hakuna address najua unalijua hilo.....kwahiyo line za simu ukinunua haihitajiki kupeleka proof yoyote kama wanavyofanya ughaibuni...line zinauzwa Shillingi 100 zimetandazwa chini
 
Kwakuwa namba yake ya simu ipo wanausalama serious hakwepi kukamatwa kwani mitambo ya simu inazorekodi za simu... hapa ni swala la wanausalama wakiamua kukomesha utapeli huu au kuacha uendelee
 
Kwakuwa namba yake ya simu ipo wanausalama serious hakwepi kukamatwa kwani mitambo ya simu inazorekodi za simu... hapa ni swala la wanausalama wakiamua kukomesha utapeli huu au kuacha uendelee

Hawawezi kwani watu hawa wana namba kibao na wakishatapeli mtu wanabadili line. Mimi nadhani tatizo kubwa ni makampuni ya simu ambayo yameruhusu simu card kuuzwa kwa fedha kiduchu! Wao wenyewe wana wafanyakazi wezi maana siku moja nimeibiwa simu ilikuwa kama na shilingi 20000, nikaripoti zikiwa bado hazijatumika, waliponirudishia line kukawa na shilingi 12 tu!
 
Mkubwa Bongo hakuna address najua unalijua hilo.....kwahiyo line za simu ukinunua haihitajiki kupeleka proof yoyote kama wanavyofanya ughaibuni...line zinauzwa Shillingi 100 zimetandazwa chini

Celtel wanaregister walau jina, at least waweza kutrace ila sijui kama ni wauzaji wote wanaregister customer wao. Hii ni rahisi sana kufanya hata kama ni kijijini kwa sababu dealers na subdealers wanajulikana, basi waambiwe wawe wanarecord majina ya wateja wao.
 
hii habari nimeipenda na mm pia ilishanitokea niliambiwa niweke elfu 10 kisha nibonyeze namba za kuhamisha salio then miujiza itatokea nitapata mara mbili ya pesa kwakua nami ni mjanja nikastukia nakumwambia weka elfu20 ufanye hivyo then utapata elu20 hapohapo, niliiripori hii namba kwa mtandao husika na kuifunga na kurudisha pesa zote alizokua ametapale kwa siku ile namba ilikutwa na 39,000, muhimu hapa ni wateja kuwa waelewa na wasipende pesa za kiurahisi, hujacheza lotto toka uzaliwe utashinda vipi? kuna huduma kwa wateja basi tupige kuuliza kabla ya kukurupuka
 
Kitu cha ajabu ambacho hadi nilimwonea huruma yule mwizi, ni kwamba alijitahidi sana kuongea kiswahili cha Kitz, akawa anashindwa maskini wa mungu, akajikuta akiendelea tu kuongea kiswahili cha kikenya kilichojaa lafudhi ya kikikuyu kiasi kwamba hauwezi kupenda uendelee kukisikiliza, kinakera, kinakereketa yaani. Nilishawai sikia kweli kuwa, hawa watu wako mpakani. hasa kule Namanga, Arusha yote na wala sio mombasa. manake mombasa wanaongea kiswahili kama cha Tanga tu.

Well, nijuavyo mimi, kama makampuni ya simu yakishirikiana na wana usalama, wanaweza wakawakamata vizuri tu, kwa kuweka trick mbalimbali hata za bahati nasibu tu, na wakajileta wenyewe. pia, mtu anapoongea kwenye simu, ile mitambo huwa inaonyesha kule makao makuu anapiga yuko wapi, kama anaongea yuko arusha, inaonyesha hivyo kwasababu kila mahali kuna mitambo,ile wanayojenga ili kudaka mawasiliano, na inaweza kuonyesha jamaa yuko wapi. kama kweli tunataka kutoa example hata kwa mmoja tu, ni vyema wawe serious kwa hili. watz wengi ndo maana wanatutukanaga kuwa sisi wajinga(wakenya hututukana), ni kwasababu, sisi tumelelewa kuwa watu wema, madili kama haya kwetu ni mageni. twawezafanya mabaya mengine lakini siyo kama haya.

jana tu tumeshuhudia hawa wenzetu wa kikenya kula wilaya ya Ryola(kule Musoma)wemefanya dili na wanakijiji wasioelewa wakawadanganya wakaiba ng'ombe 300 za wanakijiji wa kitz. hata siku moja hujawai sikia mtz ameiba kenya, ila wakenya wameiba tz. hawa ndo watu tunaotaka kuwa pamoja kwenye jumuiya. tena walitumia silaha nzito unaambiwa. lini ulisikia watz au waganda wameiba kenya? kule mpakani uganda na kenya wanataka hadi kuleta ugomvi wa nchi kwasababu wakenya wanaiba ng'ombe za waganda....kule arusha na moshi ndo usiseme, ndo majambazi wa kwanza. kwanini tuishi bila raha kwenye nchi yetu kwasababu ya hawa wakenya?
 
Back
Top Bottom