Ungependa Serikali ifanye nini kuongeza chachu ya maendeleo ya watu na Taifa?

Mparee2

JF-Expert Member
Sep 2, 2012
2,580
4,262
Natamani kuona mawazo chanya ya watanzania wakipendekeza nini kingefanyika ili kikidhi matarajio ya ndoto zao na za Taifa.

Hapa tuongelee maendeleo/Uchumi, mambo ya kampeni za siasa tuweke pembeni.

Kama hoja inahusu mkoa/eneo fulani litaje.

Binafsi napendekeza;
1. Vijana wetu wanao maliza Kozi za juu za Kilimo; kwa wale wenye ari ya kilimo wajiunge makundi ya vijana 20 hivi wa fani tofauti tofauti wapewe mtaji wa Tractor na pembejeo waka anzishe kilimo bora kwa mazao waliyo yachagua; kiwango cha chini cha shamba lao liwe angalau heka 100. Naamini hapo wata ajiri watu wengi wa kawaida. Tofauti na hapo ni kuhakikisha mikoa yenye Mvua nyingi inapata trector moja walau kwa kila kijiji na lifuatiliwe..lilete faida

2. Ajira za wataalamu (Diploma/Degree); kwa kuwa watu wapo wengi nafikiri viwepo vigezo vya ubora vilivyo wazi ili ziwafikie na wale wasio onekana.

3. Biashara mpya kabisa zingepewa angalau mwaka mmoja wa kutolipa kodi kwani kipindi hicho ni cha kujitangaza na pengine kusoma soko. Nafikiri utakuwa muda muafaka wa kulea biashara

4. Baada ya kuwa na sekondari, sasa tujenge Vyuo vya Veta na kuimarishwa vile vilivyopo; kwa kuanzia kuwe na mkakati wa kuwa na chuo kimoja kizuri kwa kila wilaya Kinachotoa elimu tofauti tofauti ya kujitegemea

6. Kila wilaya iweze kujenga ajira kwa vijana wake mf: kila mwaka wilaya iweze kuwawezesha vijana wake idadi flani kuweza kujitegemea (biashara, Kilimo, Ufugaji nk) na wafuatiliwe na kusaidiwa kiutaalam (mf vijana 100)

7. Mazao yanayo tumika ndani ya Nchi yawekewe utaratibu kwa soko la ndani kuyanunua kulingana na mahitaji
1: Korosho kwa wakulima imekosa soko ila soko la ndani halina korosho na wafanya biashara hawaruhusiwi kununua
ii: Miwa; wakulima wa nje wa kilombero wanakosa soko kwa kiwanda kuzidiwa na uzalishaji; serikali iingilie kati iwasaidie wakulima /kiwanda kupata mtambo mwingine

8......
 
Sio kila mwenye kiwango kikubwa cha pesa Bank basi anahujumu uchumi au anatakatisha fedha au mwizi.

Hivyo waache huo muenendo.

Au kama jeff na mr musk wangekuwa Tanzania basi wangekuwa wanaokota chupa au wangekuwa jela na hivyo nchi kukosa maendeleo.

Dunia imeendelea hatupo miaka ya 60 tena.
 
Kiongozi;
kutaja hivyo hakusaidii; ungetaja iache ufisadi kwenye nini ili kama kweli kuna ufisadi ushuhulikiwe
Ufisadi unafanyika kwa kukwepa kupeleka bungeni matumizi ya miradi mikubwa ya serekali kama vile manunuzi ya ndege,Mayanga contractors ni agent alietukuka wa ufisadi,fedha za EU za COVID-19 ni ufisadi wa karne,Rais anahamishia mashirika kibao ikulu ambapo hapakaguliwi(TIC,ATCL,e.t.c),CAG haruhusiwi kuzungumzia matumizi mabaya ya fedha katika serekali,ufisadi wa TZS 1.5 trillion ambao uliibuliwa na CAG bado tunaukumbuka sana tu,e.t.c
 
Kilimo
Kilimo
Kilimo
Ili uweze kupunguza idadi ya watu wasio na kazi mijini njia pekee ni kukifanya kilimo kiwe njia kuu ya kupata pesa.
Tanzania tuna ardhi kubwa isiyotumika,zile fedha zinazotumika kununua magari ya kifahari kama maLand Cruiser V8 zingetumika kununua matrekta ya kukodi kwa bei rahisi walau kila Kijiji liwepo moja tu ili kuwawezesha wakulima wadogo wadogo wapate unafuu.
Land Cruiser moja V8 ni zaidi ya M200 wakati kwa pesa hio unapata trekta zaidi ya 4.
 
Serikali isimamie haki,mihimili mitatu ifanye kazi tofauti,sio kuipongeza serikali kila siku,
Katiba mpya inaitajika mapema,pia viongoz wetu wasiwe na madaraka katika chama pia haohao wanaiongoza nchi...nadhani tutawapita mpaka south africa kwenye swala la maendeleo vinginevyo na hapo tufanye tuishi alafu tufee basi...
 
Kilimo,ujasiriamali na kujitegemea vifundishwe kuanzia shule ya msingi
 
Back
Top Bottom