Ungekuwa wewe Tundu Lissu - Baada ya kumiminiwa risasi zote zile ungefanyaje?

Mchanya

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
974
1,525
Ndugu zangu,
Hebu kwa dakika moja turudi kwenye ubinadamu na tutafakari kwa kutumia akili zetu timamu. Hebu fikiria kwamba umepigwa risasi zaidi ya thelathini (30)!!!!, maana yake lengo lilikuwa kukutoa uhai. Bahati nzuri Mungu amekuwa upande wako umenusurika.

Licha ya kunusurika kifo bado ofisi yako (Bunge) haikupatii haki zako stahiki za matibabu wala kupewa pole kama taasisi. Hakuna kiongozi yeyote wa juu aidha aliyekupa pole au angalau kulaani waovu waliofanya jaribio lile.

ItSi Rais, Si Makamu, Si Waziri Mkuu, Si Waziri anayeshukulika na usalama wa raia - angalau aliyeguswa kwa tukio lile la kinyama. Cha kushangaza hadi leo HAKUNA juhudi wala uchunguzi wowote uliofanyika kuwakama wahusika UNGEKUWA WEWE NI TUNDU LISSU UNGEFANYAJE!!??

Ni tukio lisilo la kibinadamu kuwahi kutokea nchini Tanzania na limetia DOA kubwa nchi yetu.

Tuweke ushabiki wa kisiasa pembeni, tuweke jazba pembeni, tuwe wakweli wa nafsi zetu, kama binadamu wenye moyo wa kibinadamu. Tutumie akili zetu timamu tulizopewa na Mungu. Hisia, ushabiki na jazba zitatuhamisha na tukashindwa kufikiri vizuri.

Tujifunze kujadili CHANZO na sio MATOKEO. Achana na siasa na anza kutafakari kwamba Tundu Lissu ni binadamu wa kawaida, labda kaka yako, baba yako, mume, au binadamu mwingine wa kawaida, mwenye haki ya kuishi kama wengine.

Tundu Lissu anapigania roho yake binadamu aliyenusurika kifo, na yanayoendelea sasa ni matokeo ya kilichomkuta, hivyo ni vema tujadili chanzo kuliko matokeo ya anachofanya leo.

Kitu gani kina thamani zaidi kulinganisha uhai wa binadamu?
 
CCM supremacy ni chanzo cha haya yote

Hebu angalia reaction ya serikali kingwangala alipopata ajali linganisha na tukio lililomkuta lissu! reaction yao ilikuwaje?

Nchi hii kuwa ccm tu! kunakufanya uwe km malaika!

Rejea kesi ya ditopile kumpiga risasi dereva wa daladala na mwisho wa siku kuachiwa, laiti km asingekuwa mwana ccm na uhakika angefia jela.

Kuna mifano mingi inayoonesha privillege walionao wanaccm nchi hii.

Kuanzia kiuchumi , kisiasa, hta kiusalama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati mwingine unaweza toa shutuma kwa watesi wa mh Lissu ila ukijaribu kutafakari kwa umakini ni watu wenye moyo wakujari kuna wakati aliwai kulalamika kupokea jumbe za vitisho,huenda walikua wakimsisitiza kuepuka kikombe cha njugu 38 ila ndo hivyo kusikia kwa kenge mpaka damu itoke.
 
Ningeruhusu dereva ahojojiwe polisi

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa usalama upi.?
Hebu tuache siasa za visasi na kuua.
Mtu ni kitu cha thamani.
Ukidharau utu wa mtu usitegemee unaweza kuishi kwa amani mana visasi vitakuandama.

Hakuna mtuhumiwa aliyekamatwa halafu Dereva anaitwa kwa vyombo vya habari kuwa akatoe maelezo.
Haoajambazi yatamuachaje wakati yanafikiri kuwa yameonekana na huyo Dereva.

Watu wana Silaha za Vita na hazijakamatwa halafu Dereva aonekane akitokea kituo cha Polisi kutoa maelezo.

Kwa nini watuhumiwa wasikamatwe kwanza!
Kwa nini walinzi wa eneo hilo na majirani wasitoe maelezo tena kwa Siri.

Na kwa nini Dereva wa Lisu aliyenusurika kiuawa mana risasi 30 huenda zililenga kuwaua wote mana zilielekezwa kwenye gari kwa maana ya kuwamaliza walioko ndani.

Kwa nini wasiende Kimya kimya kumhoji huko kwa ajili ya kulinda usalama wa mtoa taarifa.
Kwa nini wanataka iwe ni ishu ya vyombo vya habari wakati wanafanya upelelezi?

Je,ingekuwa ni mtu mkubwa yeyote ndani ya mfumo wangeshindwa kukamata watuhumiwa mpaka wamhoji Muhanga wa tukio aliyoko Hospitalini.

Je, atakaporudi na kuhojiwa watapatikana hao majambazi waliojaribu kumuua Lisu na Dereva wake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni jambo baya lilimfika ndugu lissu nadhani MUNGU hakuwa anamuhitaji wakati huo, ila hadi leo huwa napata ukakasi wa dereva wake tu
 
Wakati mwingine unaweza toa shutuma kwa watesi wa mh Lissu ila ukijaribu kutafakari kwa umakini ni watu wenye moyo wakujari kuna wakati aliwai kulalamika kupokea jumbe za vitisho,huenda walikua wakimsisitiza kuepuka kikombe cha njugu 38 ila ndo hivyo kusikia kwa kenge mpaka damu itoke.
Hapo ndiyo mwisho wako wakufikiri?? Tuna safari ndefu mno ktk kuijenga Tz yetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haujui ni kwa nini amepigwa risasi na kwa nini waliompiga risasi waliamua kufanya hivyo, mtu hapigwi tu risasi bila ya sababu, labda ni false flag ya chadema ili waisingizie Serikali yetu iliyoback fire labda ni crime wamedhulumiana, labda ni drugs money, labda mambo ya mapenzi na mke wa mtu, labda ni power ndani ya chadema.

Anayejua ni yeye mwenye Tundu Lisu na dereva wake, kwanini na nani aliyempiga risasi, sisi wengine hatujui chochote.
 
Haujui ni kwa nini amepigwa risasi na kwa nini waliompiga risasi waliamua kufanya hivyo, mtu hapigwi tu risasi bila ya sababu, labda ni false flag ya chadema ili waisingizie Serikali yetu iliyoback fire labda ni crime wamedhulumiana, labda ni drugs money, labda mambo ya mapenzi na mke wa mtu, labda ni power ndani ya chadema.

Anayejua ni yeye mwenye Tundu Lisu na dereva wake, kwanini na nani aliyempiga risasi, sisi wengine hatujui chochote.
Zile risasi zilipiga upande wa kushoto ambako ndo alikuwa wakili msomi sana TL lakini tunashangaa kwamba eti mguu wa kulia ndo ulioathirika sana.... lakini jambo lingine la kushangaza ni kwamba ktk risasi zote zile yule dereva wetu hakuguswa hata na ganda la risasi huwa nacheka sana kwa hivi viroja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu zangu,
Hebu kwa dakika moja turudi kwenye ubinadamu na tutafakari kwa kutumia akili zetu timamu. Hebu fikiria kwamba umepigwa risasi zaidi ya thelathini (30)!!!!, maana yake lengo lilikuwa kukutoa uhai. Bahati nzuri Mungu amekuwa upande wako umenusurika.

Licha ya kunusurika kifo bado ofisi yako (Bunge) haikupatii haki zako stahiki za matibabu wala kupewa pole kama taasisi. Hakuna kiongozi yeyote wa juu aidha aliyekupa pole au angalau kulaani waovu waliofanya jaribio lile.

ItSi Rais, Si Makamu, Si Waziri Mkuu, Si Waziri anayeshukulika na usalama wa raia - angalau aliyeguswa kwa tukio lile la kinyama. Cha kushangaza hadi leo HAKUNA juhudi wala uchunguzi wowote uliofanyika kuwakama wahusika UNGEKUWA WEWE NI TUNDU LISSU UNGEFANYAJE!!??

Ni tukio lisilo la kibinadamu kuwahi kutokea nchini Tanzania na limetia DOA kubwa nchi yetu.

Tuweke ushabiki wa kisiasa pembeni, tuweke jazba pembeni, tuwe wakweli wa nafsi zetu, kama binadamu wenye moyo wa kibinadamu. Tutumie akili zetu timamu tulizopewa na Mungu. Hisia, ushabiki na jazba zitatuhamisha na tukashindwa kufikiri vizuri.

Tujifunze kujadili CHANZO na sio MATOKEO. Achana na siasa na anza kutafakari kwamba Tundu Lissu ni binadamu wa kawaida, labda kaka yako, baba yako, mume, au binadamu mwingine wa kawaida, mwenye haki ya kuishi kama wengine.

Tundu Lissu anapigania roho yake binadamu aliyenusurika kifo, na yanayoendelea sasa ni matokeo ya kilichomkuta, hivyo ni vema tujadili chanzo kuliko matokeo ya anachofanya leo.

Kitu gani kina thamani zaidi kulinganisha uhai wa binadamu?
Jambo la kwanza ningekimbilia hospitali ya Muhimbili ili nisikose stahiki zangu za ubunge kuhusu tiba!
 
Zile risasi zilipiga upande wa kushoto ambako ndo alikuwa wakili msomi sana TL lakini tunashangaa kwamba eti mguu wa kulia ndo ulioathirika sana.... lakini jambo lingine la kushangaza ni kwamba ktk risasi zote zile yule dereva wetu hakuguswa hata na ganda la risasi huwa nacheka sana kwa hivi viroja

Sent using Jamii Forums mobile app
Utakuwa ulitoroka shule au ulikimbia umande, ulichoandika tofauti na swali.
 
Haujui ni kwa nini amepigwa risasi na kwa nini waliompiga risasi waliamua kufanya hivyo, mtu hapigwi tu risasi bila ya sababu, labda ni false flag ya chadema ili waisingizie Serikali yetu iliyoback fire labda ni crime wamedhulumiana, labda ni drugs money, labda mambo ya mapenzi na mke wa mtu, labda ni power ndani ya chadema.

Anayejua ni yeye mwenye Tundu Lisu na dereva wake, kwanini na nani aliyempiga risasi, sisi wengine hatujui chochote.
JIBU SWALI.
Acha maelezo yasiyohusu swali.
 
Back
Top Bottom