Ungekuwa we ndio mjomba ungefanyaje?

Kobe

JF-Expert Member
Jun 17, 2009
1,794
808
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS Jakaya Mrisho Kikwete ameuomba Mfuko wa Maendeleo wa Saudi Arabia kuchangia katika ujenzi wa barabara ya Manyoni -Kigoma ambayo ni sehemu ya barabara muhimu ya Central Corridor.

Rais amesema kuwa barabara hiyo inayokadiriwa kuwa na kilomita 700 ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi ya Tanzania na kwa matumizi ya nchi za jirani na hasa Burundi.

“Najua mnatusaidia katika miradi mingi, ikiwamo ile mitatu ya maji na tunashukuru sana. Lakini mahitaji ya maendeleo ya binadamu hayana mwisho… ningefurahi sana kama Saudi Fund ingeshiriki katika kusaidia ujenzi wa barabara hii ya Central Corridor,” amesema Rais Kikwete.

Rais Kikwete ametoa ombi hilo leo, Jumatatu, Juni 22, 2009, alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mfuko wa Maendeleo wa Saudi Arabia ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Ufundi ya mfuko huo, Bwana Hassan M. Al-Attaas Ikulu, Dar es Salaam.

Rais Kikwete ameusisitiza ujumbe huo kuwa maeneo ya kipaumbele ya Serikali yake yataendelea kuwa katika maeneo ya elimu, miundombinu, maji na afya.

“Lakini ombi langu kwenu ni kushiriki katika miradi ya miundombinu. Najua kuna baadhi wameanza kutusaidia katika barabara hii ya Manyoni - Kigoma, lakini ningefurahi kama na nyie mngeshiriki katika kuchagua ujenzi huu… kwa kuunga mkono, kwa mfano, ujenzi wa barabara hiyo kati ya Tabora na Kaliua,” amesema Rais Kikwete.

Naye Bw. Attaas amemwambia Rais Kikwete kuwa ziara yake ni kufuatilia utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa wakati wa ziara ya Rais Kikwete katika Saudi Arabia mwezi Aprili, mwaka huu.

Amesema kuwa Saudi Fund utahakikisha kuwa miradi yote ambayo imekubaliwa kutekelezwa katika Tanzania kwa kugharimiwa na Mfuko huo itatakelezwa kama ilivyokubaliwa. “Tuko tayari hata kuanzia leo.”

Serikali ya Rais Kikwete imo katika juhudi kubwa kutafuta fedha za ujenzi wa barabara zote kuu na kubwa kama mojawapo ya njia rahisi zaidi za kufungua zaidi uchumi wa Tanzania.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

22 Juni, 2009
 
pop_Full.jpg


stay tuned kuona watakao kuja kupinga huu mradi kwa sababu waliombwa kufund hii project ni KSA...haya ukumbi wenu wapinga maendeleo


5


4

3

2

1
 
"Najua mnatusaidia katika miradi mingi, ikiwamo ile mitatu ya maji na tunashukuru sana. Lakini mahitaji ya maendeleo ya binadamu hayana mwisho… ningefurahi sana kama Saudi Fund ingeshiriki katika kusaidia ujenzi wa barabara hii ya Central Corridor," amesema Rais Kikwete.

Hivi tutaendelea kuomba omba mpaka lini???
 
stay tuned kuona watakao kuja kupinga huu mradi kwa sababu waliombwa kufund hii project ni KSA...haya ukumbi wenu wapinga maendeleo

Nini maana ya maendeleo?
 
Kama mkazi wa Tabora napenda kueleza kuchikizwa kwangu na kitendo cha rais wetu kujifanya anaona mradi huu ni muhimu leo tena karibu na uchaguzi. Moja ya ahadi za serikali hii kwa watu wa Tabora ilikuwa ni kutengeneza barabara hii kabla kipindi chao cha miaka mitano hakijesha. Kutoa taarifa kwa vyombo vya habari eti rais ameomba msaada wa kujenga barabara si kutimiza ahadi hii. Serikali aiche kutubagua wananchi wa mikoa ya Magharibi kwani na sisi ni watanzania.Kifupi hapa hoja si kuwa msaada unatoka wapi hoja ni kwanini mazungumzo haya yawe ni muhimu hadi Ikulu itolee taarifa maalum, huo ni usanii wa wazi wazi.
 
Hakuna nchi iliyo anzisha kasi za maendeleo bila RELI,

Tanzania inahitaji reli imara (central line, north/south, tanga line, Mtwala/makambako). Barabara zitaletwa na RELI.
 
Hakuna nchi iliyo anzisha kasi za maendeleo bila RELI,

Tanzania inahitaji reli imara (central line, north/south, tanga line, Mtwala/makambako). Barabara zitaletwa na RELI.

hivi unajua kinara wa kungoa reli Tanzania alikuwa ni Nyerere?

unajua kama aliamua kwa kususdi kunyoa reli ya kwenda kusuni?

of course hilo limefutwa katika vitabu vya historia

watu wa kusini wakisema wanaambiwa wako obsessed with conspiracies lakini huo ndio kweli
 
hivi unajua kinara wa kungoa reli Tanzania alikuwa ni Nyerere?

unajua kama aliamua kwa kususdi kunyoa reli ya kwenda kusuni?

of course hilo limefutwa katika vitabu vya historia

watu wa kusini wakisema wanaambiwa wako obsessed with conspiracies lakini huo ndio kweli
GT,
Kama unaijua historia hiyo naomba nasi utujuvye jinzi Nyerere alivyong'oa reli ya kusini na sababu zake.
 
GT,
Si uiache hoja iendelee, watu wachangie badala ya wewe kusubiria mlangoni ili umkong'ote rungu kila anayepita !? Mkuu una maslahi kwenye hii hoja nini ???
 
Back
Top Bottom