Ungekuwa ni wewe mke, ungechukua hatua gani?

WALIMWEUSI, it doesn't necessarily take a man to know that there still error in judgement. Mbona reasons zake ziko very staight n concrete? shati likichafukia kazini ndo aje nalo hivyohivyo? cm ya rafiki yake ikiisha charge ndo asimuazime?

Sikatai, unaweza kumuazima rafiki simu yako endapo simu yake ikiisha charge, lakini ebu fikiria, demu wa rafiki yako anaijua namba ya rafiki yake right? Alipigiwa mchana, sms anaituma saa4 usiku, why asiitume kwa namba ya bwanake na hali ni usiku anajua wazi kuwa bwanake hayupo na huyo mtu? Kuhusu shati, sikatai shati linaweza kuchafuka lakini kwa nini asije nalo nyumbani? Ajabu eti anaona uvivu kuja nali ili hali ana gari ingekuwa kwa daladala angesema kweli alishindwa! Looh! Kazi kweli kweli
 
Dah! Yaani wakati nasoma huu uzi nikasikia machungu utadhani ni mimi ndie nimefanyiwa haya.... Dah! Jamani inauma sana...
 
unaendelea na maisha ya mume na mke...huna la kufanya..kesho yake unamkumbusha pia kuleta shati lililofuliwa ofsini pia kesho unampa nguo chafu zoote ndani maana wadada wa ofsini kwake wanapenda kufuafua waendelee kufua...
LOL

Mi siwezi kuishi nae as if hakuna kilichotokea aisee! Yani from that day, sitoshika nguo yake kufua, looh! Kuna uzi aliuanzisha Mtambuzi kuhusu mambo haya haya, kwa nini wanawak ukiwakosea wananuna na kusitisha baadhi ya huduma, sa naomba wanaume mjue kuwa mambo kama haya ndo yanachangia mkose huduma humimu muhimu.
Smile was being sarcastic

Jana mumeo karudi toka kazini kalewa tilalila! Kwa upendo ukamhudumia hadi ukahakikisha amelala vizuri. Then ukasikia sim yake inaita, kwa vile hawezi kuongea ukataka kuipokea ila ikakata. Hujakaa sawa inaingia sms hii ' Baby niko didz nakusubiri, nimekumiss sana'. Ulipoiona ukawa mvumilivu hadi asubuhi ila ile namba ukaihifadhi somewhere.
Asubuhi ukamwambia husband wako about simu yake na sms iloingia. Akaisoma with confidence na kusema kuwa huyo ni demu wa rafiki yake na kwamba aliitumia kuwasiliana nae coz sim yake ilikuwa off. Kwa vile hukutaka malumbano ukakubali lakini ukataka kufuatilia zaidi.

Jioni ya siku hiyo mumeo akakwambia kuwa atachelewa kurudi coz ana kazi ofisini, na around saa 4 usiku ndo atarudi.Ilipofika mida ya saa 1 usiku ukampigia simu yake coz alikuja mtu kumtafta, ukakuta imezimwa. Ukawa anxious kujua why na ukaona utumie sim ya mtu mwingine kupiga ile namba ya jana ilomtext mumeo. Ukakuta haipatikani. Hadi mida ya saa 3 na nusu ndo simu zao zikapatikana tena kwa pamoja. Husband aliporudi home, alikuwa amevaa shati jipya ambalo hakulivaa asubuhi. Ukamuuliza why ana shati jipya akasema alovaa lilichafuka so kaliacha ofisini wadada wafanya usafi wamfulie.

Wewe ukiwa mke hapa, utachukua hatua gani?
fukuza huyo
  1. he's cheating on you
  2. he's taking you for a fool. (hata utetezi wake uko half-@$$ed)
 
hapo dada ni kufanya uchunguz wa kina ili kupata ushahd wa kutosha. kisha ndo ufanye uamuzi. . .
 
loh.....
Kuna wanawake mna uvumilivu jamani...
Mie mnona nisinbepata usingizi??????

Usiku huo pombe zingemuisha na kesho angerudi saa kumi na mbili
 
mhm...wewe ukishaolewa ujiandae kushare huyo mume maana wanaume kucheat wataendelea kufanya hivyo na kama wewe utaondoka kila pale mwanaume anapo cheat basi mwisho wasiku utaolewa mara kibao....kwa maisha ya sasa ya ndoa ni vyema ukajiwekea kuwa ipo siku utagundua ur husband is cheating na ku-accept kuwa hao vimada ni wapita njia tuu
 
Naungana na waliosema kesho pia kwa upole mpe nguo zake akafuriwe na wafanya usafi naona ni wafuaji wazuri kuliko wewe,nakupa pole usitafute makuu utaambulia manundu manake walishageuza wenzao uwanja wa mazoezi
 
[/COLOR]Sikatai, unaweza kumuazima rafiki simu yako endapo simu yake ikiisha charge, lakini ebu fikiria, demu wa rafiki yako anaijua namba ya rafiki yake right? Alipigiwa mchana, sms anaituma saa4 usiku, why asiitume kwa namba ya bwanake na hali ni usiku anajua wazi kuwa bwanake hayupo na huyo mtu? Kuhusu shati, sikatai shati linaweza kuchafuka lakini kwa nini asije nalo nyumbani? Ajabu eti anaona uvivu kuja nali ili hali ana gari ingekuwa kwa daladala angesema kweli alishindwa! Looh! Kazi kweli kweli

Sasa hapo ni kosa la mume au ni uelewa mdogo wa huyo msichana....Kuhusu shati inawezekana akija nalo home atakuta mambo ya usawa so akatakiwa kulifua mwenyewe akaona bora atoe hela lifuliwe...Hatukatai moja kwa moja kwamba anaweza kucheat ila maamuzi hayawezi kutolewa wakati ushahidi haujitoshelezi. There is still a large room for error.Kwa nn usijaribu kutafuta more evidence?
->Like if you find your husband in bed with another woman there is a high probability that he is cheating on you.
 
Back
Top Bottom