Smith Rowe
JF-Expert Member
- Sep 18, 2018
- 3,301
- 5,408
i appreciate ths👍Wanawake/ Mabinti wanakua na wakati mgumu sana kwa vile wao hupenda kwa dhati, shida ni kwetu tusio na huruma. Licha ya kushindwa kuwapenda kwa dhati, hata ile kuthamini upendo wao tu ili usimpotezee muda inatushinda. Mfano mzuri ni huyo jamaa aliyemzalisha binti wa watu na kujitutumua kwenda kwa wazazi, utasema aliambiwa hawana uwezo wa kutunza mjukuu.
Mwingine ni huyo jamaa yake, unamtelekezaje mchumba/rafiki bila mawasiliano kwa kipindi kirefu namna hiyo?
Binti aseme ukweli tu japo kuna wakati sio kila ukweli inabidi usemwe.
Kwangu huyo binti ni mvumilivu na mwenye hofu, angeweza hata aitoe hiyo mimba lakini kakubali kuchukua fedheha na adha zote hadi kajifungua ( Na hapa ndio napingana na wale wanaowakejeli na kuwadharau wanaowaita Single Mother japo hili jina silipendi).
Ningekua ndio huyo jamaa ningemuoa tu tuendelee na mipango ya maisha. Tatizo kwa nnavyowafaham wanawake itamsumbua sana kujisamehe na ataishi akijiona mkosefu siku zote, atahitaji msaada wa kisaikolojia na upendo wa hali ya juu kumpa furaha na amani ya kweli.
Mwisho, majibu yangu na mengine yoote yatakayotolewa hapa ni nadharia tu.
Haya mambo magumu sana yakikupata kiuhalisia, unaweza kujikuta unafanya maamuzi amvayo haujawahi kutafikiria.
Ni kama tulivyovamiwa na Covid kila mtu anakuja na suluhu yake.
Relax..!Msiwe mnatuletea visa ambavyo mwisho wa siku utata unajulikana upo wapi. Hapo wote wameleta mambo ya kisenge....
Mwanaume ndie kaanza kuleta ufala, unasafiri kwenda taifa la mbali sawa ila sasa unaanzaje kuleta ukimya usio na sababu, inamaana hakukuwa na means za kuwasiliana hata kwa Facebook...... Huo si ufala...
Na huyo demu yeye ameshatambulishwa ukweni, miaka miwili yote hakwenda tena ukweni kuwajulia hali ikiwamo kuulizia habari za jamaa....?!
Conclusion:
Acheni kuleta visa au story za kutunga ambazo hazizingatii uhalisia huo ni ufala maana mtu akisoma badala ya kuelimika au kujifunza anapata maudhi...... Coronavirus itusumbue vichwa bado na huu upuuzi pia.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi kama mimi hapo nikifahamu ukweli nampiga chini huyo binti kwasababu ame cheat akiwa na mimi kisa tu distance.
Tofauti na mimi niliepata kidi nikiwa kabla hatujakuwa kwa relationship.
Amwambie ukwel, Na sijaona kosa la binti mahusiano ambayo hamna mawasiliano huwez kuita mahusiano...
Asema alivyopotea hewan ikabd aendlee na maisha yake kama mwanadam wa kawaida naye ana mahitaj yake ya kimwili.
Though hujasema sababu iliyomfanya jamaa apotee hewan kwa muda wote huo ina maana hata familia yake walikua hawawasiliani?
Sent using Jamii Forums mobile app
Yeah maana sababu ya jamaa kukata mawasiliano haijulikani mpka sasaUnataka sema stori haijakamilika?
Najua nipo nje ya mada lakini inakuwaje mnapotezana for years kwenye hii dunia iliyojaa teknolojia mitandao mingi ya kuwezesha mawasiliano kati ya mataifa, kuna fb, insta,whatsap, skype na mingine mingi tu ukishaenda uko nchi za wenzetu ndio mawasiliano yanapotea?
Mm ningemwambia kila kitu before anything.Mistari ya mwisho nadhani ina majibu ya maswali yako, hivyo ndivyo nilivyoamini pia ila huwezi mshauri hivii mtu aliyependa akakuelewa, Cc; Chindy..!
Turudi kwenye mada.!
Mimi ni nani nikupinge?Truth truth truth, as early as possible.
Vinginevyo ndoa itakua ndoano.