Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Bunge kama mwakilishi wa wananchi, linapashwa kuendesha mambo yake kwa uwazi kabisa na kwa kutanguliza maslahi ya nchi kuliko ya vyama vya siasa. Mtu pekee ambaye yuko katika nafasi nzuri ya kuhakikisha kuwa hayo yanatendeka ni spika wa bunge hilo. Kwa bahati mbaya spika aliyopo sasa, tangu aingie madarakani ameonyesha wazi wazi ya kwamba yuko pale kulinda maslahi ya chama chake na wala siyo ya wananchi wanao mlipa. Na hivyo amekuwa akitumia madaraka yake siyo tu kuwanyima fursa wabunge wa upinzani, hasa wa kutoka CDM, kutoa hoja zao kwa uhuru, lakini mara nyingi ameonekana kupindisha sheria ili kuwalinda wabunge kutoka kwenye chama chake kutokana na kusema uongo bugeni. Hali hiyo inaanza kuwafanya baadhi ya wabunge na wananchi kwa jumla kupoteza imani yao kwa mama huyo. Tafrani iliyoibuka jana humo bungeni, ni ushahidi tosha unadhihirisha ni kwa kiwango gani baadhi ya wabunge walivyoanza kutilia shaka uwezo wa mama huyo wa kuwatendea haki wabunge wote bila ya kujali vyama vyao. Pasipo kujirekebisha huko mbele ya safari uenda tukashuhudia visa vya kurushiana ngumi humo bungeni.