Unawezaje endelea na mwanamke anayekuongelea vibaya

shalet

JF-Expert Member
Feb 12, 2013
3,428
3,510
Mkasa huu umenitokea leo asubuhi, mchumba wangu ana kawaida ya kunitembelea wikend kunisaidia kufanya usafi na shughuli nyingine. Kila akija nimekuwa na mazoea ya kupekua simu yake na kwa kuwa mimi ni mtaalamu wa IT huwa na uhakika hakuna kile anaweza nificha.

Mara zote navopekua simu yake nilikuwa naangalia majina ya kiume au watu anaochat nao sana leo nadhani roho mtakatifu aliniongoza nitazame chat yake moja na rafikiake wa kike ambaye namfahamu. Kwa kweli nimesononeshwa na jinsi alivonielezea kwa huyu rafikiake, uhusiano wangu na huyu mwanmke una miezi minne lakin toka mwanzo naanza naye mahusiano mpaka sasa amekuwa ananielezea vibaya sana kwa huyu rafikiake hasa kuhusu sura yangu na urwfu wangu kwa kweli mimi ni mrefu na mweusi kuhusu uzuri uko machoni pa mtu sijijui wengine wananitazamaje ila kama watu wote wananitazama kama huyu mwanamke kwa kweli inasikitisha sana.

Kitu pekee ambacho huyu mwanamke ananisifia ni elimu yangu na kazi yangu hata anavonitaja kwa rafikiake basi atatumia engineer au atataja position yangu ya kazini kitu kingine cha kusikitisha rafikizake waliomba picha yangu akaituma ila ali crop juu walivomuuliza kwann ka crop akasema huyu mwanaume ana sura mbaya mtanicheka kuhangaika kote kule umeishia hapo.

Nilimuuliza kwanni ameniongelea vile kwa rafiki zake akasema alikuwa anawapima ili aone watasemaje ila nakumbuka alishwahi niweka dp pia ali crop kichwa kikawa hakionekani nilivomuuliza kwann ka crop kichwa akasema hataki watu wanijue mpaka nikaonekane kwao.

Ameniomba msamaha hadi kwa kulia nikasema nimesamehe ila akiri yangu inakataa kabisa huyu mwanamke kanizidi miaka kama 4 ila sikuona kama ni tatizo hata rafiki zangu hawajui ila yeye kashindwa nivumilia weusi wangu na urefu wangu.


Naombeni ushauri bila mzaa niachane naye au nimsamehe, sory kwa habari ndefu.
 
Hahaha duh! Pole mtu mzima. Kuwa cropped si dalili nzuri. Anyway, wanasema wanawake mara nyingi wanaweza kujifunza kupenda with time. Pia unaweza jaribu mbinu nyingine kupunguza attention kwenye sura, Bob...

'Heart-throb?..Never, black and ugly as ever / However..I stay coogi down to the sox, rings and watch filled with rocks /'
 
Niliojifunza kwenye uza wako.

1. Kuna tatzo hapo yani demu akuja usaf ndo unatake place coz uhakika wa kuja upo.

2. Ukifika ukweni utatambulishwa hivi. " msimuone hivyo amesoma huyo!"
3. Kiruka njia katulizwa na pesa ulizo nazo, mkitoka atakutaftia sababu atembee kama anachati iv ili utangulie yy abaki nyuma, inshort hatakuwa karibu na wewe kabsa

Over
 
Yani manzi ni miezi minne tu uko nae na kashapajua ghetto kwako?

Mimi manzi angu nipo nae tokea 2014 lakini hapajui kwetu na hata nilipohamia pindi nasepa toka kwetu


Ushauri wangu huyo manzi piga chini kabla hamjaenda mbali, next time akija ghetto piga mechi ya fainali kisha funga league.
 
Back
Top Bottom