Ethical Ninja CEH
JF-Expert Member
- May 16, 2011
- 3,695
- 5,032
Kwa wanawake si jambo la kustaajabisha hata kidogo kumwacha mumewe baada
ya kurubuniwa kwa pesa. Swali langu linakuja kwa wanaume, Linaweza kuwa swali la
ajabu lakini kwanza nikusimulie kisa hiki:-
Fundi ujenzi mmoja(.............) alikubali kumwacha mkewe baada ya kupewa mil.18
na bosi wake na kujengewa nyumba. Ni tukio la kweli kabisa na halina shaka, alimwacha
mkewe ambaye alionekana kumvutia zaidi yule bosi na mpaka sasa yuko naye na kwa
kumbukumbu yangu huu unaweza kuwa mwaka wa 12.
Nimetafakari tu hili jambo nikataka kujua je wewe unayesoma kama ni mwanaume uko tayari
kumwacha mkeo katika mazingira kama hayo, TUFANYE TU HUYO TAJIRI KAKUAHIDI MILIONI 500.
Mke ? Kuuza mke kabisa... ila likija fungu kama 1 Billion nina muuza kwa mkopo... ila nikiwa nimezaa nae basi nitafanya 500 million, maana huyo mda wowote anarudi watoto watatuunganisha