KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,139
Walikuwa wanasiasa?
Sijui yupi kulwa na yupi Doto!
Kaka hawa jamaa walikuwa moto wa kuotea mbali sauti zao zilikuwa tamu kama asali,kila wimbo walioimba ulikuwa una hit,na kila bendi waliyoeenda nayo ilikuwa inakuwa juu,waimbaji sampuli ya hao ndugu waliokuwepo na waliopo ni wachache sana,naweza kuwaweka kundi moja na akina Nico Zengekela,Bichuka na pia kuna mwanamuziki Mtanzania mmoja kafia Kenya aliwahi kupiga na hao mapacha walipokuwa Tancut halafu akaenda Watunjatanjata ya akina Sheggy na mwisho akaenda Vijana kabla ya kuishia Kenya sijui alikuwa aitwa Shaweji sikumbuki .kwa hao watatu hakika walikuwa na sauti za kumtoa nyoka pangoni kiukweliHuyu wa kwanza ndio Mwanamuziki Selemani Kasaloo Kyanga ambaye alikuwa pacha wa Kyanga Songa(huyo wa chini -DOTO) walizaliwa Kongo mwaka 1957. Walikuwa ni nyota katika bendi zote walizopitia nchini zikiwamo, Matimila, Makassy, Maquis, Sambulumaa, Ngorongoro Heroes, Tancut Alimas, Sandton Sound, Kalunde Band na bendi nyingine nyingi . Kasaloo aliyetangulia kuingia nchini akifuatana na Skassy Kasambula mwaka wa 1980, aliweza kutingisha anga za muziki kuanzia pale aliposikika kwenye nyimbo zilizorekodiwa na Super Matimila. Kyanga nae akisindikizana na Issa Nundu walifuatia na sauti zao kuanza kusikika katika recording ya Orchestra Makassy na zile nyimbo Olenge,Bembeya,na pia kuimba na Masiya Radi katika nyimbo Tunagombana Bure. Kyanga alifia Kenya na Kasaloo jijini Dar es Salaam kutokana na mapafu yake kujaa maji. Alikuwa Sandton Sound Band aliyojiunga nayo akitokea Kalunde Band
Swadakta kaka, mmojawapo alioa kwa akina Mpangala na alimtungia wimbo kwa jinsi alivyomjali. Amepiga muziki na akina John Kitime, Kawelee, na wengineo. Enzi hizo Iringa kumekucha. tancut Club, Jumba la maendeleo. Wakiwa tancut walichukua ubingwa wa bendi bora kitaifa.Huyu wa kwanza ndio Mwanamuziki Selemani Kasaloo Kyanga ambaye alikuwa pacha wa Kyanga Songa(huyo wa chini -DOTO) walizaliwa Kongo mwaka 1957. Walikuwa ni nyota katika bendi zote walizopitia nchini zikiwamo, Matimila, Makassy, Maquis, Sambulumaa, Ngorongoro Heroes, Tancut Alimas, Sandton Sound, Kalunde Band na bendi nyingine nyingi . Kasaloo aliyetangulia kuingia nchini akifuatana na Skassy Kasambula mwaka wa 1980, aliweza kutingisha anga za muziki kuanzia pale aliposikika kwenye nyimbo zilizorekodiwa na Super Matimila. Kyanga nae akisindikizana na Issa Nundu walifuatia na sauti zao kuanza kusikika katika recording ya Orchestra Makassy na zile nyimbo Olenge,Bembeya,na pia kuimba na Masiya Radi katika nyimbo Tunagombana Bure. Kyanga alifia Kenya na Kasaloo jijini Dar es Salaam kutokana na mapafu yake kujaa maji. Alikuwa Sandton Sound Band aliyojiunga nayo akitokea Kalunde Band
Swadakta kaka, mmojawapo alioa kwa akina Mpangala na alimtungia wimbo kwa jinsi alivyomjali. Amepiga muziki na akina John Kitime, Kawelee, na wengineo. Enzi hizo Iringa kumekucha. tancut Club, Jumba la maendeleo. Wakiwa tancut walichukua ubingwa wa bendi bora kitaifa.
Kuna mmoja alimuoa Jeni Butinini sijui ni yupi kati ya hao na sijui kama walikuwa na mtoto maana na mimi Iringa niliondoka siku nyingi sana na sijui kama huyo Jeni naye bado yupo. Ila ninachojua familia yao walikuwa wanapenda sana michezo. kuanzia mama na wanawe. nilikuwa nawajua Jeni, Bethi au mama Happy (huyu nasikia naye alisha fariki) na kaka yao Duncan Butini.
Nakumbuka baadhi ya nyimbo zao hao mapacha kama "Mama -------- aah mama aa........... aa naona raha..... miezi tisa ya uchungu tumboni mwako yote umevumlia mama-------------- uchungu mwingi umeupata aa mama..................", na mwingine "Ninakwenda safari safari yenyewe ya masafa marefu ---------------- najua kama utabaki watasema mengi pia wabaya wetu mama watafurahi.......................safari sio kifo mama iyeye subiri nitarudi mama iyeye......................."
Kwa kweli enzi hizo inangawa nilikuwa kinda lakini miziki ya enzi hizo kweli huwezi kuilinganisha hata robo na miziki ya vijana wa leo ambao 90% kati yao kutwa kucha kuwaza ngono. kutoboa masiko, kupaka lipstiki na angel face, kutumia karolite hujui yupi mwanaume na yupi mwanamke ukiwaangalia unaona wote wanawake maana wote wamejipamba na kujiita Sharouharo. hivi mimi sijui kama huwa wanasimamisha
na pengine ndio maana siku hizi wanaume wenye uwezo wachache wengi bila bila viagra hawawezi kwa sababu miili imejaa kemikali, vyakula vya supamaketi n.k. samahanini msinimalize.
Wanaweza kuwa hawa wanafanana sana????