Unawafahamu vizuri madaktari wa muhimbili?

mkuu umeshtukia ee?msiumize vichwa na watu wenye low self esteem.ni kawaida sana kusikia madaktari wa muhimbili wauaji,manurse wa mwananyamala wanaua watoto,hospitali ya amana ni machinjion n.kingawa ukijaribu kuuliza uthibitisho wa madai haya utasikia vijistori vya kutunga!Kinachoshangaza huwezi kusikia madaktari au manurse wakisifiwa hasa pale afya ya mtanzania inapoboreka mfano vifo vya mama na mtoto vikipungua sana sana utasikia sifa inaenda kwa mkuu wa mkoa au kwa chama tawala.Fundi mchundo haelewi kwamba serikali inalazimisha madaktari bingwa waende mikoani sasa anategemea madakta hawa wakatoe emperical treatment kama Clinical officers?!wanahitaji vitu kama C.T SCANNERS n.k kama tunaweza kununua mashangingi zaidi ya 200 kwa wabunge iweje tushindwe kununua hizo scanners kwa mikoa 28?

Hiyo ni kuwambia ngoma kwako. Si siku nyingi sana Mwaka huu kuna muhudumu wa afya (nurse/mid wife) wa pale TMJ alifanya "kazi yake kwa mujibu wa kiapo" kwa kumtolea damu mama aliyekuwa akijifungua akiwa hana damu. Aliokoa uhai wa mama huyu pamoja na mtoto. Japo muhudumu huyu alikuwa mwenyewe alifanya hayo yote.

JE HUKUSIKIA MAJIBU YA WANANCHI, WAMILIKI WA HOSPITALI, FAMILIA YA MGONJWA, VYOMBO VYA HABARI ETC KWA MUHUDUMU HUYU?

Tuache propaganda kwenye mambo yanayoonekana wazi.
 
ZOTE NI MUHIMBILI NA ZIPO MUHIMBILI NA ZOTE ZINAFANYA KAZI KWA UTARATIBU MMOJA WA UOZO. Kama sivyo, mheshimiwa Malechela angepelekwa hapo! Tusidanganyane, Tz hatuna "huduma ya Afya kwa walala hoi na watu wa kati"

Na hapo kwenye red unadhani hilo tatizo limesababishwa na madaktari?

Pia husipende kukurupuka kuongelea mambo ambayo huna ujuzi/taarifa nayo. Muhimbili National Hospital (MNH) ni taasisi nyingine tofauti kabisa na Muhimbili Orthopedic Institute (MOI)...ni taasisi zenye uongozi tofauti kabisa (Wakurugenzi, mameneja, wakuu wa vitengo na bodi), wana taratibu tofauti kabisa za kiutendaji, wana salary scale tofauti kabisa, na kila taasisi inapokea ruzuku tofauti toka Wizara ya Afya!

Shame on you kushangilia Malecela kwenda kufanyiwa upasuaji wa moyo nje ya Nchi wakati MNH wapo Drs Wandwi, Nyawawa, Ussiri, na Nyangassa wanafanya operation hizo kutwa kuchwa kwa matokeo mazuri sana!
 
Ozzie, P53...naona mnabishana na mbumbumbu Fundi 'Feki' Mchundo ambaye anaonekana wazi ana 'chuki binafsi' na fani ya udaktari, labda alishindwa kuafulu kiasi cha kuweza kujoin medical school..maana naona ametoka kwenye mada ya rushwa na kukimbilia affairs za medical profession per se! Mnapoteza muda wenu, najua Ozzie una wagonjwa zaidi ya 100 wanakusubiri Mwaisela, na wanafunzi wa udaktari kama 30 wansubiri uwape shule ili waje kutukanwa na watu mbumbumbu ka Fundi huyu feki. Mtaokoa muda wenu kama mtaenende kwenye kazi zenu na kuachana na huyu jamaa!
Hata mimi nilishamshtukia. Ana wivu fulani. Atakuwa kaungaunga mpaka hapo alipo. Nina wasiwasi kama ana elimu ya kutosha zaidi ya ku google. Maana hata anaamini daktari anaweza soma degree ya miaka mitano kwa miaka 13 bila ku disco!!!
 
Ozzie, P53...naona mnabishana na mbumbumbu Fundi 'Feki' Mchundo ambaye anaonekana wazi ana 'chuki binafsi' na fani ya udaktari, labda alishindwa kuafulu kiasi cha kuweza kujoin medical school..maana naona ametoka kwenye mada ya rushwa na kukimbilia affairs za medical profession per se! Mnapoteza muda wenu, najua Ozzie una wagonjwa zaidi ya 100 wanakusubiri Mwaisela, na wanafunzi wa udaktari kama 30 wansubiri uwape shule ili waje kutukanwa na watu mbumbumbu ka Fundi huyu feki. Mtaokoa muda wenu kama mtaenende kwenye kazi zenu na kuachana na huyu jamaa!

Kumbe mko wengi? Hivi, wewe msomi, niambie affairs za medical profession ni zipi? Na unawezaje kuongelea rushwa katika medical professinon bila kuzungumzia "affairs" zake? Tatizo ni kuwa mnajidanganya kuwa kwa sababu nyinyi ni madaktari basi mna busara kuliko yeyote yule! Kama shule yenyewe ndiyo inawapelekea kutoa upuuzi mnaojaza humu basi heri ambao hatukwenda hiyo shule.

mkuu umeshtukia ee?msiumize vichwa na watu wenye low self esteem.ni kawaida sana kusikia madaktari wa muhimbili wauaji,manurse wa mwananyamala wanaua watoto,hospitali ya amana ni machinjion n.kingawa ukijaribu kuuliza uthibitisho wa madai haya utasikia vijistori vya kutunga!Kinachoshangaza huwezi kusikia madaktari au manurse wakisifiwa hasa pale afya ya mtanzania inapoboreka mfano vifo vya mama na mtoto vikipungua sana sana utasikia sifa inaenda kwa mkuu wa mkoa au kwa chama tawala.Fundi mchundo haelewi kwamba serikali inalazimisha madaktari bingwa waende mikoani sasa anategemea madakta hawa wakatoe emperical treatment kama Clinical officers?!wanahitaji vitu kama C.T SCANNERS n.k kama tunaweza kununua mashangingi zaidi ya 200 kwa wabunge iweje tushindwe kununua hizo scanners kwa mikoa 28?

Another educated fool. Huyo daktari bingwa asiyeweza kutoa huduma bila CT Scanner kweli anastahili kujiita daktari bingwa? Kumbe ndio maana watu wanakufa ovyo kwa sababu hawana CT scanner za kufanyia uchuinguzi! Mna tofauti gani na hao wabunge ambao wanaona ufahari kuendeshwa katika gari la dola 100,000 wakati waliompigia kura hata baiskeli inawashinda. Kama hao, mnang'ang'ania CT scanner wakati infrastructure ya kuzihudumia haipo. Kama hao, mnataka toys za miamilioni ya dola wakati watu wenu kinachowasumbua ni utapia mlo, malaria, n.k. Wote hamna msaada kwa mtanzania wa kawaida. Badala ya kuendekeza hivyo vi sense ya victim-hood, wasikilizeni wananchi wanapolalamika badala ya kuwabeza.

hivi hii michango ya harusi huwa inatolewa na watanzania hawa hawa wasioshika 1000 kwa mwezi?nyie ndo wale mnaoshindwa kuchangia huduma za mgonjwa lakini wepesi sana kuchangia majeneza na tisheti(sare) za msiba.Shame on you!Kweli unaendana na username yako hufikirii, kazi yako ni kuangalia manual na kufanya tu.

Hivi kwa upuuzi wako mnapoona wapuuzi wenzenu wakiziba barabara siku za jumamosi basi mnaamini kuwa watanzania wote wako hivyo? Hao wanaotembea kwa mguu kila siku kutoka Kimara au Mbagala unadhani wanafanya hivyo kwa sababu wanataka kuwa na six-packs! Watanzania wengi ni maskini wa kutupwa, na ndio hawa wanaohitaji msaada wenu. Hao mnaotaka kushindana nao na ma-SUV zamani walishawaona hamnazo na kuamua kufuata tiba India, Afrika ya Kusini n.k. Hivi hamuoni aibu kuwa wananchi wamekata tamaa na huduma zenu kiasi cha kuamini kuwa kikombe cha maji ni bora kuliko utaalam wenu? Kuweni humble kidogo na msibweteke na huo usomi wenu. Kama utafanya kazi yako kwa uwezo wako wote, watu watakushukuru na kukuombea. Hiyo ni zaidi kuliko mapambio ya hapa JF.

Amandla......
 
Na hapo kwenye red unadhani hilo tatizo limesababishwa na madaktari?

Pia husipende kukurupuka kuongelea mambo ambayo huna ujuzi/taarifa nayo. Muhimbili National Hospital (MNH) ni taasisi nyingine tofauti kabisa na Muhimbili Orthopedic Institute (MOI)...ni taasisi zenye uongozi tofauti kabisa (Wakurugenzi, mameneja, wakuu wa vitengo na bodi), wana taratibu tofauti kabisa za kiutendaji, wana salary scale tofauti kabisa, na kila taasisi inapokea ruzuku tofauti toka Wizara ya Afya!

Shame on you kushangilia Malecela kwenda kufanyiwa upasuaji wa moyo nje ya Nchi wakati MNH wapo Drs Wandwi, Nyawawa, Ussiri, na Nyangassa wanafanya operation hizo kutwa kuchwa kwa matokeo mazuri sana!

Asante kwa mchanganuo wako mzuri na laumu lako kuwa "nimekurupuka". Yawezekana ndio na sivyo.

PAMOJA NA YOOOTE ULIYOELEZA KUNA VI2 HUJUI NDANI YAKE; UTENDAJI WA MOI NA MNH NI SAWA HAUNA TOFAUTI YOYOTE.

Je unakumbuka MOI ilipoanzishwa? Watendaji wa awali walipatikana wapi? Ni nani mama wa MOI?
"Like mother like daughter"
 
Hata mimi nilishamshtukia. Ana wivu fulani. Atakuwa kaungaunga mpaka hapo alipo. Nina wasiwasi kama ana elimu ya kutosha zaidi ya ku google. Maana hata anaamini daktari anaweza soma degree ya miaka mitano kwa miaka 13 bila ku disco!!!

Naam, elimu yangu ni ya ku-google. Kama nilivyomwambia mwenzio, kama usomi wenyewe ndio huu mnaouonyesha hapa ( bila aibu unajifahamisha kama daktari bingwa) heri ni bakie mbumbumbu.

Ni mwenzako ndiye aliyesema kuwa mnasoma miaka 13 na sio mimi. Kwangu mimi, msome miaka miwili, minne, mia wala haileti tofauti kama mawazo yenu yatabaki yamejaa ubinafsi mnaouonyesha hapa. Hamna faida kwangu na sehemu kubwa ya wananchi. Msaada wenu ni kwa hao wanaoweza kuwalipa konsaltansi fii ya malaki ili muwapime kifua. Jidanganyeni kuwa mnaonewa wivu lakini mjue kuwa laana za hao msiowatendea haki zitakuja wafikia siku moja.

Amandla........
 
Hao wanaotembea kwa mguu kila siku kutoka Kimara au Mbagala unadhani wanafanya hivyo kwa sababu wanataka kuwa na six-packs! Watanzania wengi ni maskini wa kutupwa, na ndio hawa wanaohitaji msaada wenu. Hao mnaotaka kushindana nao na ma-SUV zamani walishawaona hamnazo na kuamua kufuata tiba India, Afrika ya Kusini n.k.......

Hili ndio hao madakitari wangejiuliza wanamkomoa nani..?
 
Hili ndio hao madakitari wangejiuliza wanamkomoa nani..?

Wakati wetu, wasomi kweli walikuwa watoto wa wakulima na walijua adha na umaskini wa wazazi wao. Sasa hivi watoto wa hao wasomi ndio wamekuwa wasomi na hawajui adha na umaskini wa babu na bibi yao. Hawa wamekuwa wakipelekwa shule kwa SUV, kwenda pikniki na kuhudhuria harusi zinazogharimu mamilioni. Hawa, fools, wanadhani kuwa Tanzania yote ni hivyo kwa hiyo unaweza kubeba mashine ya dola milioni moja na kuipachika Tabora, Bukoba, Lindi au Sumbawanga na mambo yatakuwa safi tu. Mbaya zaidi ni hao wazazi wao ambao waliujua umaskini wa wazazi wao basi wamekunywa kool-aid ya Neo-liberalism na kujiona kuwa wao na vizazi vyao wako entitled kwa hizo perks kama SUVs, mamilioni benki n.k. Hawa vijana wako ( na inavyoelekea baadhi ya walimu wao) so delusional hawaelewi kuwa kweli kuna watu wanakunywa muarubaini si kwa kupenda lakini huo uwezo wa kufika huko hospitali hawana! Neno empathy hawalijui, wanachotaka wao ni uwezo wa kunywa Pina Colada,n.k. kila jioni kwa vile tu ati masomo waliyosoma ni magumu! Pleease.

Amandla......
 
Jamani tutambue mchango wa madaktari, si wote wenye matatizo kama tunavyofikiri, Last month mdogo wangu anayesoma shule ya boarding aligundulika ana kisukari, daktari wa hospitali iliyo karibu na shule alimdiscourage sana kwamba ni ugonjwa atakaokuwa nao mpaka mwisho, lazima achome sindano, shule sidhani kama ataweza kwa muda huu boarding labda angekuwa home n.k Mdogo wangu alikuwa frustrated sana akawa wa kulia kila siku, nikapiga simu nikamleta kwa Dr. mmoja Specialist wa sukari, Huwezi kuamini that single day the way Dr. alivyompokea, akaongea naye, akampa councelling, namna ya kuhandle na dawa ofcourse, mdogo wangu kuanzia siku hiyo alihisi amepona though bado anatumia dawa, Dr. alikuwa mkarimu sana, Nilimfurahia, SO KUNA MADOCTOR WENGINE VERY CARING, WE HAVE TO APPRECIATE THEM.
Huwa naumia kweli madaktari wote wanapopakwa matope kwa makosa ya daktari mmoja ua madaktari wachache...hivi mnajua kuna madaktari wangapi ni wazuri na wenye upendo wa hali ya juu kwa wagonjwa? Wanatoa mpaka hela zao mfukoni kununulia dawa wagonjwa hoe hae, na wengine wanaokuwa discharged ahata nauli za kurudi nyumbani hawana? Hivi mnajua kuna madaktari wangapi wanaenda extra miles mpaka kugombana na manesi, wakubwa wao wa kazi kutetea haki za wagonjwa wao? Hivi mnajua kuna wagonjwa wangapi walio mawodini na clinic hutukana na kudhalilisha madaktari na manesi na bado wanapata huduma stahiki toka kwa hao hao waliowatukana tena kwa upendo tu. Hivi mnajua kuna madaktari wangapi hawakati tamaa hata kwa wagonjwa ambao wenyewe, ndugu zao na hata baadhi ya wahudumu wengine wa afya wamekata tamaa na huyu daktari anajitahidi na hawa wagonjwa wanapona. JEEE, mmehswahi kuweka thread ya kuwapongeza/kuwashukuru/kuwasifu kwa utendaji wao wa kazi katika forums kama hizi ili kuwamotivate? Mbona kila thread ni kwa ajili ya ubaya wao tuu au ubaya wa wenzao na hakuna za kuacknowledge uzuri wao?

Hivi mnajua kuna madaktari wangapi wanakatishwa tamaa na wengine kuacha kabisa kufanya kazi hospitali za serikali au kazi za kidaktari kabisa kutokana na comments na lawama zenu hizi...I am the living proof, I gave my everything to my patients..always went ana extra mile, but I left practising clinical medicine (surgery) kwa sababu ya kukatishwa tamaa na watu wenye mrengo kama huo wenu, I never regretted. And I know a number of my fellow colleagues ambao wamejoin programmes/research/public health/private practice kama mimi sababu ya mirengo hiyo hiyo!

Till when we will keep on loosing our good and dedicated doctors kwa mambo hizi tuu?! kuna boards za kupeleka haya malalamiko za kiserikali, dola na kitaaluma pia...mbona malalamiko hayaendi huko yanakuja huku JF?

Hivi kweli katika madaktari wote wanaokesha MOI kila siku wakati we unakoroma baada ya kupata cha usiku kwa mkeo, woooote hao wabaya wala rushwa, hawajali? Kama wapo wazuri, unawaacknowledge vipi? Hivi hakuna mtu humu amepewa matibabu mazuri na akaona kabisa daktari wake amefanya ziada kumhudumia yeye au mtu amhusuye, mbona hamna confessions?!

This is so discouraging, so frustrating, so annoying...am sorry to say so!
 
Judges should not hear cases in which they have a financial interest. Reporters should not write stories about companies in which they have a financial interest. By the same token, doctors should not have a financial interest in treatments they provide, or accept gifts from patients they prescribe drugs. Unfortunately, this is not the case in these professions and others in the country. The reality is that corruption does exists in every profession including the education, health, public service, the police finance, local government, legal sectors, etc. You may not be one of the corrupt persons, but corruption is prevalent in the health sector just as in other sectors. That is a naked truth. Some may not believe that health professionals could have conflicts of interest that affect their judgement, but in fact this can be the case.

Corruption in the health sector is a concern in all countries particular developing countries and can't see why Tanzania should be exempted. Despite limited research in Tanzania, the health sector appears to be particularly vulnerable to corruption. This is the result of many processes with high risks of bribery. The health sector is marked by a high degree of imbalances of information and an inelastic demand for services. The high degree of discretion given to professionals in choosing services for patients put patients in a vulnerable position. This is particular where the relationship is that of trust and confidence. In Tanzania, health professionals have assumed a cultural role as trusted healers who are above suspicion.

The Warioba Report (1996) revealed that corruption in the health sector is serious problem. In a recent empirical study conducted by Sikika in 2010 titled PETTY CORRUPTION IN HEALTH SERVICES IN DAR ES SALAAM AND COAST REGIONS shows that corruption is entrenched in the health services. It involves all cadres of health workers whose motives are varied.

According to the study, patients, their relatives and the general population are not mere objects who suffer the consequences of the corrupt system either. Rather, they also sustain the system by offering bribes even when not asked for. This is because of the social norm which appears to have emerged, that one cannot obtain high quality care unless one knows or is known to health workers. Without such connections, one has to pay a bribe as an incentive for health workers to do what they were trained and are paid for. This social norm is associated with mutual definition of situations in which bribes are deemed to be appropriate.

I have been following this thread and I have to say that I am disappointed with some posts which I have read so so far. Instead of abusing each other, download and read this recent empirical study on corruption in the health sector then come back her and provide your analysis. You can download the report at: http://www.sikika.or.tz/yavworks/Researches/Soma English Book F2 final_Corruption Study.pdf
 
Jamani tutambue mchango wa madaktari, si wote wenye matatizo kama tunavyofikiri, Last month mdogo wangu anayesoma shule ya boarding aligundulika ana kisukari, daktari wa hospitali iliyo karibu na shule alimdiscourage sana kwamba ni ugonjwa atakaokuwa nao mpaka mwisho, lazima achome sindano, shule sidhani kama ataweza kwa muda huu boarding labda angekuwa home n.k Mdogo wangu alikuwa frustrated sana akawa wa kulia kila siku, nikapiga simu nikamleta kwa Dr. mmoja Specialist wa sukari, Huwezi kuamini that single day the way Dr. alivyompokea, akaongea naye, akampa councelling, namna ya kuhandle na dawa ofcourse, mdogo wangu kuanzia siku hiyo alihisi amepona though bado anatumia dawa, Dr. alikuwa mkarimu sana, Nilimfurahia, SO KUNA MADOCTOR WENGINE VERY CARING, WE HAVE TO APPRECIATE THEM.

Mimi sijasema madaktari WOTE ni waovu. Kama vile si trafik wote wanaoendekeza rushwa.Watoza ushuru nao si wote wanaovuta mlungula. Hata mahakimu nao, si wote wanaukula rushwa au mafundi mchundo. Katika taaluma zote hizi wako wazuri na wabaya. Ninachopingana na hawa wasomi ni:
  1. Wao kukana kuwa kuna madaktari wabovu wanaoendekeza rushwa. Daktari Bingwa amefikia mpaka hatua ya kudai kuwa wanaoendekeza rushwa ni wale wa chini kama wauguzi, wafagizi n.k. Kututukana zaidi wanadai kuwa hatujui tofauti kati ya daktari na nesi ndio maana tunawasingizia malaika wa watu!
  2. Dhana ya kudai kuwa wanakula rushwa (contradiction hawaioni hapa) kwa sababu ya mishahara midogo na kutothaminiwa na serikali. Nimewaomba wanitajie ni taaluma ipi ambayo ina starting salary zaidi ya madaktari, wameshindwa. Ninachoamini kuwa mpenda rushwa hata umlipe vipi, ataendelea kudai rushwa. Wala rushwa wakubwa si maskini.
  3. Dhana ya kudai kuwa ni lazima walipwe mishahara mikubwa kwa sababu masomo yao ni magumu. Kwangu mimi hii ni dhana ya kipuuzi kwa sababu ugumu wa masomo unategemea mtu. Kuna watu wanamudu hesabu lakini historia inawasumbua n.k. Ninachoweza kuwaelewa ni kama watadai walipwe vizuri kwa sababu kazi yao ni stressful kuliko kazi nyingi nyingine. Lakini pamoja na kusema hivyo, mshahara wao ni lazima ulingane na hali halisi ya nchi yetu yotena si kujilinganisha na vibaka wachache waliofanikiwa kujipendelea.
  4. Dhana ya kudai kuwa bila vyombo kama CT Scanner hawawezi kutoa huduma nzuri. Hii ni kama leo, mhandisi aseme bila kompyuta hawezi kufanya kazi wakati hesabu nyingi anaweza anachohitaji ni calculator tu.
  5. Dhana ya kusema CT Scanner zisambazwe mikoa yote bila kuangalia kama tuna infrastructure ya kuzihudumia. Hivi kweli katika nchi ambayo umeme wake hauaminiki, ina mafundi mchundo wenye uwezo wa kuziendesha na kuzihudumia wachache, na wengi wa wananchi wake matatizo yao yanaweza kutatuliwa na basic preventive measures, kweli ijitose kununua mashine 28 zenye bei ya karibu dola milioni moja kila moja. Kwanza kabla ya kuziweka katika hayo mahospitali itabidi zote zikarabatiwe kwa kiasi kikubwa ili kuhakikisha usalama wa chombo chenyewe. Halafu hata kikiweko, ni wananchi wangapi wenye uwezo wa kulipa sh.laki moja ili wafanyiwe scan.
Madaktari kama huyo aliyekuhudumia ndiye tunaowahitaji. Ndio maana yanapotokea magugu ambayo yanaweza kuwaharibia sifa zao, tunawapigia kelele. Rushwa ni mbaya si kwa wagonjwa peke yao, hata kwa madaktari wasiohusika wanakuwa affected. Wasio chukua rushwa wanaonekana ni wasiliti na mara nyingi wanawekewa kibano.

Amandla.......
 
ZOTE NI MUHIMBILI NA ZIPO MUHIMBILI NA ZOTE ZINAFANYA KAZI KWA UTARATIBU MMOJA WA UOZO. Kama sivyo, mheshimiwa Malechela angepelekwa hapo! Tusidanganyane, Tz hatuna "huduma ya Afya kwa walala hoi na watu wa kati"
unaelewa ulichoandika?
 
Hiyo ni kuwambia ngoma kwako. Si siku nyingi sana Mwaka huu kuna muhudumu wa afya (nurse/mid wife) wa pale TMJ alifanya "kazi yake kwa mujibu wa kiapo" kwa kumtolea damu mama aliyekuwa akijifungua akiwa hana damu. Aliokoa uhai wa mama huyu pamoja na mtoto. Japo muhudumu huyu alikuwa mwenyewe alifanya hayo yote.JE HUKUSIKIA MAJIBU YA WANANCHI, WAMILIKI WA HOSPITALI, FAMILIA YA MGONJWA, VYOMBO VYA HABARI ETC KWA MUHUDUMU HUYU?Tuache propaganda kwenye mambo yanayoonekana wazi.
unadhani tukio kama hilo likitokea Hospitali ya serikali utalisikia?!
 
  1. Dhana ya kudai kuwa ni lazima walipwe mishahara mikubwa kwa sababu masomo yao ni magumu. Kwangu mimi hii ni dhana ya kipuuzi kwa sababu ugumu wa masomo unategemea mtu. Kuna watu wanamudu hesabu lakini historia inawasumbua n.k. Ninachoweza kuwaelewa ni kama watadai walipwe vizuri kwa sababu kazi yao ni stressful kuliko kazi nyingi nyingine. Lakini pamoja na kusema hivyo, mshahara wao ni lazima ulingane na hali halisi ya nchi yetu yotena si kujilinganisha na vibaka wachache waliofanikiwa kujipendelea.
Amandla.......

Mkuu kwa mtu kuchukua mshahara mdogo kuelezea suala la rushwa ni sahisi sana. Ni rahisi kwa mtu kusem kuwa kama mtu analipwa mshahara mdogo, basi kuna uwezekano mkubwa akachkua rushwa. Tatizo la hii dhana ni kuwa rushwa huwa inatokea katika levels zote za mishahara. Anayelipwa mshahara mdogo anachukua rushwa. Anayelipwa mshahara mkubwa naye anachukua rushwa. hao mafisadi tunaolalamika hapa kila siku wanalipwa mishahara midogo? kwa hiyo itakuwa ni makosa kwa mtu kusema eti kuongeza mishahara kutapunguza rushwa. Kama mtu anachukua rushwa hata ukimwongezea mshahara bado ataendelea kuchukua rushwa tuu. Na hii dhana ya kuwa mtu alipwe mshahara mkubwa kwa kuwa masomo yake walikuwa magumu ni dhana potofu. Mtu kama huyo ndiye anayedharau fani za watu wengine na itakuwa ngumu kufanya naye kazi in a multidisciplinary team.
 
Mimi sijasema madaktari WOTE ni waovu. Kama vile si trafik wote wanaoendekeza rushwa.Watoza ushuru nao si wote wanaovuta mlungula. Hata mahakimu nao, si wote wanaukula rushwa au mafundi mchundo. Katika taaluma zote hizi wako wazuri na wabaya. Ninachopingana na hawa wasomi ni:
  1. Wao kukana kuwa kuna madaktari wabovu wanaoendekeza rushwa. Daktari Bingwa amefikia mpaka hatua ya kudai kuwa wanaoendekeza rushwa ni wale wa chini kama wauguzi, wafagizi n.k. Kututukana zaidi wanadai kuwa hatujui tofauti kati ya daktari na nesi ndio maana tunawasingizia malaika wa watu!
  2. Dhana ya kudai kuwa wanakula rushwa (contradiction hawaioni hapa) kwa sababu ya mishahara midogo na kutothaminiwa na serikali. Nimewaomba wanitajie ni taaluma ipi ambayo ina starting salary zaidi ya madaktari, wameshindwa. Ninachoamini kuwa mpenda rushwa hata umlipe vipi, ataendelea kudai rushwa. Wala rushwa wakubwa si maskini.
  3. Dhana ya kudai kuwa ni lazima walipwe mishahara mikubwa kwa sababu masomo yao ni magumu. Kwangu mimi hii ni dhana ya kipuuzi kwa sababu ugumu wa masomo unategemea mtu. Kuna watu wanamudu hesabu lakini historia inawasumbua n.k. Ninachoweza kuwaelewa ni kama watadai walipwe vizuri kwa sababu kazi yao ni stressful kuliko kazi nyingi nyingine. Lakini pamoja na kusema hivyo, mshahara wao ni lazima ulingane na hali halisi ya nchi yetu yotena si kujilinganisha na vibaka wachache waliofanikiwa kujipendelea.
  4. Dhana ya kudai kuwa bila vyombo kama CT Scanner hawawezi kutoa huduma nzuri. Hii ni kama leo, mhandisi aseme bila kompyuta hawezi kufanya kazi wakati hesabu nyingi anaweza anachohitaji ni calculator tu.
  5. Dhana ya kusema CT Scanner zisambazwe mikoa yote bila kuangalia kama tuna infrastructure ya kuzihudumia. Hivi kweli katika nchi ambayo umeme wake hauaminiki, ina mafundi mchundo wenye uwezo wa kuziendesha na kuzihudumia wachache, na wengi wa wananchi wake matatizo yao yanaweza kutatuliwa na basic preventive measures, kweli ijitose kununua mashine 28 zenye bei ya karibu dola milioni moja kila moja. Kwanza kabla ya kuziweka katika hayo mahospitali itabidi zote zikarabatiwe kwa kiasi kikubwa ili kuhakikisha usalama wa chombo chenyewe. Halafu hata kikiweko, ni wananchi wangapi wenye uwezo wa kulipa sh.laki moja ili wafanyiwe scan.
Madaktari kama huyo aliyekuhudumia ndiye tunaowahitaji. Ndio maana yanapotokea magugu ambayo yanaweza kuwaharibia sifa zao, tunawapigia kelele. Rushwa ni mbaya si kwa wagonjwa peke yao, hata kwa madaktari wasiohusika wanakuwa affected. Wasio chukua rushwa wanaonekana ni wasiliti na mara nyingi wanawekewa kibano.Amandla.......
labda ueleze hiyo miundo mbinu inayohitajika ili CT SCAN iweze kutumika huko mikoani.kwa hiyo wewe unafurahia sana mgonjwa anapokwenda muhimbili na kuambiwa 'mashine yetu ya CT SCAN ni mbovu'halafu akahitajika kwenda aga khani kulipia sh 400,000 kwa huduma hiyo? Acha kutumia ugwe mgongo(spinal cord) tumia ubongo uliopewa.Yaani wewe unafikiria malaria tu bila kujua hatari ya magonjwa yatokanayo na maendeleo.tatizo utoto unakusumbua ukikua utaacha.
 
Mkuu yaani nilivyoiona hii thread umenichochea hasira zangu kwa hawa jamaa... coz na mimi nilikuwa na mzee wangu pale tulipata shida sana mpka alipofanyiwa operation. MOI kwa kweli tubadilike maana mwisho wa siku wote tutarudi mavumbini. Vitu vyote tuanavyotamani na kujilimbikizia tutaviacha hapa hapa duniani. Yaani inaogopesha sana coz tulimpeleka ndugu yetu tukaambiwa atakaa miezi mitatu kama hatutaoa mlungula. Tukawapatia 2k siku 3 akawa amefanyiwa operation na kuruhusiwa huku tukiwa tumeshasota zaidi ya wiki tatu pale.....
 
labda ueleze hiyo miundo mbinu inayohitajika ili CT SCAN iweze kutumika huko mikoani.kwa hiyo wewe unafurahia sana mgonjwa anapokwenda muhimbili na kuambiwa 'mashine yetu ya CT SCAN ni mbovu'halafu akahitajika kwenda aga khani kulipia sh 400,000 kwa huduma hiyo? Acha kutumia ugwe mgongo(spinal cord) tumia ubongo uliopewa.Yaani wewe unafikiria malaria tu bila kujua hatari ya magonjwa yatokanayo na maendeleo.tatizo utoto unakusumbua ukikua utaacha.

Mwenzako ananiita kizee, wewe unadai mimi utoto ndio unanisumbua. Nyinyi kweli madaktari?

Sasa kama CT Scanner iliyofungwa katika mji mkuu wetu wenye kila aina ya wataalamu, majenereta kibao, ilani kuwa umeme usikatwe hapo, na bado unakiri inaharibika? sasa unadhani hiyo itakayofungwa Tabora itapona kweli. Au unadhani kwa sababu itakuwepo nyingine Morogoro basi kila wakati hiyo ya Muhimbili itakapoharibika hao wagonjwa watkimbilia Morogoro ili kukwepa kulipa sh. 400,000 za Aga Khan?

Magonjwa yanayotokana na maendeleo mtaugua nyinyi. Mkulima ambae mpaka leo anatumia jembe la mkono atauguaje magonjwa hayo unayoyaita yanayotokana na maendeleo. Ugonjwa unaosumbua wananchi wengi si presha au kisukari bali ni malaria. Na wengi wanaondoka kwa sababu sumuni ya kununua chandarua hawana. Leo unataka kuwapelekea CT Scanner ambayo utamdai sh 100,000 mtakapoitumia kumpimia.

Amandla......
 
Mimi ndio maana nasema hamjaelimika. Huyo specialist daktari anaupataje kama hajafunzwa kwanza kufunga vidonda na kutibu malaria? Au unataka kutuambia specialization imekuwa ni fani? Haujui udhaifu wa kusema kuwa huyo mtu specialist anahitaji vifaa ambavyo ni vya hadhi yake! Yaani kabla ya CT Scanners hapakuwa na ma-consultant! Huyo specialist anayeshindwa kumtibu mgonjwa wa utapia mlo mpaka awe na diagnostic tools za hadhi yake basi hatufai.Usitudanganye hapa. Haujaishi maisha duni wewe. Familia zilizoduni zitauza kuku wangapi mpaka wapate hayo mahela mnayotaka kudai? Haujui shida wewe. Zungukia nchi yako, ndiyo utajua umaskini.Amandla.......
kwa kawaida mgonjwa hutokea nyumbani>dispensary>health centre>district hospital>regional hospital(specialists)>referal hospital(specialists)>specialized hospitals(super specialists)mtiririko huo hapo juu unaonyesha mpangilio wa matibabu ya mgonjwa na kila unapopanda ngazi ndivo unavyokutana na magonjwa magumu na ya ajabu.it is very rare kwa specialist(labda yuko kwenye research) kukutana na mgonjwa wa malaria,mara nyingi mgonjwa huyu huishia level ya dispensary au hata duka la dawa la fundi mchundo.sasa mbumbu kama wewe hutaki daktari bingwa aekewe Ct scan ili asubiri kufunga vidonda na kutibu malaria!!kama huelewi nitakutafutia michoro kilaza mkubwa we.
 
kwa kawaida mgonjwa hutokea nyumbani>dispensary>health centre>district hospital>regional hospital(specialists)>referal hospital(specialists)>specialized hospitals(super specialists)mtiririko huo hapo juu unaonyesha mpangilio wa matibabu ya mgonjwa na kila unapopanda ngazi ndivo unavyokutana na magonjwa magumu na ya ajabu.it is very rare kwa specialist(labda yuko kwenye research) kukutana na mgonjwa wa malaria,mara nyingi mgonjwa huyu huishia level ya dispensary au hata duka la dawa la fundi mchundo.sasa mbumbu kama wewe hutaki daktari bingwa aekewe Ct scan ili asubiri kufunga vidonda na kutibu malaria!!kama huelewi nitakutafutia michoro kilaza mkubwa we.

Mkuu mwenzako nimeamua kuachana nae huyo mtu.Maana haelewi kabisa anachokiongea.Umeona hapo alivyoandika?Eti CT inatumika kupima presha na kisukari,duh!Tatizo la kujifanya unajua kila kitu,kisa umesoma vihistoria na vifilosofi.
 
Back
Top Bottom