GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Habarini wana JF. Bila shaka kuna watu hawawafahamu vizuri madaktari wa muhimbili. Ni watu watanashati wenye sura zenye upole na upendo. Ukikutana nao ni watu wastaarabu ambao kwa mtazamo wa haraka ni watu wenye maadili mazuri ya kazi. OLE WAKO UINGIE ANGA ZAO! Nazungumza kutokana na uzoefu nilioupata kule MOI.
Nenda na Bima yako nenda na pesa yako ya kulipia vyeti halali, Unajua wanachokifanya? Utapangiwa tarehe kila siku mpaka utoe yale malipo yasiyo na risiti ndo utapata huduma. Nawaombeni madaktari kama mmebahatika kusoma post hii mubadilike huu ukatili mnaoufanya si nzuri mnaotuumiza ni sisi ndugu zenu Watanzania wenzenu. Hebu kuweni na huruma sura zenu zifanane na nyoyo zenu. Kwanini mnakuwa na SURA ZA TWIGA LAKINI NYOYO ZA NYOKA?
Nenda na Bima yako nenda na pesa yako ya kulipia vyeti halali, Unajua wanachokifanya? Utapangiwa tarehe kila siku mpaka utoe yale malipo yasiyo na risiti ndo utapata huduma. Nawaombeni madaktari kama mmebahatika kusoma post hii mubadilike huu ukatili mnaoufanya si nzuri mnaotuumiza ni sisi ndugu zenu Watanzania wenzenu. Hebu kuweni na huruma sura zenu zifanane na nyoyo zenu. Kwanini mnakuwa na SURA ZA TWIGA LAKINI NYOYO ZA NYOKA?