Unaupimaje utendaji wa Waziri wa uchukuzi?

[MENTION]
mtotowamjini[/MENTION] katika huo ufuatiliaji wake wa jana mabehewa mangapi yamefufuliwa kama siyo kujitafutia umaarufu wa bwerere....hivi Mwakyembe anajua ni vipuri vipi vimepungua hata kulikamilisha behewa moja kama siyo ushambenga tu?

..Mkuu Ruta, Hoja yako ni Njema inayostahili majadiliano ya Great Thinkers lakini unapoiweka maneno ya 'Vidole Juu' ama ya 'Kimipasho mipasho' hivi kama niliyo-bold hapo juu Hoja inapoteza heshima yake na inaishia kuonekana ni chuki binafsi tu kwa Jamaa!
 
Sasa toa ushauri afanye nini? akae ofisini tu ili asiboe? Watanzania sijui tukoje jamani mtu akijaribu kufanya kazi tunamlaumu kwanini? kama wengine ni wazembe basi aangalie tu!kila kitu kibaya tu,Mtu akijaribu kujituma basi anatafuta Urais,akikaa kimya mtaema hafai kabisa amefanya nini nchi hii!Wengine ndiyo maana wamekata tamaa wameamua kushibisha matumbo yao maana sisi ni kulaumu kila kitu.Nchi hii inakatisha tamaa sana, kila mtu ana ajenda ya siri! Wapeni moyo watu wanao jitahidi kwa mazuri wanayofanya na mabaya wakosoeni lakini siyo kila kitu kibaya tu! sasa unataka waziri akae tu basi aangalie madudu napo utapiga kelele hawezi huyu mnafiki tu,basi onesha njia basi wewe!
mleta mada ni aidha muathirika wa fukuzafukuza ya Mwakyembe au yuko kambi ya EL inayomchukia mwakyembe kwa kila jambo.hivi yeye hajui kuwa nchi hii imeoza? akitokea mpenda nchi wa kiukweli si dhani kama kuna bodi yoyote itasalimika. ni madudu kwa kwenda mbele. VIVA MWAKYEMBE TUPO PAMOJA JUHUDI ZAKO TUNAZIONA.WATAKUBEZA LAKINI MWISHO WATACHOKA
 
Mimi binafsi naona anafanya kazi nzuri wabongo na serikali yetu inahitaji kuburuzwa kama mbwa mwitu maana vichwa vyetu vimeota kutu
 
kajembe usichojua bosi kulingana na sheria lazima awe mzambia na Mwakyembe hana ubavu wa kumwondoa.....sijui tangia lini wazambia wakawa ni ndugu zangu.................la muhimu hapa ni kuwa tutaendelea kukosoa hadi majambozi yatakapowekwa sawa ni haki yetu ya kikatiba...................aache kuingilia watendaji ambao wamewekwa kisheria na hata katibu mkuu wake hamshirikishi kama ni kasi ya kwenda Ikulu hatafika........

Kama Katibu wake Mkuu hamshirikishi basi lazima kutakuwa na kasoro kubwa na hao watendaji wa hiyo wizara kwani ikumbukwe kuwa ni Katibu Mkuu huyo huyo na watendaji wakuu hao hao waliomuhujumu waziri Nundu mpaka akaenguliwa.

Hivi sasa ni hao hao wanaomuhujumu Mwakyembe kwa kutokuviwezesha vikosi kazi anavyoviunda ili visifanye kazi stahiki.

Bila kuwabadilisha hawa watendaji wakuu kama Rais alivyoahidi alipobadilisha baraza la mawaziri, Mwakyembe atatwanga maji kwenye kinu muda wote wa uwaziri wake.
 
Kama Katibu wake Mkuu hamshirikishi basi lazima kutakuwa na kasoro kubwa na hao watendaji wa hiyo wizara kwani ikumbukwe kuwa ni Katibu Mkuu huyo huyo na watendaji wakuu hao hao waliomuhujumu waziri Nundu mpaka akaenguliwa.

Hivi sasa ni hao hao wanaomuhujumu Mwakyembe kwa kutokuviwezesha vikosi kazi anavyoviunda ili visifanye kazi stahiki.

Bila kuwabadilisha hawa watendaji wakuu kama Rais alivyoahidi alipobadilisha baraza la mawaziri, Mwakyembe atatwanga maji kwenye kinu muda wote wa uwaziri wake.

Big point............ Bulesi
 
Last edited by a moderator:
Mimi binafsi naona anafanya kazi nzuri wabongo na serikali yetu inahitaji kuburuzwa kama mbwa mwitu maana vichwa vyetu vimeota kutu
[MENTION]
Pakawa[/MENTION] na kichwa cha Mheshimiwa ndiyo hakina kutu?..................................."ukiona la kuvunda...................."...malizia mwenyewe.........."ujue halina ubani"
 
mleta mada ni aidha muathirika wa fukuzafukuza ya Mwakyembe au yuko kambi ya EL inayomchukia mwakyembe kwa kila jambo.hivi yeye hajui kuwa nchi hii imeoza? akitokea mpenda nchi wa kiukweli si dhani kama kuna bodi yoyote itasalimika. ni madudu kwa kwenda mbele. VIVA MWAKYEMBE TUPO PAMOJA JUHUDI ZAKO TUNAZIONA.WATAKUBEZA LAKINI MWISHO WATACHOKA

sanga malua hii kasi ya nguvu ya soda Mrema ndiye baba lao.............lakini leo ukimwuliza yeyote Mrema yuko wapi.........................hakuna ajuaye......................
 
Last edited by a moderator:
Uko sahihi kabisa ndugu yangu. Ziara ya ghafla haifanyiki kwa Waziri kwenda karakana peke yake bila uongozi uliopo kujua, mbaya zaidi kutishishia kumfukuza kiongozi mkuu wa sehemu hiyo akiwa hayupo. Sio sahihi kabisa hilo. Kama alitaka kufanya ziara ya angeamka akamuarifu Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mkuu siku hiyo hiyo kuwa yuko njiani kwenda kuwatembelea. TAZARA ni taasisi kubwa, sio rahisi kurekebisha jambo au mambo kwa spidi ili kumfurahisha Waziri. Ziara za ghafla zisitumike vibaya. Kama viongozi wakuu wa TAZARA wako makini, watakapokaa nae kikao watamsuta. Angekwenda nao ili awape maelekezo ya nini wafanye ili kuboresha utendaji wao. Pia asiongoze kwa vyombo vya habari, vinamwinua lakini ajue vyombo hivyohivyo vinaweza kumwangusha. amuulize Mrema

Mkuu nakubaliana nawe. Mwakyembe anatumia njia za kijima mno kuongoza Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi. Kwa ninavyo mfahamu boss wake,atakua alimteua na kumpa hiyo wizara kama mkakati wa kummaliza kisiasa. Amepwaya sana,amebakia kutapatapa kwa kutafuta huruma ya wananchi,aonekane anaangushwa na Watendaji wa chini yake. Nawaomba viongozi wa CDM ikitokea uchaguzi mkuu ujao mkachaguliwa kuongoza nchi hii,viongozi wa kukurupuka aina ya Mwakyembe hapana! Anzeni sasa kuwapa mafunzo ya uongozi makada wenu,ndani na nje ya nchi!
 
Daah! Watz bwana umbea tu! Hawakosi ya kusema ufanye mazuri au mabaya! Nadhani mtoa maada undatakiwa kudicrea interest kwanza,ww ni moja ya wahanga wa Dr,nikupe pole huyo mh atakufa na mtu sialishawaambia haogopi kufaa! Maana alisha onja mauti,kazikwenu msiojua radha ya mauti. DAWA CHAPAKAZI,SISI TUNAMKUBALI Dr mwaki.Bigup!
 
mtotowamjini kweli unaamini Mwakyembe akifuatilia atamaliza rushwa kwenye wizara yake kazi ambayo hata takukuru hawajui waanzie wapi?

If Mwakyembe wants to deliver in that ministry, he should make sure that he appoints knowledgeable people in boards as directors; he should also make sure that these directors are accountable for the performance of the institutions they lead.

Aachane na kufukuzana na daladala barabarani bali achague watu mahili afanye nao kazi; deliverance of results is what counts and not populism kama mkweree!!
 
Jamani mtajuaje mhe. yupo physically and mentally fit kwa kazi? mi najua huo si uongozi hata kidogo kila kitu anasemea kwenye vyombo vya habari anafukuza wafanyakazi kwenye runinga?

Mie nadhani lazima watu nao wajue haki zao, huwezi kuajiriwa ofisini kwa barua na kufukuzwa kwa mdomo kwenye runinga, huo ni uongozi wa kisiasa zaidi kuliko kitaaluma.
 
People want to see results which are delivered when responsible people work as a team!! Mwakyembe should mould his own team at the ministry headquarters, hiyo iliyopo sio yake na wala sio team ya ushindi bali ya kumuangusha; tokea juu hadi chini!!
 
Hiring on interview, firing on tv, tutafika tu, he might be sailing an empty boat while alone, siasa kweli ni sihasa.
 
Back
Top Bottom