Elections 2015 Unaunga mkono Lowassa kuhamia CHADEMA na kuwa mgombea Urais?

Unaunga mkono Lowassa kuhamia CHADEMA na Kugombea Urais?

  • NDIYO

    Votes: 318 59.8%
  • HAPANA

    Votes: 214 40.2%

  • Total voters
    532
  • Poll closed .
ccm pamoja na kubeba watu sijui,kutumia wasanii,ndio mbinu yao na miaka yote inawatoa.
hakuna mtu analazimishwa kwenda,,,ukiona nyomi ya magufuli mara nyingi ni wapiga kura serious,
nyomi ya lowasa ina mchanganyiko na wengine hawatampigia kura
Mbona wanaulizwa wanamtaka nani wanajibu Lowassa humo ndani ya mikutano yenu mbele ya Magufuli na kikwete au hauoni hizo video?
 
Hapana
je,utaunga mkono uamuzi wowote wa kumfanya lowassa awe mgombea uraisi kwa ticket ya chadema/ukawa endapo uamuzi huo utafikiwa?


Jibu ndio/hapana/sijui

kura hii inawahusu pro-ukawa wote na wengine wenye kuunga mkono umoja huu tu.
 
Sahihi kabisa

mtazamo unaoonekana na wengi wa wananchi ni kwamba haikuwa sahihi kwa lowasa kutoka kutaka kugombea kupitia ccm na ghafla kuangukia chadema na kuiwakilisha ukawa.

Wengi wamepata picha ya uchu wa madaraka badala ya nia ya dhati ya ukombozi.

Mtazamo wa wengi ni kua, kama lowasa angetaka kulinda heshima yake na kupeleka ushindi upinzani, nafasi hiyo ingebaki kwa dr. Slaa na yeye kuwa mhamasishaji mkuu.

Lakini kwa hali jinsi ilivyo sasa, kila mtu anapata wasi wasi wa lengo halisi la lowasa kuitaka ikulu na kupata woga. Ikulu kuna nini kupahangaikia hivyo, kila mtu anajiuliza.

Sio peke yangu lakini wengi wanaona hivyo, na hilo linaipa ushindi ccm.

Bila shaka, ccm wanapata tena nafasi ya kuongoza taifa.
 
Je,utaunga mkono uamuzi wowote wa kumfanya Lowassa awe mgombea uraisi kwa ticket ya CHADEMA/UKAWA endapo uamuzi huo utafikiwa?

Jibu Ndio/Hapana/Sijui

Kura hii inawahusu Pro-UKAWA wote na wengine wenye kuunga mkono umoja huu tu.

eddo the din
 
Mimi mwana CCM Kindakindaki naapa kuwa nitampigia kura Edward Ngoyai Lowassa anayeiwakilisha CHADEMA kupitia mwamvuli wa Muungano wa vyama vya UKAWA. Kama kunawakati ambapo CCM inahitaji kujipanga vyema na kurekebisha mapungufu yaliyopo wakati huo ndio sasa.Kwa yeyote anayeipenda CCM kama mimi,naomba kwa Moyo Mkunjufu tuiweke CCM pembeni ili ikajikague,ikajitafakari na kisha ijipange kwa ajili ya 2020 - 2025.Gari ama mashine yeyote ile hata iwe tingatinga ikiharibika sharti iwekwe pembeni ili ifanyiwe marekebisho.Ukiilazimisha iendelee na kazi ama iendelee na safari madhara yake ni makubwa sana kwa abiria,mazingira na hata watu waliokaribu na mashine hiyo!!Kataa vitisho,kataa kununuliwa kama bidhaa,kataa uchochezi,kataa michezo michafu ya Kisiasa...Jiandae kupiga kura yako kwa Diwani,Mbunge na Rais wa UKAWA.....MUNGU ibariki TANZANIA na watu wake wote!!
 
Back
Top Bottom