Unaujua ugonjwa wa Mafua ya Nyanya ulioanza kuivuruga tena dunia?

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,364
8,096
Wakati dunia ikiwa bado na makovu ya ugonjwa wa Covid_19 ulioishambulia na kuua watu milioni 6.4, na ule wa MonkeyPox ulioua karibu watu 100 Afrika mwaka huu, kumeibuka homa ya mafua ya nyanya.

Kumeripotiwa kuweko kwa visa vipya nchini India na kuanza kuibua hofu ya kuenea katika maeneo mengine duniani. Lakini unaufahamu ugonjwa huu vyema? kama dalili zake, madhara na tiba?
1662221909130.png

Umeanzia wapi?​


Homa ya Nyanya iligunduliwa kwa mara ya kwanza nchini India. Mnamo Mei 6, 2022, Wizara ya Afya ya India ilithibitisha kisa cha kwanza katika wilaya ya Kollam.

Kitivo cha Tiba cha Hospitali ya Ramathibodi kinatoa taarifa kuhusu homa ya nyanya kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Iligundua maambukizo kwa mtoto wa mwaka mmoja na kaka yake mwenye miaka 5 kutoka Uingereza, ambao wazazi wao waliwapeleka watoto hao kutembelea ndugu huko India na kukaa kwa mwezi mmoja. Lakini wiki moja baada ya kurudi kutoka Kerala mwezi uliopita, wakabainika kuwa na homa hiyo. May alikuwa na vipele kwenye mikono na miguu yake, kama homa ya mafua ya nyanya.

Wazazi wa watoto hao waliviambia vyombo va habari kwamba, waliona vipele na watoto wakishikwa homa, na kwamba wakiwa India walikuwa wakicheza na mtoto mmoja ambaye anaelezwa kuwa na ugonjwa huo.
Wataalam wanasema, dalili zote zinaonyesha ni homa ya mafua ya nyanya.

Hivi sasa, wanasayansi bado wanajaribu kujua sababu ya ugonjwa huo. Hata hivyo, nakala iliyochapishwa kupitia The Lancet, jarida kuhusu masuala ya tiba la Uingereza, inasema kwamba ugonjwa huo hauna uhusiano na virusi vya COVID-19 (SARS-CoV-2). Hata kama mgonjwa anaonyesha dalili zinazofanana.

Dalili za homa hii​

Watu walioambukizwa na homa ya nyanya wanakumbwa na malengelenge makubwa mekundu ya mfanano wa nyanya na vipele. Vikiguswa vinaleta maumivu. Dalili nyingine za ugonjwa huo ni uchovu, kichefuchefu, kutapika, kuhara, homa, maumivu ya viungo, na mwili kuumwa, sawa na dalili za kawaida za mafua.

Kundi gani lenye hatari zaidi ya kuambukizwa homa hii?​


Watoto walio chini ya umri wa miaka 5 wako katika hatari ya kuambukizwa kwa sababu virusi vinaweza kuenea haraka kwa kugusana kwa karibu, kama vile kugusa sehemu chafu au kinyesi cha watu walioambukizwa, au kula vitu vilivyo na virusi.

Hali ya janga la homa hii kwa sasa duniani​

Hadi sasa, kuna angalau kesi 100 za homa ya nyanya nchini India, ambapo 82 ni watoto chini ya umri wa miaka 5. Eneo lililo na mlipuko mkubwa zaidi ni Kerala, ikifuatiwa na Tamil Nadu.

Orissa na Haryana Wakati Wizara ya Afya ya India imethibitisha kuwa ugonjwa huo sio hatari kwa maisha. Na kwa sasa madaktari wanatiba dalili zake tu.

Mapema wiki hii ilitoa miongozo ya kuzuia, kupima na matibabu ya magonjwa kwa majimbo yote. Ikiwa mtu yeyote anashukiwa kuambukizwa, anawekwa karantini kwa siku 5-7 baada ya dalili, na wazazi pia wanahimizwa kuwa waangalifu haswa kwa kufuatilia dalili za watoto wao.
 
Yani siku hizi kakitokea kamlipuko kadogo tuu labda kanakosababishwa na local environment na hali ya hewa tuu, tena kamlipuko kenyewe huenda ni self limiting, lakini wajuba wanataka wakape promo mpaka dunia nzima tuwe juu juu?
 
Hatari na inasikitisha sana...

Huo ugonjwa ungeanzia Africa sasa hivi lockdown zingetangazwa dunia nzima...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom