Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 26,008
- 68,154
Habari zenu wakuu, herini kwa sikukuu pendwa za mwisho wa mwaka. Tukiwa tunaelekea ukingoni mwa mwaka 2021 kwanza tumshukuru Mungu kwa zawadi ya huu mwaka na uhai hadi sasa tukiwa na imani ya kuuona mwaka mpya 2022.
2021 umekuwa na mambo mengi mazuri na mabaya, inawezekana kwa wengine ni mwaka wenye nuru, furaha, amani na mafanikio tofauti kabisa na miaka mingine iliyopita.
2021 kwangu ni tofauti kabisa ni mwaka ambao umekuwa mgumu sana kwangu sijapiga hatua kurudi nyuma lakini nmekutana na ya kuniumiza, kunikatisha tamaa lakini yote yameniachia somo kwenye maisha.
Nilipata ajali nkatumia akiba yote kujiuguza namshukuru Mungu kwa sasa nipo vyema japo ilikuwa ni mateso(nilipotea hadi humu jf for months) Ndani ya hiki kipindi niliachwa na mpenzi wangu baada ya kujua nimepata ajali alinitafuta na kunijulia hali na kuniahid atakuja jioni kunijulia hali lakini ndio mpaka kesho hakuwahi kuja wala kuulizia hali yangu na sijawahi kumtafuta tena. Sasa nipo singo nainjoiii
Rafiki wa kweli yupo? Ni nani? Rafiki wa kweli ni pesa huyu ndie anaekujali kwa kukutimizia mahitaji yako on time. Marafiki wanafki sana nmegundua hili ndani ya mwaka huu. Ndugu ndio kabisa kikubwa ni kuwafumbia macho na kuziba masikio ili usiyape mda wako.
Mambo ya familia ndani ya huu mwaka ndio pasua kichwa sipendi kabisa kuyaongelea nayo yamechangia kwa % kubwa mwaka kuwa mgumu kwangu. Kuna mda nawaza nisijali chochote lakini nna moyo wa kujali najikuta tu najali bila kujua madhara yake, hii kitu inamaliza furaha wakuu. Migogoro+misiba.
Kiuchumi kila nachokifanya ili kujiweka vizuri kinasua sua mambo yakianza kuwa sawa yanatokea matatzo yanafyeka akiba yote na mambo yanaanza kuvurugika.
Huu mwaka na uishe tu hapa imenipiga homa ya december ndio nafungia nayo mwaka, natumaini 2022 utakuwa mwaka wenye uafadhali kwenye mengi.
Pole kwa wale waliokutana na magumu ndani ya huu mwaka ni sehemu ya maisha kikubwa ni kutokukata tamaa kamwe.
Karibu sana mwaka 2022, ukawe mwaka wenye baraka na mafanikio kwa kila mmoja wetu.
2021 umekuwa na mambo mengi mazuri na mabaya, inawezekana kwa wengine ni mwaka wenye nuru, furaha, amani na mafanikio tofauti kabisa na miaka mingine iliyopita.
2021 kwangu ni tofauti kabisa ni mwaka ambao umekuwa mgumu sana kwangu sijapiga hatua kurudi nyuma lakini nmekutana na ya kuniumiza, kunikatisha tamaa lakini yote yameniachia somo kwenye maisha.
Nilipata ajali nkatumia akiba yote kujiuguza namshukuru Mungu kwa sasa nipo vyema japo ilikuwa ni mateso(nilipotea hadi humu jf for months) Ndani ya hiki kipindi niliachwa na mpenzi wangu baada ya kujua nimepata ajali alinitafuta na kunijulia hali na kuniahid atakuja jioni kunijulia hali lakini ndio mpaka kesho hakuwahi kuja wala kuulizia hali yangu na sijawahi kumtafuta tena. Sasa nipo singo nainjoiii
Rafiki wa kweli yupo? Ni nani? Rafiki wa kweli ni pesa huyu ndie anaekujali kwa kukutimizia mahitaji yako on time. Marafiki wanafki sana nmegundua hili ndani ya mwaka huu. Ndugu ndio kabisa kikubwa ni kuwafumbia macho na kuziba masikio ili usiyape mda wako.
Mambo ya familia ndani ya huu mwaka ndio pasua kichwa sipendi kabisa kuyaongelea nayo yamechangia kwa % kubwa mwaka kuwa mgumu kwangu. Kuna mda nawaza nisijali chochote lakini nna moyo wa kujali najikuta tu najali bila kujua madhara yake, hii kitu inamaliza furaha wakuu. Migogoro+misiba.
Kiuchumi kila nachokifanya ili kujiweka vizuri kinasua sua mambo yakianza kuwa sawa yanatokea matatzo yanafyeka akiba yote na mambo yanaanza kuvurugika.
Huu mwaka na uishe tu hapa imenipiga homa ya december ndio nafungia nayo mwaka, natumaini 2022 utakuwa mwaka wenye uafadhali kwenye mengi.
Pole kwa wale waliokutana na magumu ndani ya huu mwaka ni sehemu ya maisha kikubwa ni kutokukata tamaa kamwe.
Karibu sana mwaka 2022, ukawe mwaka wenye baraka na mafanikio kwa kila mmoja wetu.