Unataka kuwa mwanamziki Tanzania na ufanikiwe?

Lyamber

JF-Expert Member
Jul 24, 2012
11,716
18,753
Je unapenda kuwa mwanamziki Tanzania timiza ndoto yako?

Habari za Jioni waungwana,

Baada ya utafiti usio rasmi kwa hapa Tanzania, hasa hasa jiji la Dar es salaam, kuna vijana wengi sana wakike kwa wakiume wanavipaji vya kuimba, au tuseme wanajua sana kuimba na wanaonekana wanaweza kufika mbali sana vijana hawa wengi wao ni kuanzia miaka 16 na kuendelea, sema kinachowakawamisha sana sana ni support ili waweze kufikia malengo yao.

Ushauri wa bure ni kwamba wengi wao wa watanzania hawa huamua kufanya muziki baada ya either kushindwa kunafikiwa katika mambo mengine mfano,kushindwa kusoma shule au kukosa shughuli yoyote ile ya kufanya

Ili uweze kua msanii wa tofauti mwenye kujitambua na kuweza kufanikisha malengo yako ni lazima ujue kwamba kwa muziki wa sasa hivi kila kitu ni pesa hauwezi kua unalia lia kila siku kwamba unaweza kumba lakini haujapata chance ya kutoka, kutoka kwa mziki wa Tanzania ni juhudi zako mwenyewe tu unazoziweka mfano iliutengeneze audio production inakupaswa uwe na angalau 30,000-100,000 ili production yako iwe nzuri hapo namaanisha kurecord wimbo studio kama hauna management yani unafanya vitu kwa uwezo wako mwenyewe,

Inakupasa pia uwe na hela za kupost wimbo wako kwenye blog tofauti tofauti ili watu waweze kuusikiliza na kuudonload wimbo wako hapo gharama ni kuanzia 20,000-100,000 pia inakupasa uwe active ili uweze kua unapost sehemu nyingi nying huo wimbo wako ili upate downloads zako vizuri, blogs zipo nyingi sana za miziki kwa Tanzania

Video production inakupasa uwe na angalau 200,000 – na kuendelea za kumlipa huyo atakae enda kukutengenezea kazi yako hio 200,000 hapo namaanisha location mtakazo chukua zitakua ni za bure i.e beach, restaurant ya kitaani, nyumba ya mshkaji wako, gari la kuazima etc etc, baada ya hapo itakupasa uitume nyimbo hio kwenye blogs tofauti tofauti, video queen wa kuazima etc etc ili watu waweze kuioa na kuitambua. Kwaio ka kifui gharama za kuweza kufanikisha ndoto zako hapo si chini ya 400,000 kwa haraka haraka, kwaio wengi wao hawana vipato vyovyote ni kazi tu ya kulia lia waweze kufanyiwa vitu bure kitu ambacho kinawakwamisha ni hizo nisaidie nisaidie ambazo kimsingi hazimfikishi mtu popote pale

Ufanyaje ili uwe tofauti

Kama hauna management yoyote ile anza kutafuta shughuli yoyote ile ya kufanya ili ikuingizie kipato i.e kuuza maji, juice, kufanya kazi za vibarua etc ili uweze kufikia gharama tajwa hapo juu, baada ya kufanikisha hayo jitahidi uweze kua unajichanganya changanya kwenye matamasha mfano East Africa radio, Coca cola, E-fm, Times fm, omba uimbe hata bure angalau ujulikane watu wajue kuna mtu anaitwa fulani, kati ya watu 200 watatokezea hata 30 watakaopenda either wimbo wako au kitu kama hicho weka bidii katika kutafuta hela ufikie unachokitaka kama unaona hiyo haiwezekani au ni ngumu ushauri wa bure ni achana na ndoto za kuwa mwanamuziki maana utapata shida sana studio wanataka hela, redio station wanataka hela, video production wanataka hela, blogs nao wanataka hela.
 
Umewaambia kila kitu hukuwaficha ni juu yao kuyachukua au kuyapotezea
 
Back
Top Bottom