BRO LEE
JF-Expert Member
- Dec 25, 2011
- 826
- 600
😂 😂 😂 😂Ndio maana nina kisimu changu cha tochi kwaajili ya kuchezea faulo huko, hakina V.A.R. Akija shemeji yenu nakificha ndani ya viatu au bafuni.
Juzi alikuja halafu nikaingia bafuni kuchat na pisi moja hivi mpya, nimeisave "Covid-19 Pro" yeye nimemsave "WUHAN-VIRUS", si nikajisahau nusu saa ikapita nipo bafuni tu, akaja kunigongea mlango kama tumevamiwa na majambazi au kama ananidai vile, kidogo anitoe roho mpaka simu nusu idondoke kwenye ndoo ya maji kwa jinsi mlango ulivyo bamizwa.
Akaniuliza kwa kufoka "Wewe mwanaume unaingia bafuni saa zima, unaosha nini huko"!!!. Nikamjibu kwa upole "VYOMBO".
Nikazuga naoga zangu, fasta nikatoka, namtafuta kumbe mtu alishasepa muda kweli, nakutana na sms "Asante kwa kuni save Wuhan-Virus". Nikajua simu yangu ya tachi imeshapigwa inspection ya kufa mtu na kibarua kishaota nyasi nshaachika, wala sikumtafuta tena mpaka leo.