Unashangilia mwaka mpya unashangilia kulisogelea kaburi

mdundo ngoma sana

JF-Expert Member
Jan 2, 2016
1,002
954
Pole mwanadamu na hongera pia,unapoingia mwaka mpya na kaburi nalo linasogea karibu yako,watu wema wanalia na kutubia dhambi zao,mnaoipenda dunia mpo kwenye bar na kumbi xa starehe,enyi watu hakika maisha ya dunia ni mafupi na sio ya kudumu.JIANDAE NA MAISHA YA AKHERA KUMBUKA ARDHI IMEWAMEZA WAJANJA NA WAJUAJI KULIKO WEWE
 
Pole mwanadamu na hongera pia,unapoingia mwaka mpya na kaburi nalo linasogea karibu yako,watu wema wanalia na kutubia dhambi zao,mnaoipenda dunia mpo kwenye bar na kumbi xa starehe,enyi watu hakika maisha ya dunia ni mafupi na sio ya kudumu.JIANDAE NA MAISHA YA AKHERA KUMBUKA ARDHI IMEWAMEZA WAJANJA NA WAJUAJI KULIKO WEWE
Masha Allah,... Ujumbe mzuri sana,mwenye kusikia amesikia na mwenye kuelewa pia nae kaelewa.
 
Majira na nyakati zimewekwa ili kuwakumbusha wanadamu kuwa hakuna jambo lidumuo. Sekunde inaisha na dakika kuanza, saa, siku, juma, mwezi na hata mwaka. Kila uanzapo mwaka kumbuka umepewa nafasi ya kuanza upya. Mwaka mpya unakuwa hauna maana kama umekusudia kuendelea kuishi vile vile ulivyokuwa ukiishi mwaka jana. Kukaribia kufa siyo sababu ya kutoshangilia. Maana wako wengi walio tamani kuendelea kuishi lakini hawakuweza kuwepo. Kushangilia ni ishara ya kushukuru kwa upendeleo uliopewa wa kuishi tena ili tuzirekebishe njia zetu za kumcha Mungu na hata za mafanikio ya kimwili. Hata usiposhangilia utakufa tu.
 
Kila aliyezaliwa na mwanamke sharti afe, ushangilie usishangilie kufa kupo palepale, ila kuna kila sababu ya kumshukuru Mungu maana wapo waliokufa punde tu baada ya kuzaliwa, na wengine wanateseka na maradhi hospitalini na hata hawajui mwaka umeisha maana hauna maana kwao kwa maumivu waliyonayo! Mshukuru Mungu kwa sadaka kwa kwa wahitaji.
 
Kufariki ni matokeo hauwezi kuacha kusherehekea au kufurahia kitu kisa utaja fariki...only weak people have that perception...
 
Hata usipo shangilia utakufa tu lazima ufurahi koz wapo watu walitamani kuingia mwaka mpya but hawakuweza ni vizuri kuonyesha furaha yako kwa Mungu na kuzidi mumuomba
 
wenzio wakisherehekea tu we hua unaharibu kama ulivyopata ziro form four
 
Ndugu hutakiwi kukiogopa kifo, sababu kimepangwa, kumbuka kuhesabu miaka ni kama kuweka kumbukumbu tu. kwa maana hiyo basi kifo kipo pale pale kuwe na mwaka mpya au kusiwe, na furaha ya mtu huwezi ihoji wewe kila mtu ana malengo yake muhimu kuliko kifo unachofikilia wewe.
 
Ndugu hutakiwi kukiogopa kifo, sababu kimepangwa, kumbuka kuhesabu miaka ni kama kuweka kumbukumbu tu. kwa maana hiyo basi kifo kipo pale pale kuwe na mwaka mpya au kusiwe, na furaha ya mtu huwezi ihoji wewe kila mtu ana malengo yake muhimu kuliko kifo unachofikilia wewe.
Malengo muhimu kuliko "kifo* yako kaburini sio hapa duniani
 
Fanyakazi hapa duniani kama haufi na mtumikieni Mungu kwa sala na sadaka kama unakufa Leo. Acha ujinga mtoa mada acha watu wafurahi. Utakuwa mwisilamu wewe tena mwanamke maana ninyi ndo mafundamentalist
 
wenzio wakisherehekea tu we hua unaharibu kama ulivyopata ziro form four
Jabyz unanifataga fataga wewet
" class="bbImage lazyload" data-zoom-target="1" style="" alt="" title="" width="" height="" />
 
Jabyz unanifataga fataga wewet
" class="bbImage lazyload" data-zoom-target="1" style="" alt="" title="" width="" height="" />
hahahahaha heri ya mwaka mpya mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom