Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
Habari za hapa wanajamvi?
Leo napenda tujadili kitu tofauti kidogo na mazoea yetu. Nacho ni hisia na maisha kwa ujumla bila ya wazazi.
Umeshawahi kujiuliza ikatokea leo wazazi wako wakachukukiwa na BwANA kwenda kwenye makao ya kudumu?
Kwa wale waliopatwa na hali hiyo nadhani wana picha hali jinsi inavyokuwa. Lakini nalo nadhani inategemea unaachwa na wazazi ktk umri gani.
Hebu fikiria unafiwa na mzazi mmoja wapo ukiwa labla shule au chuo ni tofauti na yule aliyefiwa na mzazi wake wakati akiwa mtu mzima ana kazi yake na maisha yake.
Hebu fikiria ukaondokewa na baba yako mzazi aliyekuwa anakupenda sana hadi wewe mwenyewe ukajua unapendwa. Unabaki na mama ambaye sasa ni mjane na siku moja anakuomba pesa (na sio kawaida yake kukuomba pesa) na wewe ukawa huna pesa hizo kwa wakati huo utajisikiaje?
Kwangu mimi huwa nafikiri kuishi pasipo na mzazi mmoja au wote ni kama kujitenga na dunia vile. Japo sasa ni mtu mzima na familia yangu lakini naweza kuamka usingizini usiku sana na nikakumbuka kuwa sina baba ameshatangulia kwenye makao ya milele huwa natokwa na machozi na siwezi tena kulala.
Hebu tujadili kwa pamoja nini kifanyike ili mtu upate furaha ya kudumu japo huna wazazi.
Kwani huwa ni furaha ya muda tu mfano mimi nikikumbuka tu nakosa raha hata nikiwa eneo gani japo tangu nimeondokewa na mpendwa wangu miaka 6 iliyopita.
Karibuni.
Leo napenda tujadili kitu tofauti kidogo na mazoea yetu. Nacho ni hisia na maisha kwa ujumla bila ya wazazi.
Umeshawahi kujiuliza ikatokea leo wazazi wako wakachukukiwa na BwANA kwenda kwenye makao ya kudumu?
Kwa wale waliopatwa na hali hiyo nadhani wana picha hali jinsi inavyokuwa. Lakini nalo nadhani inategemea unaachwa na wazazi ktk umri gani.
Hebu fikiria unafiwa na mzazi mmoja wapo ukiwa labla shule au chuo ni tofauti na yule aliyefiwa na mzazi wake wakati akiwa mtu mzima ana kazi yake na maisha yake.
Hebu fikiria ukaondokewa na baba yako mzazi aliyekuwa anakupenda sana hadi wewe mwenyewe ukajua unapendwa. Unabaki na mama ambaye sasa ni mjane na siku moja anakuomba pesa (na sio kawaida yake kukuomba pesa) na wewe ukawa huna pesa hizo kwa wakati huo utajisikiaje?
Kwangu mimi huwa nafikiri kuishi pasipo na mzazi mmoja au wote ni kama kujitenga na dunia vile. Japo sasa ni mtu mzima na familia yangu lakini naweza kuamka usingizini usiku sana na nikakumbuka kuwa sina baba ameshatangulia kwenye makao ya milele huwa natokwa na machozi na siwezi tena kulala.
Hebu tujadili kwa pamoja nini kifanyike ili mtu upate furaha ya kudumu japo huna wazazi.
Kwani huwa ni furaha ya muda tu mfano mimi nikikumbuka tu nakosa raha hata nikiwa eneo gani japo tangu nimeondokewa na mpendwa wangu miaka 6 iliyopita.
Karibuni.