Unapoondokewa (kufiwa) na wazazi wako

Mcheza Karate

JF-Expert Member
Jun 30, 2011
690
350
Habari za hapa wanajamvi?

Leo napenda tujadili kitu tofauti kidogo na mazoea yetu. Nacho ni hisia na maisha kwa ujumla bila ya wazazi.

Umeshawahi kujiuliza ikatokea leo wazazi wako wakachukukiwa na BwANA kwenda kwenye makao ya kudumu?

Kwa wale waliopatwa na hali hiyo nadhani wana picha hali jinsi inavyokuwa. Lakini nalo nadhani inategemea unaachwa na wazazi ktk umri gani.

Hebu fikiria unafiwa na mzazi mmoja wapo ukiwa labla shule au chuo ni tofauti na yule aliyefiwa na mzazi wake wakati akiwa mtu mzima ana kazi yake na maisha yake.

Hebu fikiria ukaondokewa na baba yako mzazi aliyekuwa anakupenda sana hadi wewe mwenyewe ukajua unapendwa. Unabaki na mama ambaye sasa ni mjane na siku moja anakuomba pesa (na sio kawaida yake kukuomba pesa) na wewe ukawa huna pesa hizo kwa wakati huo utajisikiaje?

Kwangu mimi huwa nafikiri kuishi pasipo na mzazi mmoja au wote ni kama kujitenga na dunia vile. Japo sasa ni mtu mzima na familia yangu lakini naweza kuamka usingizini usiku sana na nikakumbuka kuwa sina baba ameshatangulia kwenye makao ya milele huwa natokwa na machozi na siwezi tena kulala.


Hebu tujadili kwa pamoja nini kifanyike ili mtu upate furaha ya kudumu japo huna wazazi.

Kwani huwa ni furaha ya muda tu mfano mimi nikikumbuka tu nakosa raha hata nikiwa eneo gani japo tangu nimeondokewa na mpendwa wangu miaka 6 iliyopita.

Karibuni.
 
Kuna mzee mmoja aliwahi kuniambia kwamba uchungu wa kufiwa na mzazi au wazazi anaujua yule aliyefiwa..
Kisha akaniambia kwamba kama una rafiki aliyefiwa na mzazi au wazazi halafu itokee ukamweleza kuwa unauguliwa na mzazi wako, usidhani atakusikitikia sana....

"Si afe tu ili tufanane" anaweza hata kuwaza hivyo......

Sina uhakika kama maneno ya huyo mzee ambaye ameshatangulia mbele ya haki yana ukweli.

Lakini ninachotaka kusema hapa ni kwamba ni wale tu waliofiwa na wazazi ndio wanaojua uchungu wa kufiwa lakini yule ambaye wazazi wake wote wapo hai hawezi kujua uchungu wa kufiwa.................
 
cha kufanyika ili kupata furaha ni ku let it go, adhere to the fact that kila mtu ataonja kifo, it's the destiny, pole sana
 
Kuna mzee mmoja aliwahi kuniambia kwamba uchungu wa kufiwa na mzazi au wazazi anaujua yule aliyefiwa..
Kisha akaniambia kwamba kama una rafiki aliyefiwa na mzazi au wazazi halafu itokee ukamweleza kuwa unauguliwa na mzazi wako, usidhani atakusikitikia sana....

"Si afe tu ili tufanane" anaweza hata kuwaza hivyo......

Sina uhakika kama maneno ya huyo mzee ambaye ameshatangulia mbele ya haki yana ukweli.

Lakini ninachotaka kusema hapa ni kwamba ni wale tu waliofiwa na wazazi ndio wanaojua uchungu wa kufiwa lakini yule ambaye wazazi wake wote wapo hai hawezi kujua uchungu wa kufiwa.................

Mchambuzi, ukifiwa na wazazi unakuwa kama umepooza. Unajua, toka wazazi wangu wafriki huwa hata sisikii uchungu sana mtu akifiwa na wazazi wake. Nachukulia kawaida lakini si kwa minajili kuwa tufanane, la hasha, bali ni kuwa unakuwa hujielewi!
 
Hapa hakuna forumula aisee

Inategemea na connection uliyokuwa nayo wewe na mzazi
Si wote wanapitiwa kipindi kigumu kiasi hicho.

Nakumbuka miaka ya zamani kule kijijini kwetu
Kuna familia ya jirani baba yao alifariki, na hapo first born alikuwa ndio kamaliza la saba na hajafaulu na hajaolewa
Wengine walikuwa shule za msingi na wengine hata sule hawajaanza, hapo naongelea familia ya watoto kama 9.
Halafu mama hakuwa na kazi, ni mama wa nyumbani na alikuwa anafuga kuku wa kienyeji na kuuza, na alikuwa na bustani ya mchicha.

Lakini unajua nini kilitokea? Baada ya baba tu kufariki, familia ilikuwa ya furaha na ushirikiano, pesa ndogo ila wana amani na wamenawiri kweli. Hadi mtaani tukawa tunawatania 'msiba umewakubali'

Maumivu yanatofautiana kulingana na ukaribu wa mzazi husika.

Kwa wale walio karibu na wazazi wao, ni pigo.
Cha kufanya ni kujaribu kuomba kama ni muumini, assume kuwa ameenda kuliko kuzuri kuliko dunia hii
Pia waweza concentrate na walio hai, hasa mjane aliyeachwa anahitaji upendo zaidi ili aweze ku-move on
Hujapoteza maana bado una familia yako, mke na watoto labda.

Kama ni mkatoliki kuna misa za kuombea marehemu, huwa zinaleta amani hivi maana unaamini umemtendea jema huko aliko.
 
Kuna mzee mmoja aliwahi kuniambia kwamba uchungu wa kufiwa na mzazi au wazazi anaujua yule aliyefiwa..
Kisha akaniambia kwamba kama una rafiki aliyefiwa na mzazi au wazazi halafu itokee ukamweleza kuwa unauguliwa na mzazi wako, usidhani atakusikitikia sana....

"Si afe tu ili tufanane" anaweza hata kuwaza hivyo......

Sina uhakika kama maneno ya huyo mzee ambaye ameshatangulia mbele ya haki yana ukweli.

Lakini ninachotaka kusema hapa ni kwamba ni wale tu waliofiwa na wazazi ndio wanaojua uchungu wa kufiwa lakini yule ambaye wazazi wake wote wapo hai hawezi kujua uchungu wa kufiwa.................

kaka MTAMBUZI, Ni kweli kwa maneno ya mzee kwani sasa nikiambiwa na mtu kuwa amefiwa na mzazi wake huwa naona kawaida sana sio kama ili tufanane bali kuna kitu cha kiroho kipo katikati yake.
 
Habari za hapa wanajamvi?

Leo napenda tujadili kitu tofauti kidogo na mazoea yetu. Nacho ni hisia na maisha kwa ujumla bila ya wazazi.

Umeshawahi kujiuliza ikatokea leo wazazi wako wakachukukiwa na BwANA kwenda kwenye makao ya kudumu?

Kwa wale waliopatwa na hali hiyo nadhani wana picha hali jinsi inavyokuwa. Lakini nalo nadhani inategemea unaachwa na wazazi ktk umri gani.

Hebu fikiria unafiwa na mzazi mmoja wapo ukiwa labla shule au chuo ni tofauti na yule aliyefiwa na mzazi wake wakati akiwa mtu mzima ana kazi yake na maisha yake.

Hebu fikiria ukaondokewa na baba yako mzazi aliyekuwa anakupenda sana hadi wewe mwenyewe ukajua unapendwa. Unabaki na mama ambaye sasa ni mjane na siku moja anakuomba pesa(na sio kawaida yake kukuomba pesa) na wewe ukawa huna pesa hizo kwa wakati huo utajisikiaje?

Kwangu mimi huwa nafikiri kuishi pasipo na mzazi mmoja au wote ni kama kujitenga na dunia vile. Japo sasa ni mtu mzima na familia yangu lakini naweza kuamka usingizini usiku sana na nikakumbuka kuwa sina baba ameshatangulia kwenye makao ya milele huwa natokwa na machozi na siwezi tena kulala.


Hebu tujadili kwa pamoja nini kifanyike ili mtu upate furaha ya kudumu japo huna wazazi.

Kwani huwa ni furaha ya muda tu mfano mimi nikikumbuka tu nakosa raha hata nikiwa eneo gani japo tangu nimeondokewa na mpendwa wangu miaka 6 iliyopita.

Karibuni.

well 4 me, kuondokewa na mzazi au wazazi hasa toka umri mdogo nachukulia kama hali isiyoweza kuzoeleka maisha yote sana sana tunasahau kwa muda then tunakumbuka. whether u hv money or ur poor, thamani ya mzazi inabaki palepale.
kwa upande wangu mimi, nilipoteza wazazi wangu nikiwa na umri mdogo. sikuwa na matatizo ya kiuchumi saaaana mpaka kujikuta namkumbuka mama au baba just 4 money, no but daima niliwakumbuka na ninaendelea kuwakumbuka sababu kuwakosa wao duniani ni sawa na kukosa miungu inayoonekana.
Hata watu wazima waliopoteza wazazi katika umri mkubwa, still wana suffer a lot bt tofaut ni kuwa mdogo anahitaji kuwa karibu sana na wazazi wakati mkubwa anauwezo wa kumake his/her own decisions. so this makes mtoto mdogo aliyepoteza wazazi kutoweza kuficha hisia zake mbele za watu wyl mkubwa ana uwezo wa kuficha hisia bt wote wana maumivu makubwa ndani ya mioyo yao.
 
Duh!..
Yaani mm leo tu asubuhi nimetoa machozi kumkumbuka mzee father pia huwa zikikaribia tarehe hz alizofariki huwa ninajikuta namkumbuka sana.
Lakini mm huwa ctamani wengine wapitie uzoefu huu hata kdg na huwa hata rafiki yangu akifiwa na mtu km huyu huwa ninakosa ujasiri wa kumnyamazisha kwasababu huwa ninahisi jinsi anavyojisikia huwa nami ninaishia kutoa machozi!..
 
I lost him, I was too young to see the difference! (its sad I can't really recall anything of him)
I lost her, I was old enough....old enough to live with the grieve all the time....the pain won't go away in totality it is past a decade since she left us!
 
hii thread IMENILIZA, NA WOTE MLIOCHANGIA! i have both parents though my mama is seriously sick huu ni mwaka wa 3! hawezi kuongea anaongea kw ishara na akihuzunika au kama kuna kitu kinamuuma hulia! my dad is ONE in a million man! kila anapokwenda huenda na mama, kabla ya kwenda kazini anahakikisha mum kapewa dawa, chakula etc, labda tu niseme kuwa hata kula mum hali kwa mdomo ana mwaka wa tatu pia, amewekewa tube TUMBONI, SO KILA KITU KINAPITA KWA TUBE!

NIMESHALIA SANA, NIMESHAKUWA SUGU, NAMUOMBEA UJASIRI WA KUVUMILIA YOTE NAIOMBEA PIA FAMILIA YANGU TUSHIKAMANE KATIKA KIPINDI HIKI CHA KUMUUGUZA MAMA MPAKA HAPO MUNGU ITAKAPOMPENDEZA KUMPONYA KABISA!

SIJUI NI KWA NINI, ILA NINA IMANI KUBWAAAAAAA KUWA ATAPONA KABISA! ATAKUJA KUONGEA NA KUWA MZIMA TENA!! poleni wapendwa wote mliopoteza wazazi,. HAKIKA INAUMA SANA, I CAN IMAGINE WHAT U HAVE BEEN THROUGH!! MUNGU WETU AWAPE FARAJA, ATUPE NA SISI MAISHA MAREFU, ILI tuweze kuwalea watoto wetu mpaka wawe wakubwaaaaaaa, na wajukuu TUWAONE! amen!
 
Kuna mzee mmoja aliwahi kuniambia kwamba uchungu wa kufiwa na mzazi au wazazi anaujua yule aliyefiwa..
Kisha akaniambia kwamba kama una rafiki aliyefiwa na mzazi au wazazi halafu itokee ukamweleza kuwa unauguliwa na mzazi wako, usidhani atakusikitikia sana....

"Si afe tu ili tufanane" anaweza hata kuwaza hivyo......

Sina uhakika kama maneno ya huyo mzee ambaye ameshatangulia mbele ya haki yana ukweli.

Lakini ninachotaka kusema hapa ni kwamba ni wale tu waliofiwa na wazazi ndio wanaojua uchungu wa kufiwa lakini yule ambaye wazazi wake wote wapo hai hawezi kujua uchungu wa kufiwa.................
mimi nilifiwa na baba yangu nikiwa mtu mzima hivi, nimeolewa na nina watoto....... uchungu niliousikia sitataka mtu yeyote aupate, let alone my friend.....
juzi kati kuna my best friend alikuwa anauguliwa na mamake, literary nilikuwa nashinda hospitali, yaani siwezi hata kutoka, usiku nakumbushwa na mgonjwa "sasa rudi home". yaani nilikuwa natamani niwe na power ya uponyaji ili nimponye yule mama. namshukuru Mungu alikuja kupona........
 
hii thread IMENILIZA, NA WOTE MLIOCHANGIA! i have both parents though my mama is seriously sick huu ni mwaka wa 3! hawezi kuongea anaongea kw ishara na akihuzunika au kama kuna kitu kinamuuma hulia! my dad is ONE in a million man! kila anapokwenda huenda na mama, kabla ya kwenda kazini anahakikisha mum kapewa dawa, chakula etc, labda tu niseme kuwa hata kula mum hali kwa mdomo ana mwaka wa tatu pia, amewekewa tube TUMBONI, SO KILA KITU KINAPITA KWA TUBE!

NIMESHALIA SANA, NIMESHAKUWA SUGU, NAMUOMBEA UJASIRI WA KUVUMILIA YOTE NAIOMBEA PIA FAMILIA YANGU TUSHIKAMANE KATIKA KIPINDI HIKI CHA KUMUUGUZA MAMA MPAKA HAPO MUNGU ITAKAPOMPENDEZA KUMPONYA KABISA!

SIJUI NI KWA NINI, ILA NINA IMANI KUBWAAAAAAA KUWA ATAPONA KABISA! ATAKUJA KUONGEA NA KUWA MZIMA TENA!! poleni wapendwa wote mliopoteza wazazi,. HAKIKA INAUMA SANA, I CAN IMAGINE WHAT U HAVE BEEN THROUGH!! MUNGU WETU AWAPE FARAJA, ATUPE NA SISI MAISHA MAREFU, ILI tuweze kuwalea watoto wetu mpaka wawe wakubwaaaaaaa, na wajukuu TUWAONE! amen!

mchana huu umeniliza tena. Nimelia sana baada ya kukumbuka nami pia baba aliumwa kwa miaka 4 then akatangulia so nakumbuka magumu unayopitia. Kwa kweli kuna roho inakuja inakupa amani kuwa yataisha tu na atapona kumbe sio. Unakuwa una nature ya kifo. Kwani hata mgonjwa anapojiwa na roho ya mauti huwa anakataa kuwa atakufa. Umewahi kujiuliza kwa nini mgonjwa siku anakufa huwa anaonyesha ahueni then anafariki? Hayo ni mambo ya ulimwengu wa roho.
 
cha kufanyika ili kupata furaha ni ku let it go, adhere to the fact that kila mtu ataonja kifo, it's the destiny, pole sana

sio rahisi mkuu,binafsi inaniumiza sana,mara nyingi nalia tu na kumshukuru mungu kwa yote.nimefiwa na baba nikiwa form two.
 
hii thread IMENILIZA, NA WOTE MLIOCHANGIA! i have both parents though my mama is seriously sick huu ni mwaka wa 3! hawezi kuongea anaongea kw ishara na akihuzunika au kama kuna kitu kinamuuma hulia! my dad is ONE in a million man! kila anapokwenda huenda na mama, kabla ya kwenda kazini anahakikisha mum kapewa dawa, chakula etc, labda tu niseme kuwa hata kula mum hali kwa mdomo ana mwaka wa tatu pia, amewekewa tube TUMBONI, SO KILA KITU KINAPITA KWA TUBE!

NIMESHALIA SANA, NIMESHAKUWA SUGU, NAMUOMBEA UJASIRI WA KUVUMILIA YOTE NAIOMBEA PIA FAMILIA YANGU TUSHIKAMANE KATIKA KIPINDI HIKI CHA KUMUUGUZA MAMA MPAKA HAPO MUNGU ITAKAPOMPENDEZA KUMPONYA KABISA!

SIJUI NI KWA NINI, ILA NINA IMANI KUBWAAAAAAA KUWA ATAPONA KABISA! ATAKUJA KUONGEA NA KUWA MZIMA TENA!! poleni wapendwa wote mliopoteza wazazi,. HAKIKA INAUMA SANA, I CAN IMAGINE WHAT U HAVE BEEN THROUGH!! MUNGU WETU AWAPE FARAJA, ATUPE NA SISI MAISHA MAREFU, ILI tuweze kuwalea watoto wetu mpaka wawe wakubwaaaaaaa, na wajukuu TUWAONE! amen!
nilipokuwa naisoma hii post nimekumbuka mambo mengi sana P,those days tunakua the way nlikuwa namwona mzee K akiongozana na mama kanisani na rozali zao mkononi!nimelia kusema ukweli!wazazi wako wanapenda sana kusali mke mwenza no wonder una imani kubwa kiasi hiki! I LOVE YU SIS!
mi wazazi wote hawapo ! RR naomba nikudese mstari wako! I LOST HIM NIKIWA VERY YOUNG KIASI SIKUONA TOFAUTI
I LOST HER NIKIWA NAJIELEWA KIASI SIWEZI KUSAHAU MAUMIVU YAKE!dah!acheni jamani!mlio na wazazi wenu muwapende na kuwaenzi sana jamani!wenzenu tunatamani sana tungekuwa nao sasa tuweze kuwashower na haya tuliyonayo!mi huwa kila nikiona suti nzuri ya kimama huwa namuimagine mama yangu angekuwa ameivaa baada ya mimi kumnunulia na kumpelekea nyumbani kwake yani ile makelele flan hivi "mum check nimekulipuaje leo!''
DAH! i miss them badly!sana jamani!
 
Oooh so sory cacico Mungu ni mwema ataendelea kumlinda na tuwe na imani atapona!

hii thread IMENILIZA, NA WOTE MLIOCHANGIA! i have both parents though my mama is seriously sick huu ni mwaka wa 3! hawezi kuongea anaongea kw ishara na akihuzunika au kama kuna kitu kinamuuma hulia! my dad is ONE in a million man! kila anapokwenda huenda na mama, kabla ya kwenda kazini anahakikisha mum kapewa dawa, chakula etc, labda tu niseme kuwa hata kula mum hali kwa mdomo ana mwaka wa tatu pia, amewekewa tube TUMBONI, SO KILA KITU KINAPITA KWA TUBE!

NIMESHALIA SANA, NIMESHAKUWA SUGU, NAMUOMBEA UJASIRI WA KUVUMILIA YOTE NAIOMBEA PIA FAMILIA YANGU TUSHIKAMANE KATIKA KIPINDI HIKI CHA KUMUUGUZA MAMA MPAKA HAPO MUNGU ITAKAPOMPENDEZA KUMPONYA KABISA!

SIJUI NI KWA NINI, ILA NINA IMANI KUBWAAAAAAA KUWA ATAPONA KABISA! ATAKUJA KUONGEA NA KUWA MZIMA TENA!! poleni wapendwa wote mliopoteza wazazi,. HAKIKA INAUMA SANA, I CAN IMAGINE WHAT U HAVE BEEN THROUGH!! MUNGU WETU AWAPE FARAJA, ATUPE NA SISI MAISHA MAREFU, ILI tuweze kuwalea watoto wetu mpaka wawe wakubwaaaaaaa, na wajukuu TUWAONE! amen!
 
Ooh sorry snowhite, daa wazazi ni muhimu sana na tunapo wapoteza tuna umia sana bila shaka mungu wetu ni mwema anaendelea kutufariji!

Mimi mwenyewe hii post kwa kweli imenitoa machozi pamoja nilimpoteza baba yangu nikiwa mdogo sana lakini najua umuhimu wa wazazi na upendo wao, namshukuru mungu ameendelea kumpigania mama yangu na kutuendelea kutulea na mungu wetu ameendelea kuwa mfariji wetu kila leo. Kwakweli uchungu wa kufiwa na mzazi anajua yule ambaye ameondokewa na wazazi!

Mungu ni mwema kila leo.

nilipokuwa naisoma hii post nimekumbuka mambo mengi sana P,those days tunakua the way nlikuwa namwona mzee K akiongozana na mama kanisani na rozali zao mkononi!nimelia kusema ukweli!wazazi wako wanapenda sana kusali mke mwenza no wonder una imani kubwa kiasi hiki! I LOVE YU SIS!
mi wazazi wote hawapo ! RR naomba nikudese mstari wako! I LOST HIM NIKIWA VERY YOUNG KIASI SIKUONA TOFAUTI
I LOST HER NIKIWA NAJIELEWA KIASI SIWEZI KUSAHAU MAUMIVU YAKE!dah!acheni jamani!mlio na wazazi wenu muwapende na kuwaenzi sana jamani!wenzenu tunatamani sana tungekuwa nao sasa tuweze kuwashower na haya tuliyonayo!mi huwa kila nikiona suti nzuri ya kimama huwa namuimagine mama yangu angekuwa ameivaa baada ya mimi kumnunulia na kumpelekea nyumbani kwake yani ile makelele flan hivi "mum check nimekulipuaje leo!''
DAH! i miss them badly!sana jamani!
 
Ooh sorry snowhite, daa wazazi ni muhimu sana na tunapo wapoteza tuna umia sana bila shaka mungu wetu ni mwema anaendelea kutufariji!

Mimi mwenyewe hii post kwa kweli imenitoa machozi pamoja nilimpoteza baba yangu nikiwa mdogo sana lakini najua umuhimu wa wazazi na upendo wao, namshukuru mungu ameendelea kumpigania mama yangu na kutuendelea kutulea na mungu wetu ameendelea kuwa mfariji wetu kila leo. Kwakweli uchungu wa kufiwa na mzazi anajua yule ambaye ameondokewa na wazazi!

Mungu ni mwema kila leo.
pole nawe!jamaa sijui kafikiria nini!kimsingi nawamiss sana wazazi wangu shem!sana!sina tu jinsi!
 
Habari za hapa wanajamvi?

Leo napenda tujadili kitu tofauti kidogo na mazoea yetu. Nacho ni hisia na maisha kwa ujumla bila ya wazazi.

Umeshawahi kujiuliza ikatokea leo wazazi wako wakachukukiwa na BwANA kwenda kwenye makao ya kudumu?

Kwa wale waliopatwa na hali hiyo nadhani wana picha hali jinsi inavyokuwa. Lakini nalo nadhani inategemea unaachwa na wazazi ktk umri gani.

Hebu fikiria unafiwa na mzazi mmoja wapo ukiwa labla shule au chuo ni tofauti na yule aliyefiwa na mzazi wake wakati akiwa mtu mzima ana kazi yake na maisha yake.

Hebu fikiria ukaondokewa na baba yako mzazi aliyekuwa anakupenda sana hadi wewe mwenyewe ukajua unapendwa. Unabaki na mama ambaye sasa ni mjane na siku moja anakuomba pesa(na sio kawaida yake kukuomba pesa) na wewe ukawa huna pesa hizo kwa wakati huo utajisikiaje?

Kwangu mimi huwa nafikiri kuishi pasipo na mzazi mmoja au wote ni kama kujitenga na dunia vile. Japo sasa ni mtu mzima na familia yangu lakini naweza kuamka usingizini usiku sana na nikakumbuka kuwa sina baba ameshatangulia kwenye makao ya milele huwa natokwa na machozi na siwezi tena kulala.


Hebu tujadili kwa pamoja nini kifanyike ili mtu upate furaha ya kudumu japo huna wazazi.

Kwani huwa ni furaha ya muda tu mfano mimi nikikumbuka tu nakosa raha hata nikiwa eneo gani japo tangu nimeondokewa na mpendwa wangu miaka 6 iliyopita.

Karibuni.


nimesoma uzi huu nikapata hisia kali. Nimefiwa na wazazi wangu wote wawili this year (2012) kwa wakati mmoja na siku moja ni kitu kigumu kidogo kueleza but atleast mtanielewa, and nilikua wa kwanza kwenda kutambua miili kama ni yao kweli. It pains a lot aisee but through GOD the Almight Father yote yanawezekana na unaendelea na maisha!

wazazi wametangulia bado sijaanza kujitegemea but wameniacha na urithi wa elimu ambao unanipa nguvu na moyo wa kujipanga na kujitegemea na kuona maisha ni changamoto ambayo haipaswi kukimbiwa but ni kupigana nayo mpaka utakapopata mafanikio.
ninachojaribu kuwashirikisha kwamba ni kitu kigumu sana kukielewa na ni kigumu sana kukikubali lakini sio kwamba ndio mwisho wa maisha, maisha yanaendelea na unatakiwa usimame na upigane kiume ukiendeleza yale mazuri na bora ambayo wazazi/mzazi alikuachia.

wazazi wangu walikua wanatupenda mimi na ndugu zangu na walikua karibu sana na sisi ni pigo kubwa tulipata na pengo ambalo haliwezi kuzibika na halitakuja kuzibika lakini bado tunapambana na maisha na kumtegemea aliye juu (Mungu) katika kila kitu!
nadhani ni hayo tu nilijisikia ku-share nanyi wana jamii wenzangu. may God bless u all and awape strength ya ku-face magumu yakijitokeza! Mungu Ibariki Tanzania, Mungu wabariki Watanzania! Amen
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom