Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Sizungumzii kwamba ulikuwa unampenda zamani halafu baadaye mapenzi yakachuja. Sizungumzii kwamba ulikuwa unampenda mtu kiukweli kabisa na ukajitoa jumla jumla katika taasisi takatifu ya ndoa na ukafurahia mwanzoni lakini baadaye vikachachuka. Nazungumzia wale ambao toka mwanzo kabisa anajua kabisa anaoa au anaoelewa na mtu asiyempenda hasa kama alivyokuwa anampenda "fulani' ambaye kutokana na sababu zilizokuwa nje yao hawakuweza kufunga ndoa.
Sasa unaingia katika ndoa ukijua kabisa kuwa moyo wako ulishatekwa na mtu mwingine na majaribio yako yote ya maisha kumuondoa moyoni yalishindikana na hivyo ukakubali kuendelea na maisha ukijua kabisa kuwa moyo wako uko kwa fulani. Ulijitahidi kumfuta lakini ikatokea siku mkakutana au mkaonana na kujua kuwa mioyo yenu bado inawaka kwa mapenzi ya ajabu. Huko uliko labda umeshajaliwa na vijunior kadhaa. Lakini katika udhaifu wako ukaamua kwenda "kuonana" na yule mwenzio wa zamani na kwa kweli "kuonana" mlionana; siyo mara moja wala mara mbili.
Na yeye huko aliko kaoa au kaolewa lakini naye kabisa kabisa anakumbuka mapenzi yenu. Sasa mwisho mnajikuta mnakula kuwili kama ndumilakuwili. Huku unafurahia maisha ya ndoa na usalama wa ndoa lakini kule kwingine unafurahia mapenzi ambayo unaamini kabisa ni "haki" yenu kwa sababu hayakuwahi kufa.
Katika mazingira hayo unajiona ni mnafiki una cheat au humtendei haki mwenzio?
Je, kama ungepewa uwzo wa kutoka kwenye ndoa na yule mwingine akatoka kwenye ya kwake (tukiassume kuwa hilo linawezekana) je ungetoka ili muweze kuwa pamoja?
Itakuwaje kama ukitoka kwenye ndoa yako na yeye akatoka kwenye ya kwake halafu mkaishi pamoja na mambo yasiwe vile ulivyofikiria? siyo kwamba ikawa yale ya "kukosa mwana na maji moto"?
Je yawezekana kumbe upendo ni zaidi ya hisia tu ya mahaba bali pia ni uamuzi wa akili? Lakini moyo kweli ukipenda waweza kukoma?
tafakari ya leo
Sasa unaingia katika ndoa ukijua kabisa kuwa moyo wako ulishatekwa na mtu mwingine na majaribio yako yote ya maisha kumuondoa moyoni yalishindikana na hivyo ukakubali kuendelea na maisha ukijua kabisa kuwa moyo wako uko kwa fulani. Ulijitahidi kumfuta lakini ikatokea siku mkakutana au mkaonana na kujua kuwa mioyo yenu bado inawaka kwa mapenzi ya ajabu. Huko uliko labda umeshajaliwa na vijunior kadhaa. Lakini katika udhaifu wako ukaamua kwenda "kuonana" na yule mwenzio wa zamani na kwa kweli "kuonana" mlionana; siyo mara moja wala mara mbili.
Na yeye huko aliko kaoa au kaolewa lakini naye kabisa kabisa anakumbuka mapenzi yenu. Sasa mwisho mnajikuta mnakula kuwili kama ndumilakuwili. Huku unafurahia maisha ya ndoa na usalama wa ndoa lakini kule kwingine unafurahia mapenzi ambayo unaamini kabisa ni "haki" yenu kwa sababu hayakuwahi kufa.
Katika mazingira hayo unajiona ni mnafiki una cheat au humtendei haki mwenzio?
Je, kama ungepewa uwzo wa kutoka kwenye ndoa na yule mwingine akatoka kwenye ya kwake (tukiassume kuwa hilo linawezekana) je ungetoka ili muweze kuwa pamoja?
Itakuwaje kama ukitoka kwenye ndoa yako na yeye akatoka kwenye ya kwake halafu mkaishi pamoja na mambo yasiwe vile ulivyofikiria? siyo kwamba ikawa yale ya "kukosa mwana na maji moto"?
Je yawezekana kumbe upendo ni zaidi ya hisia tu ya mahaba bali pia ni uamuzi wa akili? Lakini moyo kweli ukipenda waweza kukoma?
tafakari ya leo