masara
JF-Expert Member
- Jul 20, 2016
- 1,738
- 2,279
Mwaka ndio bado mmbichi kabisa naamini uko salama salimini.
Ni ukweli kwamba mtu kuoa au kuolewa haimaniishi kwamba ndio amefungiwa kabisa kupenda na kupendwa na mwingine ila kinachofanyika huwa heshima ya kiapo tu. lakini pamoja na kiapo bado hisia na tamaa au mazingira huwa yanalazimisha kuvunja kiapo kama inavyovunjwa katiba na sheria za nchi fulani fulani duniani.
Sasa inapotokea uko kimahusiano na mume au mke wa mtu au mtu ambaye yuko kwenye mahusiano rasmi basi hakikisha mnakubaliana namna ya kuwasiliana ili kuweka usalama kati yenu na mahusiano yaliyokuwepo,
Kwa mfano muwe na namna kuandika ujumbe wa kwanza na namna ya jumbe kujibu ili kujiridhisha kuwa anayeandika ujumbe ndio mhusika na sio mtu mwingine , au namna ya kupokea simu ili kujiridhisha aliyepokea sio ni mhusika na sio mwingine kabla ya kuongea chochote, maana kuna wale wazee wa simu ikishapokelewa tu yeye tayari ameshaongea maneno kama yote bila kujua anaogea na nani.
Mfano, ujumbe wa kwanza kama haujaona kitu fulani basi usijisumbue kujibu na kama ataendelea kukusumbua basi unajifanya hauijui hiyo namba maana unaweza kuta mtu amebananishwa huko katoa pasword na unayechat naye ndio aliyelipia mahali au ndi mke mkubwa na wewe ukajaa bila kujua.
Au namna ya kupokea simu yaani hata kama unaharaka gani akipokea simu na asipoanza na code mlizokubaliana hata kama saui ni ya kwake yaani hapo kata simu chap pita hivi.
Lakini la muhimu zaidi ni kuelewa mwandiko mwa mwenzako kwenye ujumbe huwa anaandikaje, maana kila mtu na mwandiko wake kwenye simu ukiwa makini unaweza ukajua tofauti ya uandishi wa watu.
Unaweza kugundua mtu anapenda kuandika kwa kifupi sana au neno zima au kuna vitu anapenda kuweka ili ujue labda katikati ya kuchat mambo yameharibika na wewe unabadilisha ngia angani
Ni ukweli kwamba mtu kuoa au kuolewa haimaniishi kwamba ndio amefungiwa kabisa kupenda na kupendwa na mwingine ila kinachofanyika huwa heshima ya kiapo tu. lakini pamoja na kiapo bado hisia na tamaa au mazingira huwa yanalazimisha kuvunja kiapo kama inavyovunjwa katiba na sheria za nchi fulani fulani duniani.
Sasa inapotokea uko kimahusiano na mume au mke wa mtu au mtu ambaye yuko kwenye mahusiano rasmi basi hakikisha mnakubaliana namna ya kuwasiliana ili kuweka usalama kati yenu na mahusiano yaliyokuwepo,
Kwa mfano muwe na namna kuandika ujumbe wa kwanza na namna ya jumbe kujibu ili kujiridhisha kuwa anayeandika ujumbe ndio mhusika na sio mtu mwingine , au namna ya kupokea simu ili kujiridhisha aliyepokea sio ni mhusika na sio mwingine kabla ya kuongea chochote, maana kuna wale wazee wa simu ikishapokelewa tu yeye tayari ameshaongea maneno kama yote bila kujua anaogea na nani.
Mfano, ujumbe wa kwanza kama haujaona kitu fulani basi usijisumbue kujibu na kama ataendelea kukusumbua basi unajifanya hauijui hiyo namba maana unaweza kuta mtu amebananishwa huko katoa pasword na unayechat naye ndio aliyelipia mahali au ndi mke mkubwa na wewe ukajaa bila kujua.
Au namna ya kupokea simu yaani hata kama unaharaka gani akipokea simu na asipoanza na code mlizokubaliana hata kama saui ni ya kwake yaani hapo kata simu chap pita hivi.
Lakini la muhimu zaidi ni kuelewa mwandiko mwa mwenzako kwenye ujumbe huwa anaandikaje, maana kila mtu na mwandiko wake kwenye simu ukiwa makini unaweza ukajua tofauti ya uandishi wa watu.
Unaweza kugundua mtu anapenda kuandika kwa kifupi sana au neno zima au kuna vitu anapenda kuweka ili ujue labda katikati ya kuchat mambo yameharibika na wewe unabadilisha ngia angani