Unapenda ipi kati ya hizi?

RayB

JF-Expert Member
Nov 27, 2009
2,752
196
Tukiwa ndo kwanza tunahang over ya Valentine day, je ulipata zawadi gani toka kwa akupendae?

Anyway hoja kubwa niliyonayo ni kuhusu kadi au message tunazotumiana wakati wa siku za kawaida na hasa siku maalumu kama ya jana. Kwa upande wa SMS utaona message nyingi ambazo mara nyingi huwa zimekuwafowaded. Kwa kifupi unaweza kupata ujumbe ule ule toka kwa watu mbali mbali.

Hivyo hivyo kwa utamaduni wengi wa sisi wabongo siku hizi huwa tunanunua kadi. LAkini kadi nyingi tunazotumiana huwa zinakuwa na maneno tayari. Yaani ndo kusema ukipata kadi leo, maneno matamu yaliyomo humo basi sio ya kutoka katika kichwa au moyo wa aliyekuletea bali ni maneno ya mchapishaji ambayo yule aliyekuletea kayapenda ndo kusema hayako real. Hii ni tofauti sana na kwa wenzetu amnako kadi nyingi huwa zinakiuwa BLANK na mtu huandika maneno yake REAL hapo. Kuna kipindi nilitafuta kadi blank bongo sikufanikiwa kupata kwa haraka kiasi hicho. Vivyo hiivyo kwa SMS.Je tatizo ni nini?

Hoja inakuja je unajisijisikiaje unapopata kadi za namna hiyo? Huwa unazipenda? Binafsi huwa sizipendi na nigependa maneno hata kama ni mawili tu lakini ya ukweli toka kwake. Wewe je unapenda style ipi kati ya hizo?
 
Asavali umeiongelea hii kitu!
Mie imenitoa ushabiki kabisa ; kwanza msg za aina hiyo nikizipzzta kwenye sms sizipi uzito sawa na mtu akiniandikia ama akipiga!

Sipendi teknolojia kuteka uhalisia wa mambo na wakati mwingine mambo yamecheleweshwa kwa kuwa watu wana imani sana na technolojia
 
Tukiwa ndo kwanza tunahang over ya Valentine day, je ulipata zawadi gani toka kwa akupendae?

Anyway hoja kubwa niliyonayo ni kuhusu kadi au message tunazotumiana wakati wa siku za kawaida na hasa siku maalumu kama ya jana. Kwa upande wa SMS utaona message nyingi ambazo mara nyingi huwa zimekuwafowaded. Kwa kifupi unaweza kupata ujumbe ule ule toka kwa watu mbali mbali.

Hivyo hivyo kwa utamaduni wengi wa sisi wabongo siku hizi huwa tunanunua kadi. LAkini kadi nyingi tunazotumiana huwa zinakuwa na maneno tayari. Yaani ndo kusema ukipata kadi leo, maneno matamu yaliyomo humo basi sio ya kutoka katika kichwa au moyo wa aliyekuletea bali ni maneno ya mchapishaji ambayo yule aliyekuletea kayapenda ndo kusema hayako real. Hii ni tofauti sana na kwa wenzetu amnako kadi nyingi huwa zinakiuwa BLANK na mtu huandika maneno yake REAL hapo. Kuna kipindi nilitafuta kadi blank bongo sikufanikiwa kupata kwa haraka kiasi hicho. Vivyo hiivyo kwa SMS.Je tatizo ni nini?

Hoja inakuja je unajisijisikiaje unapopata kadi za namna hiyo? Huwa unazipenda? Binafsi huwa sizipendi na nigependa maneno hata kama ni mawili tu lakini ya ukweli toka kwake. Wewe je unapenda style ipi kati ya hizo?
Its a copy and paste theory!!Huu ni ugonjwa tuliojijengea toka mashuleni,yaani hizi ndio athali za kugezeana,unakuta mtu anadigrii lakini tokea nursery kafaulu kwa kugezea tuu,unahisi nini atakifanya huku ukubwani kwenye mambo magumu hivi?
 
Yaani wakuu huwa naichukia hakuna mfano. Ni bora mtu asiwe na kadi akaleta karatasi iliyoandikwa kwa maandishi yake. Unakuta katika zile ready made cards mtu anaweka signature tu pale mwishoni eti "says me" ni uvivu wa kufikiri.

Natoa mfano katika valentine hii jamaa yangu alifanya funny thing kweli lakini very romantic; alikuwa na laptop iliyokufa basi alichofanya ni kuchomoa keys na kuzibandika ktk kadi aliyoitengeneza na ikasomeka "........... I LOVE YOU" Hhpo kwenyew dots likiwa ni jina la mpenzi wake yaani vey romantic kwa kweli
 
Habari hiyo ipo pia kwenye forwarded emails, ningekuwa na uwezo wa kudhibiti ningefurahi mno!! sifagilii kabisa la kutumiana emails za nini sijui, zingine zina vitisho usipotuma sijui utakufa, nadhani ningekuwa mbolea sasa kwa ukaidi huo.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom