Atoto
JF-Expert Member
- Jul 19, 2013
- 82,086
- 158,877
Nami nije mnilee?Nipo nae hapa. Tunalea
Nami nije mnilee?Nipo nae hapa. Tunalea
HahahahahahNimemkumbuka Dotto Manyasi. Tulisoma Pamoja Iseni Primary School, Nyegezi Mwanza. Nilikuwa tukitoka Shule saa 8 mchana, jioni saa 10 nafunga safari mpaka kwao Nyegezi kijiweni, Naangalia nyumba yao mpaka saa 12 jioni narudi home. Moyo umefurahi kabisa.
Sikuwahi kumtamkia chochote zaidi ya kutabasamu kila tukigongana macho.
Nashukuru Mungu nilifanikiwa kupata picha yake siku ya Graduation ya la Saba. Mpaka sasa ninayo.
Umeitendea haki ID yako, ndugu storyteller.Dah... mtoto pendo... nisipoenda class vidudu hasomi, analia siku nzima hadi arud hom anione....
Nami nikampenda, sipandi piki piki 110 ya baba adi niwe na pendo
Pendo roho iliniuma baba angu alipoamua darasa la kwanza nikasomee kwetu milimani... huo ukawa mwanzo wa kukupoteza pendo.
Ninarud darasa la3, pendo wamehama, haijulikani wapi... naangukia kwa salma... mtoto mixer mrangi na muarabu... salma anakua serious hanipendi hadi siku nawakuta wanacheza kimama mama... nakaitwa niwe baba... penzi likawa la kweli... nikitoka shule salma lazma aje kwetu... nimuoneshe mbwa wangu simba.. mbwa anayeogopeka mtaani kwetu nyuma ya mskiti wa masjid qubah.... ah salma tukicheza kombolela twaenda jificha juu ya magunia ya mahindi yalopangwa hadi juu... tunatafutwa hadi tunaitwa tujitokeze...
Tunahamia chang'ombe hadith yangu na salma nayo inaishia hapo...
Najikuta namtaman nankumpenda mtoto anjelina... ila yuko sirias na shule, hataki ujinga... ananikataa
Maisha yanaenda kwa kasi huku na kule namaliza form4... nakuwa rafiki na jamaa mmoja... urafiki kupitia rafiki.
Naenda kumpitia nyumbani kwa jamaa twende club84, lahaulaaaah... namkuta pendo... kumbe jamaa ni kaka ake pendo... pendo hanikumbuki na mm naingia ganzi coz imekua pisi kali balaaaaaaaa.
Baada ya muda namkumbusha... dah pendo anafurah... tunaanza urafiki.... baada ya muda kidume naomba game...
Pendo anakolea kwa shoo za kibabe na kisela.... lkn anakuja gundua nina pisi nyingine..... anapata tabu sana hadi jamaa ikabidi aniombe nimsaidie dada ake asije kufa kwa tatizo la moyo... mimi usela unakua mwingi nimekolea kwa mtoto wa kiswazi mtoto wa kawaida sina ilanhana complication... mtoto wa kiswazi ila anaishi kizungu..... kuhama mkoa inakua suluhisho kwa pendo... anaenda kwao moshi....
Maisha yanaenda kwa kasi ya ajabu...
Siku nipo nam hotel, nakula zangu bia, mara zinaingia pisi kama 3 ivi kali balaa... kuchek moja naiona kumbe ni salma... dahhh.... bila kujizuia kaja tukahug.... salma kachora mitatuu... salma anaonekana kawa paka shume... anaonekana ukiingia kiboya unapigwa ela na mzigo hupati... kumbe yana apointment na mbunge fulani wakale raha..
Salma ananipa namba.... baada ya kuondoka na yule mbunge... usiku salma ananichek ananiambia amelewa sana anaomba nikamchkue nmpeleke nyumbani... dah
Kiukweli sikuweza kubisha, namkuta dodoma hotel, anaingia kwe taksi ya jamaa yangu yasin mzee wa kuwalamba... jinsi alivyo jambazi kumbe salma keshanitathmini kajua labda nna maisha... dah kumbe me kachala tu mzee wa mishe mtu wa watu... akiwa amenikumbatia ananiambia hawez kwenda kulala pekeake kwanza kwao hawatamfungulia.... dah.. kidume namwambia yassin anipeleke geto.....
Mwezi na zaidi salma anakolea... mara paap... siku anakuja na kikaratas cha hospital... kapima ana mimba, yuko pia na kipimo cha mkojo kwamba kama siamini apime tena mbele yangu... lahaulaaa
Salma uyu uyu mtoto wa mjini mwenye mambo mengi... aaah siwez zaa na mwanamke wa ivi mimi... najisemea akilini
Salama anagoma kutoa mimba anaamua kuzaa..
Mishe za hapa na pale... huku na kule tunapoteana na salma...
Maisha yanaendelea...
This is wonderfulCrush wangu wa utotoni ndio mume wangu
Nilijua sana ulinizimia ata Mimi nilikuzimia sema tuyarudieRichie W. aka Richie Richie ( huyu tulipendana wote hadi tunamaliza lasaba B ila wote tulikuwa tunanata hakuna aliyetaka kumsemesha mwenzake. Tukawa tukasalimiana tuu na kupeana tabasamu basi). Sekondari tulipangiwa shule jirani tukawa tunaonana njiani saa ya kutoka au asubuhi kuingia shule.... alipopangiwa Minaki tukapotezana mazima hadi leo. Nilifatilia post za A level shule yao nikajua kapangiwa Minaki.... crush ya primary ikaishia hapo.)
Nkundwe ....( huyu hakujua kama nilimzimikia ila sababu alikuwa handsome waschana wengi walikuwa wanamsonga.... sikumbuki vizuri kama alihama tukiwa lasaba B au baada ya hapo alihamia ughaibuni.
Baada ya hapo nikawa mkaksi hadi nilipoingia chuo ndo nikaanza mahanjam .
Sio kuwa alikuwa kiranja au kipanga fulani?Same
Crush wangu wa secondary nikimuona najishangaa sana
Kasinde...Upendo ni Mungu.
Upendo unapokuwa asili bila mapenzi ndani yake ni utu.
Mungu akutie nguvu, hatuijui kesho yetu, si ajabu baada ya kukuona ukampa tumaini na nguvu kutoka ndani yake ya kuinuka tena kwa kutia bidii kwenye mazoezi.
Kila la kheri.
Kuna jamaa yeye alipenda mpaka mtaa anaoishi na kila kitu, yele mapenzi yaachwe kama yalivyo.Anitha alinitamkia ananipenda tulikutana tuition tukiwa darasa la pili alinipenda sana nikatokea kumpenda Dah! Kwao walikuwa na duka kuna wakati yeye alikua anauza nikienda dukani kununua kitu cha mia 500 anaweka 1,500 Mama akashtuka ikabidi nimwambie ukweli nilimpenda Anitha nilikua napenda hadi magari ya Baba yake
Balaa haya mambo hayo haaaaaaaah haaaaaahKuna jamaa yeye alipenda mpaka mtaa anaoishi na kila kitu, yele mapenzi yaachwe kama yalivyo.
Kwa mara ya kwanza Nimepata mtu aliyetajwa humu naemfahamu, huyo nkundwe Ni mnyaki madam kasie, na amesharudi bongo ana mke wa kihaya na watoto wawili?????
Ndio.. unaweza kutana na mwanamke mwenye nguvu 🤭
Nilijua sana ulinizimia ata Mimi nilikuzimia sema tuyarudie
Kasie Mahaba Matata
Kasinde...
Umeandika mistari fulani ambayo natamani kila mtu angelielewa