Unakumbuka wimbo wa Stella wa Freshley Mwambuli? Kisa chake hiki hapa

Wildlifer

JF-Expert Member
May 12, 2021
1,881
5,183
Mambo ya mapenzi ni mazito sana. Huu wimbo sikuwahi jua kuwa ni kisa cha kweli.

=========

Wakenya katika mitandao ya kijamii wamechangamkia sana wimbo wa Stella Wangu wa mwanamziki mashuhuri wa humu nchini Freshley Mwamburi.

Wamechangamkia wimbo huo wakikumbuka leo hii ni tarehe 17 mwezi wa tano mwaka wa 1992 mpenzi wake wa Kenya, Stella, aliposhuka kutoka kwa ndege na mchumba wake wa urefu wa futi nne Mjapani huku amebeba mtoto mkononi.

Leo ni miaka 30 tangu siku hiyo.
Freshley anasema alitaka tu kuthibitisha ni kweli Stella ameamua kuolewa na mwalimu wake huyo huko Japan alikoenda kusomea utabibu.

Wakenya wametuma ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, wengine wakimkashifu Stella kwa kumtumia vibaya Freshley ambaye aliuza mifugo na shamba lake ili Stella apate nauli ya kusafiri Japan.

Lakini sasa Freshley amesahau yote hayo, na bado anawasiliana kwa simu na Stella akiwa Tokyo, Japan lakini anasema hamna lolote hapo kimapenzi ila ni kujuliana hali tu.

Stella sasa ana watoto wawili, naye Freshley ameoa na ana watoto wanne - wavulana watatu na msichana mmoja.

Katika wimbo wake, Freshley aliimba:

"Nilikua na mchumba wangu, tulipendana kama nyama choma

Alibahatika kwenda ngambo, chuo kikuu kwenda kusoma, miaka mitatu kule Japani kusomea udakitari, Stella wangu ehhh.

Nilivyompenda Stella jamani kajitolea kwa roho moja, nikauza shamba langu, sababu yake yeye,

Nikauza gari langu, sababu yake yeye nikauza Ng'ombe na mbuzi sababu yake yeye,

Ili apate nauli ya ndege na pesa nyngine za matumizi kule Japani,

Ilikua tarehe kumi na saba mwezi wa tano, ilikuwa tarehe kumi na saba mwezi wa tano, mwaka elfu moja tisa mia tisaini na mbili, ndiyo ilokua tarehe kamili ya Stella kurudi Kenya.

Nilikwenda uwanja wa ndege kwenda kumlaki Stella, nilikua na uncle (mjomba/au rafiki) Kilinda uwanja wa ndege.,"

Anaendelea:

"Ghafla ndege ilipotua uwanajani tuliona vituko, Stella alishuka amebeba mtoto mkononi, nyuma yake mchumba wake mfupi, futii nne Mjapani,

Nilisikitika ndani ya moyo nikakosa la kufanya,

Nilitamani nilie Kikamba lakini si kijui, ilibidii nilie Kijaluo "anatimang'owajowa",

Freshley, nilitamani nilie Kihindi lakini si kijui, ilini bidii nilie Kitaita lugha ya mama na baba,

ilinibidi nilie Kitaita, "beke mwana niponyebanda, Freshley".


 
Mambo ya mapenzi ni mazito sana. Huu wimbo sikuwahi jua kuwa ni kisa cha kweli.

=========

Wakenya katika mitandao ya kijamii wamechangamkia sana wimbo wa Stella Wangu wa mwanamziki mashuhuri wa humu nchini Freshley Mwamburi.

Wamechangamkia wimbo huo wakikumbuka leo hii ni tarehe 17 mwezi wa tano mwaka wa 1992 mpenzi wake wa Kenya, Stella, aliposhuka kutoka kwa ndege na mchumba wake wa urefu wa futi nne Mjapani huku amebeba mtoto mkononi.

Leo ni miaka 30 tangu siku hiyo.
Freshley anasema alitaka tu kuthibitisha ni kweli Stella ameamua kuolewa na mwalimu wake huyo huko Japan alikoenda kusomea utabibu.

Wakenya wametuma ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, wengine wakimkashifu Stella kwa kumtumia vibaya Freshley ambaye aliuza mifugo na shamba lake ili Stella apate nauli ya kusafiri Japan.

Lakini sasa Freshley amesahau yote hayo, na bado anawasiliana kwa simu na Stella akiwa Tokyo, Japan lakini anasema hamna lolote hapo kimapenzi ila ni kujuliana hali tu.

Stella sasa ana watoto wawili, naye Freshley ameoa na ana watoto wanne - wavulana watatu na msichana mmoja.

Katika wimbo wake, Freshley aliimba:

"Nilikua na mchumba wangu, tulipendana kama nyama choma

Alibahatika kwenda ngambo, chuo kikuu kwenda kusoma, miaka mitatu kule Japani kusomea udakitari, Stella wangu ehhh.

Nilivyompenda Stella jamani kajitolea kwa roho moja, nikauza shamba langu, sababu yake yeye,

Nikauza gari langu, sababu yake yeye nikauza Ng'ombe na mbuzi sababu yake yeye,

Ili apate nauli ya ndege na pesa nyngine za matumizi kule Japani,

Ilikua tarehe kumi na saba mwezi wa tano, ilikuwa tarehe kumi na saba mwezi wa tano, mwaka elfu moja tisa mia tisaini na mbili, ndiyo ilokua tarehe kamili ya Stella kurudi Kenya.

Nilikwenda uwanja wa ndege kwenda kumlaki Stella, nilikua na uncle (mjomba/au rafiki) Kilinda uwanja wa ndege.,"

Anaendelea:

"Ghafla ndege ilipotua uwanajani tuliona vituko, Stella alishuka amebeba mtoto mkononi, nyuma yake mchumba wake mfupi, futii nne Mjapani,

Nilisikitika ndani ya moyo nikakosa la kufanya,

Nilitamani nilie Kikamba lakini si kijui, ilibidii nilie Kijaluo "anatimang'owajowa",

Freshley, nilitamani nilie Kihindi lakini si kijui, ilini bidii nilie Kitaita lugha ya mama na baba,

ilinibidi nilie Kitaita, "beke mwana niponyebanda, Freshley".


Leo ni miaka 29.
 
nae alizidi mtu hamjamit kitambo na bebi wako siku ya kumpokea unaenda na lundo la watu faragha mtaipata sangapi? uambebe mpk mtu na mke na watoto na ndugu Hafidhi mtoto wa Mombasa saafi Stella komesha
 
nae alizidi mtu hamjamit kitambo na bebi wako siku ya kumpokea unaenda na lundo la watu faragha mtaipata sangapi? uambebe mpk mtu na mke na watoto na ndugu Hafidhi mtoto wa Mombasa saafi Stella komesha
Mapenzi dada. Mshawasha wa kutaka kuonyesha mapenzi humfanya mtu atende kile anachoona kitamkonga nyoyo mwanamke wake. Ndio maana alitaka kufanya 'mapokezi ya kitaifa'
 
Hivi huyu ndiye Stella mwenyewe?
Screenshot_20210517-135911.jpg
 
Mapenzi dada. Mshawasha wa kutaka kuonyesha mapenzi humfanya mtu atende kile anachoona kitamkonga nyoyo mwanamke wake. Ndio maana alitaka kufanya 'mapokezi ya kitaifa'
ha haa ndo akome na mapenzi yake ya plural angeenda peke yake angeona stela anashuka na futi nne mjapani ye angejificha then asepe akalie mbele ya safari ndg na jamaa angewadanganya alishuka tukaenda kupima nimemkuta ana ngwengwe nikamuacha na staki kumskia tena. ingebaki yeye kuwa analia mda akienda kuoga na usiku mda wa kulala
 
ha haa ndo akome na mapenzi yake ya plural angeenda peke yake angeona stela anashuka na futi nne mjapani ye angejificha then asepe akalie mbele ya safari ndg na jamaa angewadanganya alishuka tukaenda kupima nimemkuta ana ngwengwe nikamuacha na staki kumskia tena. ingebaki yeye kuwa analia mda akienda kuoga na usiku mda wa kulala
Hahaha. Hii ni 'modern thinking', back in 92 dunia ilikuwa tofauti kabisa. Enzi zetu hizi za 'tuma na ya kutolea' kupokea mgeni ndio inabidi uende kijasusi.
 
This is one of my best song za zamani haichushi kuisikiliza huwa nacheka anapoongea kilugha chao halafu na picture hiyo convoy alienda nayo uwanjani walivyopanua midomo kumuona Stella na mjapenga hahahahaaaa
 
This is one of my best song za zamani haichushi kuisikiliza huwa nacheka anapoongea kilugha chao halafu na picture hiyo convoy alienda nayo uwanjani walivyopanua midomo kumuona Stella na mjapenga hahahahaaaa
Ukisikiliza nyimbo za hawa wazee, unaona kuwa hekaheka za mapenzi ni jambo la kale sana. Kuna wimbo mmoja wa Marijan Rajab [siukumbuki jina], ila story nyuma ya kile kisa ni kuwa, Marijani alienda mwanza kufanya show na Band yake. Akiwa kule akakutana na mwanamke anaitwa Habiba. Akamuelewa piga sound. Akamwambia aje dar akampa na nauli na pocket money, akamuelekeza na hotel ya kufikia akifika pale amuulizie. Basi baada ya kurudi dar na siku walizokubaliana kufika, Marijani akaenda pale hotelini kuulizia kama kuna mgeni wake. Akakuta hola. Basi karibu wiki mbili anaulizia tu, hakuna mtu aliyekuja. Kiufupi akawa ameambulia patupu. Sasa kwanini hakuja, anayejua ni Habiba tu. Kiufupi alikula nauli na hakutokea.
 
Ukisikiliza nyimbo za hawa wazee, unaona kuwa hekaheka za mapenzi ni jambo la kale sana. Kuna wimbo mmoja wa Marijan Rajab [siukumbuki jina], ila story nyuma ya kile kisa ni kuwa, Marijani alienda mwanza kufanya show na Band yake. Akiwa kule akakutana na mwanamke anaitwa Habiba. Akamuelewa piga sound. Akamwambia aje dar akampa na nauli na pocket money, akamuelekeza na hotel ya kufikia akifika pale amuulizie. Basi baada ya kurudi dar na siku walizokubaliana kufika, Marijani akaenda pale hotelini kuulizia kama kuna mgeni wake. Akakuta hola. Basi karibu wiki mbili anaulizia tu, hakuna mtu aliyekuja. Kiufupi akawa ameambulia patupu. Sasa kwanini hakuja, anayejua ni Habiba tu. Kiufupi alikula nauli na hakutokea.
Kweli mkuu visa vilianza muda sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom