Unakumbuka vioja vipi siku unatahiriwa?

Aisee mi nilienda wakati mkubwa mkubwa nipo secondary tena shule ya Boarding.. Kipindi icho kuna katabia nilikuwa nimetoka nako Boarding ka Pull table...

Ishu ni kwamba baada ya kukatwa mwezi mmoja mbele nikaona hii imekuwa too much lazima nirudi kwenye mchezo wangu wa pull table .. Kilicho tokea najua mwenyewe ili bidi nirudishwe upya hospital..

ukaona hapana lazima ujiselfie
 
Atakae anzisha Uzi wa kinyime chake, ndipo nitakuja kukomenti.
Wakubwa watakuwa wamenielewa.
tapatalk_1574003001155.gif
 
mwenye kibamia wa kwanza kuwa proudly hadharani, hongera kaka angu :D
Basi itakua tunapishana majukwaa. Ila humu nilianzisha hadi movement niliita #IamTiny tukafanya kikao na kuna uzi wetu kabisa. Nikachaguliwa kua mwakilishi kanda ya Pwani wa Chama cha SDU (Short Dicks United) chenye makao yake Nairobi.

So I have always been open about this.

Am so sorry haukuwahi kujua kabla ya leo.
 
kipindi hiko mimi binafsi ndio nimekuwa mkubwa (darasa la sita) nilikuwa namng'ang'ania mzee anipeleke baada ya kuona washikaji zangu wote wameshakatwa..

Basi siku tu mzee akanambia twende hospital moja hv binafsi ambayo daktari mkuu ni rafiki ake.Basi mzee akawasha baiskeli yake phoneix tukaondoka kuelekea huko mida kama ya saa tisa hv adhuhuri

tukafika mapokezi daktari akamwambia wee mzee baki hapa endelea kuangalia mpira (nakumbuka ilikuwa Argentina vs korea kusini)

tuakamuacha mzee ,daktari akiwa katangulia kunipeleka chumba cha mauaji.kiufupi nilikuwa na karoho ka kujiamini na sijui kalitokea wapi. tukaingia hcho chumba cha operation. duh kucheki hv mikasi na vifas kibao vya upasuaji vimejaa ohoo mbona ule ujasiri ukaanza kuniyoyoma.

dr. akanambia vua suruali panda hapo juu .nikapanda asa mule chumbani doctor alikuwa akisaidiana na nurse mmoja ambaye baada ya kupanda kitandani akaanza kumchezea abdala nae akakakamaa. mara paap nikasikia sindano ya kwanza,pili,tatu na nyingne hata sikuzisikia.. nilitamani kulia lakini nikasema mie ni kidume kulia hapana

nilisali sala zote huku akili zikiwa mbali nikisikia msuguano wa mikasi..aloo

baada ya kama saa hv nikaambiwa amka ..kucheki hv dushe limepigwa sijui plaster na bandej afu limevimba na kibaya walivoanza sikuwaambia kuwa nmebanwa na mkojo..nilivoamka doctor akanionesha kile kinyama baada ya operation.. sikuwa na hamu hata ya kukiona kilikuwa cheusi tii afu kina sura mbaya

nikavaa suruali fresh mikono mfukoni nikafika mapokezi mzee akalipa.ile tunatoka nje ya geti duh si ganzi ikakata alooooo yale maumivu sitaki tena kuyasikia afu mzee aliniudhi kinyama eti anataka anipandishe kwenye baiskeli na maumivu yale

nikakataa basi akasema chukua hela ukapande daladala me natangulia nyumbani.. mzee huyo akatokomea na baiskeli..ngoma ikawa kwangu daladala muda wa jioni zinakuwa hamna nikasubiri wee na yale maumivu basi bahati nzur nikapata ..nilichokuws nakiwaza muda huo ni kufika home tu then nilale ..ula mwendo wa daladal ukawa kama wa kinyonga..mara paap nikashushwa kituo cha nyumbani na ikabidi nivuke road. aisee misuli ya miguu nayo ni kama ilipoteza nguvu nikajikuta natembea polepole nikafika home mama hata hajauliza akanipa bonge la bukta (kitenge nilikataa) ila sio mbya mida ya saa 4, usiku maumivu yalikata

Aisee kukojoa ndio ikawa msala mkojo unatoka kidogo kwa kugoma afu unakuwa na njis kama zote.waweza maliza dk 10kibofu hakijawa empty ...

siku yakubadilisha bandeji ya kwanza ndio nililia aiseee kidonda chekundu balaa mpka nikawa najiuliza kitapona kweli..ile anaweka dawa mpya na kufunga bandeji mpya kwa yale maumivu nikawa naona akheri ya siku ile ndio nakatwa govi..

baada ya week hv nikawa fresh.. wazee wanaenda kazini me nmebaki ndani..wakiondoka tu me huyo mtaani nacheza mpira weee nikiona ndio mida yao ya kurudi chap narudi home kama kagonjwa vile.........

aisee kila nikikutana na yule doctor hiwa anacheka sana na kunitania "dogo ushaanza kukitumia?"

najua humu jf wapo waliokatwa govinda porini...leta ushuhuda wako hapa maana na sie wanaume tuna changamoto kama hii
Sijui hata ilikuwaje,mi nilikuwa najuwa ndio nimezaliwa hivyo hivyo,baadaye ndio nikaja kujua kumbe waliniwahi kabla sijawa na akili timamu...
Ilikuwa nikifunikwa nisione mi nafunua nataka nione!! Mpaka walichoka ila ganzi ilikuja kuniishia wkt wanashona Tena kwa huku chini nilitoa ukelele!! Wakaongeza.. nishamaliza daktari ananiita tena kunidunga sindano ya tako nilikasirika hlf kabla yangu kulikuwa na lijamaa kubwa tu ati limetoka kutairiwa duh! Nililicheki kinoma! Watu wengine huwa wanakuwa wapi mpk kufikia umri wa ujana kabisa ndi anatairiwa si shughuli pevu ile! Madaktari wanatabu
Sitakuja kuisahau hiyo siku kwa kweli. Walaaniwe wale jamaa.
Mi wakat wa shughr mkojo ukabana.. na muambia dkt subir nikakojoe hasikii et mpk amalize kushona...

Aaah nikaurusha asingekua mwepes ange'unywa..
Mkojo ulipaa juu then ukarud kwenye dudu baada ya hapo ile chumvi chumvi ya mkojo ikamalza ganzi yote af hajamalza kushona nilijuta,
Dah! Nilikuwa darasa la tatu!
Tulikuwa kama watoto 6 mtaani kwetu.
Nakumbuka nilikuwa na kama miaka 7 na kilichofanyika tulikuwa watoto 6 wa mtaa mmoja. Enzi hizo vijijini kulikuwa na umoja sana. Yaani majirani wenye watoto wanahitaji tohara wanachagua wakakae kwa mtu mmoja mwenye chumba kikubwa na magodoro yanatandikwa chini ndio tunalala hapo mpaka siku mnapona.
Sisi ilikuwa hakuna kulia kwakuwa tuliambiwa ukilia tu wenzako wanakucheka na unatahiriwa huku wenzako wanaona.

Mwanaume anatakiwa atahiriwe kwa kisu, hadharani, umetulia bila kutikisika wala Kutoa chozi hata kidogo. Sio hizi hadithi za ngazi na sijui madakitari.

Mwanaume usipotahiriwa hivi, unakuwa umezidiwa na binti aliyekeketwa.

Inaonyesha kusingekuwa na hospital wengi wenu mngekuwa na mkono wa sweta.
 
Jamaa walinisimamisha kwenye sehemu iliyo na siafu pasipo mimi kujua. Ile kufika usiku kumbe bwana siafu kaingia mtaa wa Magogoni. Kile kilio ilibidi asubuhi nikasalimishwe hospitali, njia ya kumtoa huyo bwana siafu ilibidi nitahiriwe tu. Na mlaaniwe nyie jamaa mlionisimamisua kwenye siafu popote mlipo.
 
nilipelekwa na mamdogo kununua gari la tipper kufika hospital akantoroka nkakutana na mdada nesi mzurii...Akaniingiza wodini basi akiwepo yeye silii akitoka nalia dah wakanikata dushe nikawa natembea na kanzu tu
 
Mwanaume anatakiwa atahiriwe kwa kisu, hadharani, umetulia bila kutikisika wala Kutoa chozi hata kidogo. Sio hizi hadithi za ngazi na sijui madakitari.

Mwanaume usipotahiriwa hivi, unakuwa umezidiwa na binti aliyekeketwa.

Inaonyesha kusingekuwa na hospital wengi wenu mngekuwa na mkono wa sweta.
View attachment 1265772
Nyakati zinabadilika ndugu hapo kabla kulikuwa na simu za mezani baada Miche,sahivi touch.. usikariri binadamu anaenda kwa ufahamu kuna muda ila ilimradi tu tusiiharibu nature laws,Kuna watu wametahiriwa hospital na wanaujasili kushinda huyo uliomuweka hapa jifunze kitu kinaitwa saikolojia ya binadamu utanielewa namaanisha Nini.
 
kivipi mkuu? Yaani mimi niliyesimama naangalia mbele huku ngariba anafanya yake bila hata kutikisika nijidhalilishe kwa huyu aliyepigwa nusu kaputi ndo akakatwa?
ni kujidharirisha Sana, mtu uliyesimama tuli huku ngariba akifanya yake kuchangamana na watu waliochomwa ngazi halafu anajisifia kuwa kaenda jando.
 
kupigwa ganzi ni umama, mtu aliyepigwa ganzi status yake ni sawa na binti aliyevunja ungo, binti akivunja ungo anajikuta tu damu inatoka bila maumivu yoyote.
Faida za kutahiriwa bila ganzi ni nini...?
 
Aisee baada ya siku kadhaa baada ya kukatwa govi, yaani ile alfajiri nikidindisha dudu linauma balaa, sitasahau
 
Mimi nilikuwa darasa la nne.. Nilifungwa macho nikapigigwa ganzi... Nilikuwa nasikia sauti za mikasi tuu... Baadae nafunguliwa naona imevalishwa plasta


Kile kipindi nilikula bata sana, kila mtu alikuwa ananijali
 
Mimi nakumbuka baada ya kutoka hospital nilikua na babu yangu, yeye akafuata mishe zake mimi nikarudi nyumbani. Sasa kabla sijafika hom acha nikutane na mbwa wengi. Ikabidi nisimame kwanza hapo mikono ipo mfukoni naugulia maumivu. Mbele hamna mtu, nyuma hamna mtu kukimbia siwezi. Hapo mbwa wananibwekea huku wananifuata. Nikasema hapa kilichopo akinisogelea nampa buti moja sitajali kama nitaumia. Bahati nzuri haooo wakasepa migombani huko. Nikavuta pumzi nikaendelea na safari. Mshumaa wa Mbao,
 
kweli kabisa wakati umebadirika, ndio maana wanaume wanaolewa siku hizi Kwa kisingizio cha usasa.

Nyakati zinabadilika ndugu hapo kabla kulikuwa na simu za mezani baada Miche,sahivi touch.. usikariri binadamu anaenda kwa ufahamu kuna muda ila ilimradi tu tusiiharibu nature laws,Kuna watu wametahiriwa hospital na wanaujasili kushinda huyo uliomuweka hapa jifunze kitu kinaitwa saikolojia ya binadamu utanielewa namaanisha Nini.
 
wale wa kimila kuna msoto usio na maana. Picha linaanza siku mnatahiriwa mnajengewa kabisa geto la mabua na choo chake mbali na nyumba ili msichangamane. Baada ya ile shughuli kufanyika mnafungwa vitenge kiunoni kifua kikiwa wazi, unapita wembe kichwani bonge la upara halafu mnapakwa matope kuanzia kichwani mpk kiunoni na miguuni. Mtu akishapakwa hilo tope ndo hakuna kuoga mpk mwezi uishe ambapo kuoga ni siku ya kumaliza jando. Maisha ya jando sasa kinachoendelea uko ni mnapoamka asubuhi inatakiwa muondoke mkashinde porini kurudi muda wa msosi mchana, huko porini ndo kufundishana maadili wenyewe wanavyosema japo imetawala misemo fln ya kiluga ambayo ni fulu matusi wenyewe wanaita mizimu, ukiulizwa muzimu na huna jibu basi ni stiki zinatembea haijalishi umefundishwa ama laa, baada ya stiki kama huufahamu huo mzimu ndo utapewa jibu. Stiki zenyewe zinachongwa halafu zinawekwa kwenye moto zikiwa za moto ndo mnaulizana ukikosa inatolewa kwenye moto/majivu unachapwa nayo kwa kufuata mishipa ya mikono yaani inapigwa parallel to veins. Kuna mambo mambo mengi sana ya kiboya huwa yanaendelea huko lakini yote lazima utii iwe umeonewa au laa. Tena ile siku ya kwanza mnatahiriwa tayari mnapewa majina/vyeo kulingana na umri pia mnapewa na kiongozi wenu wa kuwapeleka porini, kuwafundisha na kuwafuatia chakula kwamaana kipindi chote hicho haitakiwi kuonana na wanawake, mkipita mtaani basi macho chini kwa mstari huku mkiimbishwa mapambio ya kilugha. Ikitokea mpo porini mmekutana na mwanamke asiyeolewa bado basi inatakiwa awaheshimu kwa kukimbia asipofanya hivyo mnaruhusiwa kumpiga. Ubaya wazee washapitisha hayo yote so hakuna anayepinga wala kubisha yaani kifupi ni kama all kinds of umama hakuna kabisa hata uonewe na kiongozi bado hauna pa kulalamika. Kuna wadau wanatokaga huko wakiwa wamepata alama za viboko mikono yote kama tatoo kumbuka unachapwa kiboko kikiwa cha moto. Kuna ishu ya msosi pia kula ni lazima hakuna kusema nimeshiba mpk kiongozi aridhike tena kuna ujinga mwingine ile msosi unaletwa ugali ukiwa kama mlima hlf kiongozi anachoma katikati mnatakiwa kula mpk lile tundu lifutike na akijisijia kuongeza anaongeza wala hakuna wa kumuuliza
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom