Unakumbuka Siku ile ya machozi...

Kuhani Mkuu,

..naomba u-edit na kuondoa jina langu kwenye hapo ulipom-quote gagnija.

..naamini kuna kuna wasomaji kutokana na haraka zao wanaweza kufikiri ni mimi ninayedai kwamba kifo cha Sokoine kilitokana na hujuma.
 
UMMA UMTENDEE HAKI EDWARD MORINGE SOKINE, TUNAYO HAKI YA KUJUA NI NANI WALIOKUWA NYUMA YA KIFO CHAKE, JE NI KWELI KAWAWA? MSUYA? NA NANI WALE? TUNAPENDA KUUFAHAMU UKWELI MAANA KAMA NI KWELI ALIUAWA BASI TUWAANGALIE VIONGOZI WETU WA ZAMA HIZO WALIOKUWA NA SURA ZA KIBEPARI NA KUJIFANYA WAJAMAA, NILIKUWA KIJANA WA MIAKA 11 BY THEN BUT NAIKUMBUKA HALI YA MVUA NZITO KULE KIJIJINI KAMA ILIVYOKUWA 2WEEKS HIZI HAPA DAR,YALIKUWA NI MAOMBOLEZO TOKA ROHONI TOKA KWA WATOTO MPAKA WAZEE,NI MAUMIVU YA KWELI,ndio maana ninahamu ya kuangalia TBC1 kama wana lolote kwa kutwa ya kesho hao wengine sitarajii maana wengine ni matunda ya kifo cha Sokoine ila wanajifanya wanataka haki sasa na kusahau walichoifanyia Tanzania zama zao.

FDR Jr,:
Imenibidi niweke mawili matatu katika mchango wako huu.

Kule kwa wenzetu, au hata hapa kwetu isingekuwa njaa kuwa kubwa, jambo la kufanya utafiti na kutunga kitabu, zikiwa juhudi za mtu au watu binafsi zingesaidia kuondoa mambo ya utata kama haya uliyoyazungumzia hapa, hata kama serikali haitaki kujihusisha na uchunguzi kama huo.

Kwa bahati mbaya, utaratibu huu bado hatunao, lakini sina shaka utakuja tu miaka si mingi.

Jamani Eeeee, Tuanze kuwa na tabia ya kuandika vitabu, hasa kuhusu mambo yanayowahusu viongozi wetu (hata wale mafisadi). OOOookay, Mkjj, you can do it, just play your part" au wewe naniiihiii....
 
Kalamu, tatizo hawataki kuzungumza; yaani kuweka historia yetu kwenye maandishi ni kazi sana..
 
Ni kweli lazima akane Bwana. Unajua kilichompata Dr. Fupi wa Morogoro ambaye alifanya postmoterm? Hii ndiyo Tanzania, hata hivyo katika Tanzania hii tunao viongozi wenye uchungu halisi nanchi yao ambao kwasasa hatunao tena. Wish them RIP.


Prof Shaba ndie alifanya postmortem ya kifo cha sokoine na hakufa labda kama kafa hivi karibuni maana mara ya mwisho nimemwona 1998.Na waliosoma Muhimbili watakuwa wanamjua maana alikuwa akifundisha hapo.
 
Mzee wa Kijijini.

Namkumbuka vilivyo huyu jemedari Moringe Sokoine wakati wa vita vya uhujumu uchumi alikuwa imara kweli kutetea wanyonge.Huyu hastahili kusahauliwa katu kwa kazi yake njema maana amekuwa piawaziri mkuu ktk nchi hii tena kwa vipindi viwili tena wakati chama kikiwa hiki sisiem.Yaani mwaka 1977-80 na Mwaka 1983-84.Huyu jemedari hakuangalia uso wa mtu,kwa kweli tulipoteza mwarubaini wa Taifa hili.

Wakati wa kifo chake Moringe sokoine nakumbuka yule Kijana wake wa kwanza aitwaye LAZARO alikuwa anasoma Cuba.Toka hapo sijasikia kama naye kaingizwa NEC au hata jumuia ya vijana ya sisiem ili kukumbuka mchango wa huyu jemedari.Nyerere akifufuka na kukuta sisiem hii atakufa tena maana imekuwa ya mke na mme na watoto wote NEC.
Wako wapi hawa watoto?huyu LAZARO NA MWINGINE ALIIITWA JOSEPH MORINGE SOKOINE?

Wake zake pale Monduli juu sijui kama wako safi kimaisha maana kipindi kile hakikuwa na mwanya wa kupora kama tunavyoona wake wa marais na mawaziri wakuu wanavyotengeneza mafuko ya fedha ya kuleta maendeleo na pia fursa sawa kwa wanawake wote(ha ha ha),ngoja nicheke kidogo.

Tudumishe mema yote ya MORINGE SOKOINE

CCM NI NGO YA WAKUBWA
 
Kuhani Mkuu,
Kwa kifupi sana hivi ndivyo ajali ilivyotokea. Wakati Sokoine akielekea Dar, msafara wake ulikutana na gari la bwana Dube aliyeamriwa na magari yaliyokuwa mbele ya msafara asimamishe gari lake lakini akakaidi kutii amri hiyo. Kwa hofu kuwa kwa kukaidi kutii amri hiyo bwana Dube anaweza kuwa na nia mbaya, walinzi wake walijulishwa na kutakiwa kuwa makini na gari la Dube. Gari la Dube lilipokaribia lile la Sokoine, kwa kile ambacho hadi leo nakichukulia kuwa ni uzembe, gari moja la walinzi likaingia upande wa bwana Dube ili liende sambamba na la Sokoine kumprotect. Hili lilitokea kwa haraka sana na bila kutarajiwa na Dube. Hivyo ilikuwa Dube apeleke gari lake kushoto porini au akwepe gari la walinzi kwa kukata kulia. Alichofanya Dube ni kukata kulia na hivyo kuvaana na gari alilokuwemo Sokoine. Baada ya ajali hii nakumbuka watu wa Ikulu na magari yao walifanya sana mazoezi kila jioni pale chang'ombe pemebeni mwa uwanja wa Taifa. Sokoine alikuwa kipenzi cha Mwalimu, Asingeuliwa na walinzi bila Mwalimu kuhusika.
 
Prof Shaba ndie alifanya postmortem ya kifo cha sokoine na hakufa labda kama kafa hivi karibuni maana mara ya mwisho nimemwona 1998.Na waliosoma Muhimbili watakuwa wanamjua maana alikuwa akifundisha hapo.


There you are. Huyu Shaba ninamfahamu nashukuru wale wote waliochangia kuhusu hilo hata hivyo kuna mmoja wapo hayuko hai kutokana na hilo. Huyu Prof Shaba mara nyingi ukitaka kumuona nenda Makumbusho, anapenda kunywa pale na mara anakuwa na watu wa Usalama. Full time ni mtu wa kutoa lecture kila analoongea Prof Shaba ni "Shule" Lakini utakuta mara nyingi akianza kugusia masuala fulani fulani yanayohusu kufichua siri fulani hawa watu wa Usalama wanaondoka naye. Anayo mengi sana yule Mzee.
 
Yes, Ilikuwa Prof. Shaba aliyefanya postmortem ya Sokoine.
Dr. Fupi mkemia mkuu "aliyekolimbwa" kabla ya kutoa ushahidi dhidi ya ME kuhusu uagizwaji wa mchele mbovu.

Nakumbuka tulikuwa Umiseta basketball pale Zanaki wakati taarifa ya msiba wa Sokoine inatangazwa RTD!
 
Ni kweli hadi leo Dr Fupi bado ni kigugumizi jinsi alivyofariki, hata mtoto wake hua haelewi hadi leo anasema ni wanasiasa walimmaliza baba yake.. tulisoma nae pale UD ni kijana mpole lakini upole wake unaonekana ni wakurevange siku za baadae....anyways R.I.P wote waliotangulia kwa maslahi ya taifa
(THE GOOD DIE YOUNG-2PAC SHAKUR)
 
...... Nakumbuka siku hiyo, siku ya huzuni. Nilikuwa shule ya msingi darasa la (kapuni), tulikuwa kwenye uwanja wa mpira tunafanya mazoezi. Mwalimu wa michezo alikuwa ametukusanya katikati ya uwanja kwa ajiri ya ushauri fulani hivi tukijiandaa na sherehe za Mei mosi....

.....Ghafla, mwalimu mwenzake akaja mkuku mkuku na kumuita mwalimu wetu wa michezo pembeni kutokana na habari aliyoisikia toka RTD. Tulipatiwa taarifa za msiba ule na kengere ikapigwa kila mmoja akaenda mtarini masaa ya jioni kabla ya kuachiliwa kwenda majumbani na taarifa ya msiba wa Sokoine kutolewa. Mengi yalifanyika kabla ya mei mosi ili kumuenzi marehemu. Maigizo na nyimbo zilitungwa kwa ajili ya kumuenzi. Niishie hapa, ila mengi nayakumbuka pamoja na kuwa nilikuwa bado kinda, hakika ilikuwa siku ya huzuni na machozi. R.I.P. Moringe Sokoine. Amen.


Kalamu, tatizo hawataki kuzungumza; yaani kuweka historia yetu kwenye maandishi ni kazi sana..


Nakumbuka sikumoja unamhoji Salim Ahmed Salim kwenye KLHNews ulijaribu kumsihi naye aandike kitabu.....

Mimi naona wengi wao inawawia vigumu hata kuandika vitabu kutokana na jinsi walivyo jiingiza kwenye makashfa mbalimbali.... yaani kiongozi akiandika kitabu, hachelewi kujikuta anamhukumu mwenziye bila kukusudia..... hili ukichanganya na kule kung'ang'ania kwenye madaraka muda mrefu, ndiyo kabisa kuandika vitabu inakuwa swala la kujiingiza mkenge. Kwa mfano upate biography ya Kingunge, Makamba, Mkapa n.k... dili ngapi utaweza kuzishitukia iwapo kweli kila kitabu kitaandikwa kwa ukweli hata kama majina yatafichwa?....

Wenzetu wameendelea kutokana na kuweka rekodi kakika maandishi.... hata wale wanaopingika katika jamii bado wana biography zao.


SteveD.
 
..Lakini sifa za Sokoine ni zipi? kuna kitu gani ambacho kipo mpaka leo Tanzania na kimetokana na matunda ya utumishi wake uliotukuka?
 
Back
Top Bottom