Ufunuo wa Yohana
JF-Expert Member
- Oct 9, 2007
- 318
- 67
Mimi nijuavyo ni kuwa Dr. Shaba ndite alifanya postmotem ya Moringe na ripoti ilikuwa siri sana kwa kweli. Kwa mara ya kwanza nilimuona Kambarage akitoa machozi hadharani pale Karimjee (bunge la zamani).
Niliambiwa kuwa Lowassa alikuwa na mpango kuwa baada ya Kikwete urais ungehamia Monduli kwa miaka 20 maana yeye angechukua kwa miaka 10 na kisha kumpisha mtoto wa Marehemu Sokoine ambaye yuko Marekanai kwa miaka mingine 10. Wakati yeye (Lowassa) akiwa rais mtoto wa Moringe angekuja kugombea ubunge wa Monduli (ambao angeupata kirahisi kutokana na jina la baba yake) na kisha baadaye kuwa waziri kwa miaka 10 ya uongozi wa Lowassa. Hiyo ingempa uzoefu wa kuwa rais baada ya Lowassa kumaliza kipindi chake.
Sasa mambo kidogo yamebadilika sijui itakuwaje.
Mpango huo haujafa ila umeongeza task kwa wanamipango kwamba ni lazima wamsafishe Lowasa kwanza ili aweze kunadika 2015 kwa wajumbe wa CCM. Hivyo mpango huo haujafa ila umeongeza majukumu tu kwa wanamipango wa mtandao